Vipapatio Vya Kuku Kwa Sosi Ya Ukwaju

Vipapatio Vya Kuku Kwa Sosi Ya Ukwaju

 

Vipimo

Vipapatio vya Kuku - 1 kilo

Kitunguu saumu (thomu) iliyokunwa - 2 vijiko vya supu

Tangawizi mbichi iliyokunwa - 2 vijiko vya supu

Ndimu - 1

Chumvi - kiasi

Mafuta ya kukaangia - Kiasi

Namna Ya  Kupika. 

  1. Changanya vipatatio na tangawizi mbichi, kitunguu thomu, chumvi, ndimu. Roweka (marinate)  kwa muda kiasi uwezacho.
  2. Tia mafuta katika karai, kaanga vipatatio hadi vigeuke rangi na kuwiva.
  3. Eupa weka katika chujio vichuje mafuta. Kisha weka katika karatasi inayonyonyoa mafuta izidi kuondosha mafuta.
  4. Tayarisha sosi ya Ukwaju 

Vipimo Vya Sosi Ya Ukwaju:

Pilipili mbichi ziliosagwa -3

Bizari ya mchuzi - 2 vijiko vya supu

Bizari ya pilau/jiyra/cumin - 1 kijiko cha chai

Pilipili manga - 1 kijiko cha chai

Ukwaju Ulokamuliwa - 1 kikombe cha chai

Chumvi - kiasi

Namna Ya Kutayarisha:  

  1. Katika kibakuli, tia viungo vyote, changanya vizuri.
  2. Mwagia katika vipatatio uchanganye vizuri.
  3. Weka katika treya ya oveni uvichome kidogo tu kiasi cha kubadilisha rangi ya vipatatio.

 

 

 

Share