Asbaabun-Nuzuwl

Asbaabun-Nuzuwl

Asbaabun-Nuzuwl

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

Al-Munaafiquwn Aayah 1 - 8

 

 Kauli za Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِذَا جَاءَكَ الْمُنَافِقُونَ قَالُوا نَشْهَدُ إِنَّكَ لَرَسُولُ اللَّـهِ ۗ وَاللَّـهُ يَعْلَمُ إِنَّكَ لَرَسُولُهُ وَاللَّـهُ يَشْهَدُ إِنَّ الْمُنَافِقِينَ لَكَاذِبُونَ﴿١﴾

1. Watakapokujia (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) wanafiki wakisema: Tunashuhudia kwamba wewe bila shaka ni Rasuli wa Allaah. Na Allaah Anajua kuwa wewe ni Rasuli Wake, na Allaah Anashuhudia kuwa hakika wanafiki ni waongo.

 

Na:

 

هُمُ الَّذِينَ يَقُولُونَ لَا تُنفِقُوا عَلَىٰ مَنْ عِندَ رَسُولِ اللَّـهِ حَتَّىٰ يَنفَضُّوا ۗ وَلِلَّـهِ خَزَائِنُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَلَـٰكِنَّ الْمُنَافِقِينَ لَا يَفْقَهُونَ﴿٧﴾

7. Wao ndio wale wasemao: Msitoe mali kwa ajili ya walioko kwa Rasuli wa Allaah mpaka waondokelee mbali.  Na ilhali ni za Allaah Pekee hazina za mbingu na ardhi, lakini wanafiki hawafahamu.

 

يَقُولُونَ لَئِن رَّجَعْنَا إِلَى الْمَدِينَةِ لَيُخْرِجَنَّ الْأَعَزُّ مِنْهَا الْأَذَلَّ ۚ وَلِلَّـهِ الْعِزَّةُ وَلِرَسُولِهِ وَلِلْمُؤْمِنِينَ وَلَـٰكِنَّ الْمُنَافِقِينَ لَا يَعْلَمُونَ﴿٨﴾

8. Wanasema: Tutakaporudi Madiynah, mwenye hadhi zaidi bila shaka atamfukuza humo aliye dhalili. Na ilhali utukufu ni wa Allaah na wa Rasuli Wake na wa Waumini, lakini wanafiki hawajui.

 

Sababun-Nuzuwl:

 

عَنْ زَيْدِ بْنِ أَرْقَمَ ـ رضى الله عنه ـ قَالَ كُنْتُ مَعَ عَمِّي فَسَمِعْتُ عَبْدَ اللَّهِ بْنَ أُبَىٍّ ابْنَ سَلُولَ يَقُولُ لاَ تُنْفِقُوا عَلَى مَنْ عِنْدَ رَسُولِ اللَّهِ حَتَّى يَنْفَضُّوا‏.‏ وَقَالَ أَيْضًا لَئِنْ رَجَعْنَا إِلَى الْمَدِينَةِ لَيُخْرِجَنَّ الأَعَزُّ مِنْهَا الأَذَلَّ‏.‏ فَذَكَرْتُ ذَلِكَ لِعَمِّي فَذَكَرَ عَمِّي لِرَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَأَرْسَلَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم إِلَى عَبْدِ اللَّهِ بْنِ أُبَىٍّ وَأَصْحَابِهِ، فَحَلَفُوا مَا قَالُوا، فَصَدَّقَهُمْ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم وَكَذَّبَنِي، فَأَصَابَنِي هَمٌّ لَمْ يُصِبْنِي مِثْلُهُ، فَجَلَسْتُ فِي بَيْتِي، فَأَنْزَلَ اللَّهُ عَزَّ وَجَلَّ: ((إِذَا جَاءَكَ الْمُنَافِقُونَ‏))‏ إِلَى قَوْلِهِ: ((‏هُمُ الَّذِينَ يَقُولُونَ لاَ تُنْفِقُوا عَلَى مَنْ عِنْدَ رَسُولِ اللَّهِ‏)) ‏ إِلَى قَوْلِهِ: ((‏لَيُخْرِجَنَّ الأَعَزُّ مِنْهَا الأَذَلَّ‏))‏ فَأَرْسَلَ إِلَىَّ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَقَرَأَهَا عَلَىَّ ثُمَّ قَالَ ‏"‏ إِنَّ اللَّهَ قَدْ صَدَّقَكَ ‏"‏‏.‏

