13-Hadiyth Al-Qudsiy: Mja Hakuonekana Na Kheri Yoyote Isipokuwa Kuamrisha Watu Wasamehe Wenzie

Hadiyth Al-Qudsiy

Hadiyth Ya 13

Mja Hakuonekana Na Kheri Yoyote Isipokuwa Kuamrisha Watu Wasamehe Wenzie

 

 

عَنْ أَبِي مَسْعُودٍ الأنصاري رضي الله عنه قال: قال رسول اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ ((حُوسِبَ رَجُلٌ مِمَّنْ كَانَ قَبْلَكُمْ فَلَمْ يُوجَدْ لَهُ مِنْ الْخَيْرِ شَيْءٌ إِلاَّ أَنَّهُ كَانَ يُخَالِطُ النَّاسَ وَكَانَ مُوسِرًا فَكَانَ يَأْمُرُ غِلْمَانَهُ أَنْ يَتَجَاوَزُوا عَنْ الْمُعْسِرِ قَالَ:  قَالَ اللَّهُ عَزَّ وَجَلَّ : نَحْنُ أَحَقُّ بِذَلِكَ مِنْهُ تَجَاوَزُوا عَنْهُ)) البخاري, مسلم والنسائي

Kutoka kwa Abu Mas’uwd Al-Answaariy (Radhwiya Allaahu ‘anhu) ambaye amesema:   Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Mtu mmoja katika wale waliokutangulieni alitakiwa ajieleze. Hakuonekana na kheri yoyote isipokuwa alikuwa akiamiliana na kuchanganyikana na watu, na alivyokuwa ni tajiri akiwaamrisha wafanyakazi wake wamuachie (wamsamehe) mtu mwenye shida (asilipe deni lake). (Akasema Rasuli) Allaah (‘Azza wa Jalla) Akasema:  Sisi Tuna haki zaidi kuliko yeye kumsamehe)) [Al-Bukhaariy, Muslim na An-Nasaaiy]

 

Share