025-Swahiyh Fiqh As-Sunnah: Mlango Wa Twahara: Wudhuu Taarifu Yake Na Dalili Ya Usharia Wake

 

Swahiyh Fiqh As-Sunnah

 

Mlango Wa Twahara

 

025-Wudhuu Taarifu Yake Na Dalili Ya Usharia Wake

 

Alhidaaya.com

 

 

 

Ama kiistilahi (kitaaluma), ni kutumia maji kwenye viungo maalumu; uso, mikono miwili, kichwa na miguu miwili, ili kuondosha kwayo kinachozuia kuswali na mfano wake.

Uthibiti wake umeashiriwa na Qur-aan, Hadiyth na Ijma’a. Ama katika Qur-aan, Allaah Mtukufu Anasema:

 

((يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِذَا قُمْتُمْ إِلَى الصَّلَاةِ فَاغْسِلُوا وُجُوهَكُمْ وَأَيْدِيَكُمْ إِلَى الْمَرَافِقِ وَامْسَحُوا بِرُءُوسِكُمْ وَأَرْجُلَكُمْ إِلَى الْكَعْبَيْنِ ۚ))

((Enyi walioamini! Mnaposimama kwa ajili ya Swalaah, basi osheni nyuso zenu, na mikono yenu mpaka vifundoni, na mpake vichwa vyenu, na osheni miguu yenu mpaka vifundoni)). [Al-Maaidah (5:6)].

 

 

Ama katika Hadiyth, tunakuta kama vile:

 

1- Hadiyth ya Abuu Hurayrah (Radhi za Allaah ziwe juu yake) aliyesema: “Amesema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

 

((لا تقبل صلاة أحدكم إذا أحدث حتى يتوضأ)) 

((Haikubaliwi Swalaah ya yeyote kati yenu anapokuwa na hadathi mpaka atawadhe)). [Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Al-Bukhaary (135), Muslim (225) na wengineo].

2- Imepokelewa toka kwa Ibn ‘Umar akisema: “Hakika nilimsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema:

 

((لا يقبل الله صلاة بغير طهور، ولا صدقة من غلول))                                      

((Allaah Haikubali Swalaah bila twahara, wala swadaqah ya mali haramu)).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na Muslim (224).

 

 

3- Imepokelewa toka kwa Ibn ‘Abbaas  akisema: “Amesema Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

((إنما أمرت بالوضوء إذا قمت إلى الصلاة))

((Hakika mimi nimeamrishwa kutawadha ninaposimama kuswali)).[Hadiyth Swahiyh. Imefanyiwa “ikhraaj” na At-Tirmidhy (1848), Abuu Daawuud (3760) na An-Nasaaiy ((1/73). Angalia kitabu cha Swahyhul Jaami’i (5761)]. 

 

 

4- Imepokelewa toka kwa Abuu Sa’iyd kwamba Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

 

((مفتاح الصلاة الطهور، وتحريمها التكبير، وتحليلها التسليم))                     

((Ufunguo wa Swalaah ni kujitwaharisha, uingio wake ni Takbiyr, na utokaji wake ni kusema “Assalaamu ‘alaykum wa RahmatuLlaah”)). [Hadiyth Hasan Lighayrih. Imefanyiwa “ikhraaj” na At-Tirmidhy (3), Abuu Daawuud ((60) na Ibn Maajah (275). Al- Albaany katika Swahiyhul Jaami’i ameizingatia kama ni Swahiyh].

 

 

Ama Ijma’a, ni kuwa Maulamaa wa Ummah wamekubaliana kwamba Swalaah haikamiliki ila kwa twahara kama itakuwa ni wepesi kufanya hivyo. [Al-Awsatw cha Ibn Al-Mundhir (1/107)].

 

 

 

Share