01-Swahiyh Fiqh As-Sunnah: Mlango Wa Zakaah: Taarifu Ya Zakaah

 

Swahiyh Fiqh As-Sunnah

 

Mlango Wa Zakaah

 

01-Taarifu Ya Zakaah

 

Alhidaaya.com

 

 

 

الزكاة “Az-Zakaah” katika lugha, ni “maswdar” ya ((زكا الشيء)) yaani kitu kimekua na kimeongezeka. Hivyo Zakaah ni barakah, ukuaji, utwahara na utengefu. [Al Mu-’ujam Al-Wasiytw]

 

Ama kisharia (kiistilahi), Zakaah ni fungu lililokadiriwa toka mali maalum na katika wakati maalum, na hupewa watu maalum. Fungu hili linalotolewa toka kwenye mali limeitwa “Zakaah” kwa kuwa linaizidishia barakah mali ya asili lilikotolewa, linaistawisha na linailinda na majanga. [Al-Majmuw’u cha An Nawawiy (5/324)]

[Majmuw’u Fataawaa Ibn Taymiyah (8/35) kwa maana yake]

 

Ni kama Anavyosema Ta’aalaa:

((خُذْ مِنْ أَمْوَالِهِمْ صَدَقَةً تُطَهِّرُهُمْ وَتُزَكِّيهِم بِهَا وَصَلِّ عَلَيْهِمْ))

((Chukua katika mali zao Swadaqah, uwatakase na ziwazidishie kwazo na waombee du’aa (na maghfirah)). [At -Tawbah (9:103)]

 

 

 

Share