10-Kwa Ajili Ya Allaah Kisha Historia: Uzinduzi 2

 

Kutokana na hayo yaliyo tangulia tumekwisha fahamu ya kuwa khumsi haitolewi kwa mashehe wala wanazuoni ,na limekuwa wazi jambo hili kwetu kufuatia maelezo ya maudhui hii tuliyo yatowa kwa pande zake zote ,na ni vizuri kwetu kuzindua  kua mafakihi na marejeo ya  kidini(wanazuoni) wanadai kuwa wao ni katika Ahlu Bayt,  utamuona moja wao akikuonesha mtiririko wa nasaba yake mpaka kwa kadhim (Alayhis Salaam), jua kwamba ni jambo lisilo wezekana kwa idadi kubwa hii yote ya wanazuoni wa Iraq, Iran, Sirya, Lebanon, nchi za ghuba na Pakistan na nyenginezo kua ni katika Ahlul-Bayt , na kuhesabu wanazuoni wa Iraqi tu ataona kua ni jambo lisilo wezekana kuwa idadi yote hiyo ya wanazuoni wa Iraqi ni katika Ahlul-Bayt , vipi itawezekana tukichanganya na wanazuoni wa miji mingine?bila shaka idadi yao ni kubwa sanasana je itawezekana vipi wote hawa wawe ni katika Ahlul-Bayt ???

 

Na zaidi ya hayo mti  wa nasabu ya mtume unauzwa na kununuliwa hapa chuoni , anaetaka  kuupata  utukufu wa nasabu ya Ahlul Bayt ni juu  yake kuja na dada yake au mke wake kwa sharti awe  mzuri kwa mtukufu mmoja wapo ili astarehe nae,au aje na kiwango cha  mali na atapata utukufu kwa moja kati ya njia mbili hizi:- na hili ni jambo  maarufu hapa chuoni kwetu (CHUO CHA KISHIA CH ANNAJAF).

Kwa ajili hiyo ninasema  yasiwahadae yale ambayo wanayafanya baadhi  ya watukufu,na waandishi wakati anapoweka mmoja  wao mti wa nasaba yake  katika ukurasa wa mbele wa kitabu chake  ni kwa ajili ya kuwahadaa watu wepesiwepesi matajiri na masikini ,ili wampelekee khumsi za mali zao.

 

Na  mwisho wa utafiti wa khumus sitosahau kuitaja kauli ya rafiki yangu mpenzi mshairi hodari Ahmad Al Safy Al Najafiy ambae nilifahamiana nae baada yakupata shahada ya Ijtihadi tukawa marafiki wapenzi achilia mbali tofauti ya umri ilopo kati yetu , kwani alikuwa akinizidi kwa miaka takriban thelathini au zaidi ,nakumbuka alipo niambia mwanangu usiichafuwe nafsi yako kwa mali ya khumsi kwani ni mali ya haramu , na akanidadisi kuhusu khumsi mpaka akanikinaisha kua ni haramu , kisha akanitajia beti za shairi alilokuwa amelitunga kwa ajili hii, ambazo nilizihifadhi kwenye mfuko wangu wa kumbukumbu, na hapa ninazinukuu kwa kwa faida ya wasomaji watukufu kama zilivyo, anasema,

 “Ninawashangaa watu, kuomba omba    kwa   kutumia dini yao  na vipi inawezekana kuomba omba  kwa mtu mwenye nguvu?

 

Basi ikiwa kupata elimu ndio sababu ya kuomba omba  basi itakuwa ujinga ni bora kuliko elimu, na je katika zama za Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) kulikuwa na watu wanaoishi kutegemea mali za watu kwa jina hilo? Na hata kama Mwenyezi Mungu ameifaradhisha zaka basi hakuna kuchukuliwa kwa udhalilishaji basi kwa malengo, wametuletea  watoto wa  sasa ni kazi,na haikua kwa watoto ni geni hilo toka zamani.

Share