Skip to main content
⌂
Alhidaaya.com homepage
slogan image
  • Log in

left sidebar menu

  • Qur-aan
  • Hadiyth
  • Sunnah
  • Tawhiyd
  • Aqiydah
  • Manhaj
  • Shirki & Kufru
  • Bid-'ah (Uzushi)
  • Salaf Wa Ummah
  • Firaq-Makundi
  • Fiqh-Ibaadah
  • Duaa-Adhkaar
  • Fataawa Za Ulamaa
  • Kauli Za Salaf
  • Akhlaaq-Aadaab
  • Raqaaiq
  • Familia-Jamii
  • Maswali-Majibu
  • Chemsha Bongo
  • Vitabu
  • Mapishi

51-Kitaab At-Tawhiyd: Majina Mazuri Kabisa Ni Ya Allaah Basi Muombeni Kwayo

Mlango Wa 51

باب: وَلِلَّـهِ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ فَادْعُوهُ بِهَا ۖ

Majina Mazuri Kabisa Ni Ya Allaah Basi Muombeni Kwayo


قَوْلُ اَللَّهِ تَعَالَى:

Kauli ya Allaah Ta’aalaa:

وَلِلَّـهِ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ فَادْعُوهُ بِهَا ۖ وَذَرُوا الَّذِينَ يُلْحِدُونَ فِي أَسْمَائِهِ ۚ  

((Na Allaah Ana Majina Mazuri kabisa, basi muombeni kwayo. Na waacheni wale wanamili katika kukadhibisha Majina Yake)) [Al-A’raaf (7: 180)]

ذَكَرَ اِبْنُ أَبِي حَاتِمٍ عَنِ اِبْنِ عَبَّاسٍ: ((يُلْحِدُونَ فِي أَسْمَائِهِ ۚ)): يُشْرِكُونَ.

Ibn Haatim ametaja kwamba Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) amesema kuhusu: ((Wanamili katika kukadhibisha Majina Yake)) yaani: wanafanya shirki.

وَعَنْهُ: سَمُّوا اَللاَّتَ مِنَ الإِلَهِ وَالْعُزَّى مِنَ الْعَزِيزِ.

Na kasema pia: “Wamewaita Al-Laata – kutokana na ‘Ilaah’. Na Al-Uzzah kutokana na ‘Al-‘Aziyz’.

وَعَنِ الأَعْمَشِ: يُدْخِلُونَ فِيهَا مَا لَيْسَ مِنْهَا

Na Al-A’mash kasema: “Wanaingiza humo (katika Majina ya Allaah, Majina) yasiyokuwemo.”

Masuala Muhimu Yaliyomo:

1-Kuthibitisha Majina ya Allaah (سبحانه وتعالى) kama Alivyosema (Al-A’raaf 7: 180).

2-Majina yote ya Allaah (سبحانه وتعالى) ni mazuri.

3-Maamrisho ya kumuomba Allaah (سبحانه وتعالى) kwa Majina Yake Mazuri.

4-Amri ya kuepukana na majahili na wakanushaji.   

5-Maelezo ya wanavyopotoa na kuharibu Majina ya Allaah (سبحانه وتعالى).

6-Adhabu imeahidiwa kwa wapotoshaji Majina ya Allaah (سبحانه وتعالى).


Book traversal links for Kitaab At-Tawhiyd (Word Doc) Chapisho La 2 Kimehaririwa 1438H (2017M)

  • ‹ 50-Kitaab At-Tawhiyd: Kuharamishwa Majina Yanayoabudiwa Badala Ya Allaah
  • Up
  • 52-Kitaab At-Tawhiyd: Haisemwi “Assalaamu ‘Ala-Allaah” ›
moon-icon

Mafunzo Katika Miezi Ya Hijri Ya Kutekeleza Na Ya Kujiepusha

  • Muharram
    image
    مُحَرَّمْ
  • Swafar
    image
    صَفَرْ
  • Rabiy’u Al-Awwal
    Rabiy’u Al-Awwal
    رَبيعُ الْأَوًّلْ
  • Rabiy'u Al-Aakhir
    Rabiy'u Al-Aakhir
    رَبيعُ الآخِرْ
  • Jumaadaa Al-Uwlaa
    image
    جُمَادَى الْأُوْلَى
  • Jumaadaa Al-Aakhirah
    image
    جُمَادَى الْآخِرَة
  • Rajab
    image
    رَجَبْ
  • Sha'baan
    Shabaan
    شَعْبَانْ
  • Ramadhwaan
    iocn
    رَمَضَانْ
  • Shawwaal
    image
    شَوّالْ
  • Dhul-Qa’dah
    image
    ذُو الْقَعْدَةْ
  • Dhul-Hijjah
    icon
    ذُو الحِجَّةْ
Alhidaaya.com homepage
  • Kuhusu Alhidaaya
  • Maoni Yako-Wasiliana Na sisi (Contact Us)
  • Tovuti Muhimu

© 2026 Alhidaaya.com All rights reserved.