Wanawake Wanaweza Kungia Katika Ihraam Wakiwa Katika Hedhi?

 

 Wanawake Wanaweza Kungia Katika Ihraam Wakiwa Katika Hedhi?

 

Alhidaaya.com

 

 

Swali:

 

Assalam alaikum warahmatullahi wabarakatu,
 
I had a question. What if someone wants to slaughter but is on their period? Is she allowed to get into ihram?
 
wasalaaam alaikum warahmatullahi wabarakatu..

 

 

Jibu: 

 

AlhamduliLLaah - Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Rabb wa walimwengu, Swalaah na salamu zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

Mwanamke mwenye hedhi anaweza kutia niyyah ya Ihraam kwa sababu Ihraam haimzuii mwanamke mwenye hedhi, ila tu hatoweza kufanya ‘ibaadah ambazo zinajulikana kuwa hazifai kutekelezwa na mwanamke akiwa katika hali hiyo kama Swalaah, kufunga, kutufu Ka’bah n.k kwa dalili zifuatazo:

 

عَنْ جَابِرِ بْنِ عَبْدِ اللَّهِ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا فِي حَدِيثِ أَسْمَاءَ بِنْتِ عُمَيْسٍ حِينَ نُفِسَتْ بِذِي الْحُلَيْفَةِ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ أَمَرَ أَبَا بَكْرٍ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ فَأَمَرَهَا أَنْ تَغْتَسِلَ وَتُهِلَّ    - مسلم

Kutoka kwa Jaabir bin 'Abdillaah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Asmaa bint 'Umays alizaa katika Dhul-Hulayfah, Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamuamrisha Abu Bakar (Radhwiya Allaahu 'anhu) amwambie afanye ghuslu na aingie katika Ihraam)) [Muslim]

 

Pia:

 

عَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا زَوْجِ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَتْ خَرَجْنَا مَعَ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ فِي حَجَّةِ الْوَدَاعِ . . فَقَدِمْتُ مَكَّةَ وَأَنَا حَائِضٌ وَلَمْ أَطُفْ بِالْبَيْتِ وَلا بَيْنَ الصَّفَا وَالْمَرْوَةِ ، فَشَكَوْتُ ذَلِكَ إِلَى النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ فَقَالَ : ((انْقُضِي رَأْسَكِ وَامْتَشِطِي وَأَهِلِّي بِالْحَجِّ )). . . الحديث . ورواه البخاري و مسلم

Kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) mke wa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ambaye amesema: Tulikwenda na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika Hijjatul-Widaa'(Hijjah ya kuaga). Nikaenda Makkah nikiwa katika hedhi na sikuzunguka Nyumba (Ka'bah) au kufanya Sa'y baina ya Asw-Swafaa na Al-Marwah. Nikalalamika kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akaniambia: ((Fungua msuko wa nywele zako na uchane nywele (yaani fanya ghuslu) na ingia katika Ihraam ya Hajj…." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Vile vile:

 

عَنْ ابْنِ عَبَّاسٍ أَنَّ النَّبِيَّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ ((الْحَائِضُ وَالنُّفَسَاءُ إِذَا أَتَتَا عَلَى الْوَقْتِ (أَيْ : الْمِيقَات) تَغْتَسِلانِ وَتُحْرِمَانِ وَتَقْضِيَانِ الْمَنَاسِكَ كُلَّهَا غَيْرَ الطَّوَافِ بِالْبَيْتِ)) رَوَاهُ أَبُو دَاوُد    وصححه الألباني في سنن أبي داود

Na kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhuma) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  amesema: ((Wanawake wenye hedhi na wanawake walio katika damu ya uzazi wakifika Miyqaat [sehemu ya kutilia Ihraam] wafanye ghuslu na waingie katika Ihraam na wafanye taratibu zote isipokuwa twawaaf ya Ka'bah)) [Abuu Daawuwd na imepewa daraja ya Swahiyh na Shaykh Al-Albaaniy katika Swahiyh Abiy Daawuwd (1774)]

 

Kwa hiyo hakuna shaka kuwa wanawake wanaweza kuingia katika Ihraam katika hali yoyote.

 

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

 

 

Share