32-Fadhila Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): Hatajwi Ila Anaswaliwa (Anaombewa Rahmah Na Amani)

 

 Fadhila Za  Nabiy  (صلى الله عليه وآله وسلم)

32-Hatajwi Ila Anaswaliwa (Anaombewa Rahmah Na Amani)

www.alhidaaya.com

 

 

Kila anapotajwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) Waislamu wanapasa kumswalia, naye Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akakemea asiyefanya hivyo katika Hadiyth:

 

 

 عنْ أبي هُريْرةَ رضي اللَّه عنهُ قال: قال رسُولُ اللَّه صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم: ((رَغِم أنْفُ رجُلٍ ذُكِرْتُ عِنْدَهُ فَلَمْ يُصَلِّ علَيَّ))  رواهُ الترمذي وقالَ : حديثٌ حسنٌ .

Imetoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Amepata khasara mtu ambaye nimetajwa kwake na hakuniswalia)) [At-Tirmidhiy na kasema Hadiyth Hasan]

 

Na pia,

 

 وعن علِيٍّ رضي اللَّه عنْهُ قال: قال رسُولُ اللَّهِ صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم: ((الْبخِيلُ من ذُكِرْتُ عِنْدَهُ فَلَم يُصَلِّ علَيَّ)) رواهُ الترمذي وقالَ : حديثٌ حسنٌ صحيحٌ .

Imetoka kwa 'Aliy (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: ((Bakhili ni yule ambaye nimetajwa kwake na hakuniswalia)) [At-Tirmidhiy na kasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

 

Share