Al-Lajnah Ad-Daaimah: Maana Ya At-Tawhiyd Ar-Rubuwbiyyah Na Al-Uluwhiyyah

 

 

Maana Ya At-Tawhiyd Ar-Rubuwbiyyah Na Al-Uluwhiyyah

 

Al-Lajanah Ad-Daaimah

 

Alhidaaya.com

 

SWALI:

 

Nini maana ya Tawhiyd Ar-Rubuwbiyyah na Al-Uluwhiyyah?

 

JIBU:

 

Maana ya Tawhiyd Ar-Rubuwbiyyah (Tawhiyd ya Uola):  Ni mja kumpwekesha Allaah Aliyetukuka na Mtukufu kwa vitendo Vyake kama kuumba, kuanzisha uumbaji,  kuruzuku, kuhuisha na kufisha.

Maana ya Tawhiyd Al-Uluwhiyyah (Tawhiyd ya ‘Ibaadah): Ni mja kumpwekesha Allaah kwa vitendo vyote ‘Ibaadah kama; du’aa, kuomba msaada, kuomba uokozi, kukhofu, kutaraji matumaini, kutawakali, na kila aina za ‘ibaadah.

 

 

Wa biLLaahi at-tawfiyq wa Swalla Allaahu ‘alaa Nabiyyina Muhammad wa aalihi wa Swahbihi wa sallam.

 

Fataawa Al-Lajnah Ad-Daaimah lil-Buhuwth Al-'Ilmiyyah wal-Iftaa. [Juz: 1   Uk. 6-7]

 

 

 

Share