Makala Za Qur-aan
Makala Za Qur-aan
Sifa Kumi Za Waumini Katika Suwrah Al-Ahzaab
Hatari Ya Kuihama Qur-aan
Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anatuambia jinsi Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) Alivyokuwa akilalamika kuwa watu wake wameihama na kuipuuza Qur-aan:
وَقَالَ الرَّسُولُ يَا رَبِّ إِنَّ قَوْمِي اتَّخَذُوا هَـٰذَا الْقُرْآنَ مَهْجُورًا ﴿٣٠﴾
Na Rasuli akasema: “Rabb wangu! Hakika watu wangu wameifanya hii Qur-aan yenye kuhamwa. [Al-Furqaan: 30]
Makafiri Quraysh walikuwa hawataki kusikiliza Qur-aan, na ilipokuwa ikisomwa walikuwa wakizungumza upuuzi au kuzungumza kwa sauti za juu mazungumzo mengine ili wasiisikie.
وَقَالَ الَّذِينَ كَفَرُوا لَا تَسْمَعُوا لِهَـٰذَا الْقُرْآنِ وَالْغَوْا فِيهِ لَعَلَّكُمْ تَغْلِبُونَ﴿٢٦﴾
Na wale waliokufuru wakasema: “Msiisikilize hii Qur-aan na ifanyieni rabsha huenda mkashinda.” [Fusswilat: 26]
Hali hii ya kuipuuza Qur-aan vile vile iko miongoni mwa Waislamu, ingawa Waislamu tofauti yake ni kuwa wameiamini na sio kama Makafiri Quraysh ambao ilikuwa ni dhaahiri kuwa waliikanusha na kutoiamini.
Wafasiri Wa Qur-aan wameifafanua Aayah hiyo ya kwanza kuhusu:
Maamrisho Ya Kuisoma Qur-aan Na Kuifanyia Kazi
Allaah ('Azza wa Jalla) Alimuamrisha kwanza Rasuli Wake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na hivyo ni amri kwa Waumini wote pia:
Ni Zipi Suwrah Zinazojulikana Kama:
As-Sab’u Atw-Twiwaal, Al-Mathaaniy, Al-Mufasw-swal Na Al-Mi-iyn
Fadhila Za Kusoma Na Kuhifadhi Qur-aan Katika Hadiyth Za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)
Fadhila Za Qur-aan Na Umuhimu Wake: Aayaat Za Qur-aan
1-Qur-aan imejaa Baraka za Allaah ('Azza wa Jalla).
Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):