Zaid bin Arqam (رضي الله عنه) amehadithia kwamba: Nilipokuwa pamoja na ‘Ammi yangu nilimsikia ‘Abdullaah bin Ubayy Ibn Masluwl (Mnafiki mkuu) akisema:  Msitoe mali kwa ajili ya walioko kwa Rasuli wa Allaah mpaka waondokelee mbali.” Na akasema pia: “Tutakaporudi Madiynah, mwenye hadhi zaidi atamfukuza humo aliye dhalili.” Nikamtajia  hayo ‘Ammi yangu na ‘Ammi yangu akamwelezea Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) kisha Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  akamwita ‘Abdullaah ibn Ubayy na Maswahaba zake (kuwauliza), wakaapa kuwa hawakusema hivyo. Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  akawasadikisha na badala yake akanikadhibisha. Ikanigubika ghamu ambayo sikuwahi kuipata mfano wake. Nikabakia nyumbani kwangu (kuogopa nisiitwe muongo) kisha hapo Allaah (عزّ وجلّ) Akateremsha:

إِذَا جَاءَكَ الْمُنَافِقُونَ قَالُوا نَشْهَدُ إِنَّكَ لَرَسُولُ اللَّـهِ ۗ  

 

Watakapokujia (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) wanafiki wakisema: Tunashuhudia kwamba wewe bila shaka ni Rasuli wa Allaah.

 

Mpaka kauli Yake Allaah (سبحانه وتعالى):

 

هُمُ الَّذِينَ يَقُولُونَ لَا تُنفِقُوا عَلَىٰ مَنْ عِندَ رَسُولِ اللَّـهِ حَتَّىٰ يَنفَضُّوا ۗ وَلِلَّـهِ خَزَائِنُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَلَـٰكِنَّ الْمُنَافِقِينَ لَا يَفْقَهُونَ﴿٧﴾

7. Wao ndio wale wasemao: Msitoe mali kwa ajili ya walioko kwa Rasuli wa Allaah mpaka waondokelee mbali.  Na ilhali ni za Allaah Pekee hazina za mbingu na ardhi, lakini wanafiki hawafahamu.

 

Mpaka kauli Yake Allaah (سبحانه وتعالى):

  لَيُخْرِجَنَّ الْأَعَزُّ مِنْهَا الْأَذَلَّ ۚ  

mwenye hadhi zaidi bila shaka atamfukuza humo aliye dhalili.  

 

Kisha Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  akaniita na kunisomea kisha akasema:  ((Allaah Amesadikisha kauli yako)). [Al-Bukhaariy Kitaab At-Tafsiyr]

 

Riwaayah nyengine ni kama ifuatavyo: (pamoja na Aayah zinazohusiana na kisa hicho):

 

 

Asbaabun-Nuzuwl

 أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

At-Taghaabun:  14

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

  يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّ مِنْ أَزْوَاجِكُمْ وَأَوْلَادِكُمْ عَدُوًّا لَّكُمْ فَاحْذَرُوهُمْ ۚ وَإِن تَعْفُوا وَتَصْفَحُوا وَتَغْفِرُوا فَإِنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ﴿١٤﴾

Enyi walioamini! Hakika miongoni mwa wake zenu na watoto wenu ni maadui kwenu, basi tahadharini nao. Na mkisamehe na mkapuuza na mkayafutilia mbali, basi hakika Allaah ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu. [At-Taghaabun: 14]

 

Sababun-Nuzuwl: 

 

عَنْ عِكْرِمَةَ، عَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ، وَسَأَلَهُ، رَجُلٌ عَنْ هَذِهِ الآيَةِ: ((يا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّ مِنْ أَزْوَاجِكُمْ وَأَوْلاَدِكُمْ عَدُوًّا لَكُمْ فَاحْذَرُوهُمْ)) ‏ قَالَ: هَؤُلاَءِ رِجَالٌ أَسْلَمُوا مِنْ أَهْلِ مَكَّةَ وَأَرَادُوا أَنْ يَأْتُوا النَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم فَأَبَى أَزْوَاجُهُمْ وَأَوْلاَدُهُمْ أَنْ يَدَعُوهُمْ أَنْ يَأْتُوا رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَلَمَّا أَتَوْا رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم رَأَوُا النَّاسَ قَدْ فَقِهُوا فِي الدِّينِ هَمُّوا أَنْ يُعَاقِبُوهُمْ فَأَنْزَلَ اللَّهُ عَزَّ وَجَل َ‏:‏ ((يا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّ مِنْ أَزْوَاجِكُمْ وَأَوْلاَدِكُمْ عَدُوًّا لَكُمْ فَاحْذَرُوهُمْ ...)) ‏ الآيَةَ ‏.‏ قَالَ أَبُو عِيسَى هَذَا حَدِيثٌ حَسَنٌ صَحِيحٌ ‏.‏

