03-Imaam Ibn Baaz: Sifa Ya Takbiyr Ayyamut-Tashriyq Tarehe 11-13 Dhul-Hijjah

 

Sifa Ya Takbiyr Ayyamut-Tashriyq Tarehe 11-13 Dhul-Hijjah

 

Imaam Ibn Baaz (Rahimahu Allaah)

 

www.alhidaaya.com

 

 

 

SWALI:

 

Zipi sifa za Takbiyr katika Ayyaamut-Tashriyq na je ni Muqayyad (maalumu iliyofungamanishwa) baada ya Swalaah au Mutwlaq (isiyofungamanishwa)

 

 

JIBU:

 

Takbiyr katika Ayyamut-Tashriyq (Tarehe 11-13 Dhul-Hijjah) ni Mutwlaq (wakati wote) na Muqayyid (wakati maalumu wa kukadirika) baada ya Swalaah  na nyakati zote. Akipenda mtu atamke mara mbili mbili au mara tatu tatu:

 

اللَّهُ أَكْبَرُ، اللَّهُ أَكْبَرُ،  لاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ، اللَّهُ أَكْبَرُ، اللَّهُ أَكْبَرُ، وَلِلَّهِ الْحَمْد

Allaahu Akbar, Allaahu Akbar, laa Ilaaha illa Allaah, Allaahu Akbar Allaahu Akbar WaliLLaahil-Hamd

 

Na azidishie kusema “Laa ilaaha illa Allaah” kwa kusema:

 

لَا إِلَهَ إِلاَّ اللهُ وَحْدَهُ لا شَرِيْكَ لَهُ، لَهُ الـمُلْكُ، ولَهُ الـحَمْدُ، وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيءٍ قَدِير

سُبْحَانَ اللَّهِ ، وَالْحَمْدُ لِلَّهِ ، وَلا إِلَهَ إِلا اللَّهُ ، وَاللَّهُ أَكْبَرُ ، وَلا حَوْلَ وَلا قُوَّةَ إِلا بِاللَّهِ 

 

Na Riwaayah ya Ahmad (Rahimahu Allaah) na Hadiyth ya ibn ‘Umar (Radhwiya Allaahu 'anhu) “Hakuna siku adhimu mbele ya Allaah wala ‘amali Aipendayo zaidi Allaah kama masiku haya basi zidisheni humo At-Tahliyl (Laa ilaaha illa-Allaah), na At-Takbiyr (Allaahu Akbar) na At-Tahmiyd (AlhamduliLLaah).

 

Na ‘Umar (Radhwiya Allaahu 'anhu)  alikuwa akileta takbiyr (Allaahu Akbar) katika khema lake katika masiku ya Minaa mpaka  Takbiyr zinavuma Minaa kama alivyokuwa Ibn ‘Umar na Abuu Huraryah (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) wakitoka katika masikku kumi wakileta takbiyr na watu wakiwafuatilia kwa takbiyr katika masoko, wakiwafundisha watu.

 

[Majmuw’ Fataawaa Wa Maqaalaat Mutanawwi’ah]

 

 

 

Share