Kuku Wa Sosi Ya Nyanya Na Dania

Kuku Wa Sosi Ya Nyanya Na Dania

 

Vipimo  

Mafuta - 4 vijiko vya supu 

Kuku - 3 LB

Kitunguu saumu(thomu) na tangawizi iliyosagwa -1 kijiko cha supu

Dania ya unga - 2 vijiko vya supu

Chumvi - kiasi

Pilipili nyekundu ya unga - 1 kijiko cha chai

Bizari ya manjano - 1 kijiko cha chai

Uzile (Bizari ya pilau ya unga/cummin powder ) - 1 kijiko cha chai

Garam masala -  ½ kijiko cha chai

Pilipili mbichi iliyokatwakatwa - 1 au 2

Ndimu - 1 kijiko cha supu

Nyanya ya kopo - 1 kijiko cha supu

Kotmiri - 2 Vijiko vya supu

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

  1. Mkate kuku vipande vikubwa vikubwa, msafishe kwa siki atoke harufu
  2. Mrowanishe na vitu vyote isipokuwa ndimu na nyanya ya kopo kwa muda wa nusu saa au zaidi.
  3. Mtie katika sufuria na mweke jikoni mpaka awive karibia na kukauka mtie nyanya ya kopo na ndimu mwache kidogo kisha muipue.
  4. Mpange kwenye sahani kisha mpambie na vitunguu au chochote.

Kidokezo : 

Nzuri kula na wali kama au mkate au upendavyo.  

 

 

Share