Makala Za Qur-aan

Makala Za Qur-aan

Makala Za Qur-aan

 

Hatari Ya Kuihama Qur-aan

Alhidaaya.com

 

 

Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa)  Anatuambia jinsi Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Alivyokuwa akilalamika kuwa watu wake wameihama na kuipuuza Qur-aan:

 

وَقَالَ الرَّسُولُ يَا رَبِّ إِنَّ قَوْمِي اتَّخَذُوا هَـٰذَا الْقُرْآنَ مَهْجُورًا ﴿٣٠﴾

Na Rasuli akasema: “Rabb wangu! Hakika watu wangu wameifanya hii Qur-aan yenye kuhamwa. [Al-Furqaan: 30]

 

 

Makafiri Quraysh walikuwa hawataki kusikiliza Qur-aan, na ilipokuwa ikisomwa walikuwa wakizungumza upuuzi au kuzungumza kwa sauti za juu mazungumzo mengine ili wasiisikie.    

 

وَقَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا لَا تَسْمَعُوا لِهَـٰذَا الْقُرْآنِ وَالْغَوْا فِيهِ لَعَلَّكُمْ تَغْلِبُونَ﴿٢٦﴾

 Na wale waliokufuru wakasema: “Msiisikilize hii Qur-aan na ifanyieni rabsha huenda mkashinda.” [Fusswilat: 26] 

 

Hali hii ya kuipuuza Qur-aan vile vile iko miongoni mwa Waislamu, ingawa Waislamu tofauti yake ni kuwa wameiamini na sio kama Makafiri Quraysh ambao ilikuwa ni dhaahiri  kuwa waliikanusha na kutoiamini.

 

Wafasiri Wa Qur-aan wameifafanua Aayah hiyo ya kwanza kuhusu: