Tambi Za Kukaanga Na Lozi

Tambi Za Kukaanga Na Lozi

 

Vipimo:

Tambi za kawaida - 1 paketi

Mafuta - 3 vijiko vya supu

Maji - 3 vikombe

Maziwa (carnation milk) - 1 kikombe

Sukari - 1 kikombe

Hiliki - 1/2 kijiko cha chai

Lozi - 1/2 kikombe

Zabibu - 1/2 kikombe

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

  1. Chambua lozi maganda uzikatekate (diced) uweke kando
  2. Tia mafuta katika sufuria, kaanga tambi hadi ziwe nyekundu.
  3. Tia maji, maziwa, sukari, hiliki, nusu ya lozi na zabibu.
  4. Acha zichemke hadi na kukauka zikiwa bado zina maji kidogo, ziepue.
  5. Paka siagi kidogo katika kikaangao (frying pan) iliyo na shimo kidogo (deep).
  6. Mimina tambi katika kikaango.
  7. Didimiza kwa mwiko kuzisawazisha zijifunge katika duara.
  8. Nyunyiza lozi na zabibu zilizobakia juu yake.
  9.  Kata karatasi (kitchen paper)  umbo la duara saizi kidogo kubwa kuliko ya kikaango. Irashie rashie (sprinkle) na maji kidogo iwe maji  maji.
  10. Funika mkate kwa kitchen paper, rudisha katika moto mdogo mdogo kwa muda wa dakika 20, na kutambua kuwa mkate uko tayari ni maji yatakapokauka katika kitchen paper na ikawa kavu.
  11. Epua, toa kitchen paper,  na upindue katika sahani, kisha katakata silesi au upendavyo.

Kidokezo:

Ikiwa huna maziwa ya carnation, tia maziwa ya kawaida vikombe 4 badala yake na badala ya maji.

Share