 

Ikrimah (رضي الله عنه) amehadithia kwamba Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) aliulizwa na mtu mmoja kuhusu Aayah hii:

 

  يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّ مِنْ أَزْوَاجِكُمْ وَأَوْلَادِكُمْ عَدُوًّا لَّكُمْ فَاحْذَرُوهُمْ ۚ وَإِن تَعْفُوا وَتَصْفَحُوا وَتَغْفِرُوا فَإِنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ﴿١٤﴾

Enyi walioamini! Hakika miongoni mwa wake zenu na watoto wenu ni maadui kwenu, basi tahadharini nao.

 

Akasema: Hao ni wanaume wa Makkah waliosilimu  wakata kwenda (kuhajiri) kwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) lakini wake zao na watoto wao wakakataa kuwaruhusu kwenda (kuhajiri) kwa kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم). Walipofika kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) waliona (yaani Muhaajiriyna waliowatangulia kuhajiri) kuwa watu wamepata ufahamu wa kina wa Dini, hapo wakadhamiria kuwatia adabu (familia zao). Hapo Allaah (عزّ وجلّ) Akateremsha: 

 

  يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّ مِنْ أَزْوَاجِكُمْ وَأَوْلَادِكُمْ عَدُوًّا لَّكُمْ فَاحْذَرُوهُمْ ۚ وَإِن تَعْفُوا وَتَصْفَحُوا وَتَغْفِرُوا فَإِنَّ اللَّـهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ﴿١٤﴾

Enyi walioamini! Hakika miongoni mwa wake zenu na watoto wenu ni maadui kwenu, basi tahadharini nao. Na mkisamehe na mkapuuza na mkayafutilia mbali, basi hakika Allaah ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu. [At-Taghaabun: 14]

 

[At-Tirmidhiy na ameipa daraja ya Hasan Imaam Al-Albaaniy katika Swahiyh At-Tirmidhiy [3317]

 

Asbaabun-Nuzuwl

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

At-Tahriym Aayah 4-5

 

Kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِن تَتُوبَا إِلَى اللَّـهِ فَقَدْ صَغَتْ قُلُوبُكُمَا ۖ وَإِن تَظَاهَرَا عَلَيْهِ فَإِنَّ اللَّـهَ هُوَ مَوْلَاهُ وَجِبْرِيلُ وَصَالِحُ الْمُؤْمِنِينَ ۖ وَالْمَلَائِكَةُ بَعْدَ ذَٰلِكَ ظَهِيرٌ﴿٤﴾

4. Ikiwa nyinyi wawili mtatubia kwa Allaah (ni kheri kwenu) kwani kwa hakika nyoyo zenu zimeelemea (yanayomchukiza Nabiy صلى الله عليه وآله وسلم). Na mkisaidiana dhidi yake, basi hakika Allaah Ndiye Mlinzi Msaidizi wake na Jibriyl na Waumini wema, na zaidi ya hayo, Malaika pia watasaidia.

 

 

 

عَسَىٰ رَبُّهُ إِن طَلَّقَكُنَّ أَن يُبْدِلَهُ أَزْوَاجًا خَيْرًا مِّنكُنَّ مُسْلِمَاتٍ مُّؤْمِنَاتٍ قَانِتَاتٍ تَائِبَاتٍ عَابِدَاتٍ سَائِحَاتٍ ثَيِّبَاتٍ وَأَبْكَارًا﴿٥﴾

5. Akikutalikini, asaa Rabb Wake Akambadilishia wake bora kuliko nyinyi; Waislamu, Waumini, watiifu na wanyenyekevu, wanaotubia, wenye kufanya ‘ibaadah, wanaofunga Swiyaam au wanaohajiri kwa ajili ya Allaah, wajane, na walio bikra.

 

Sababun-Nuzuwl:

 

عن عمر بن الخطاب رضي الله عنه ، قَالَ لَمَّا اعْتَزَلَ نَبِيُّ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم نِسَاءَهُ  قَالَ: دَخَلْتُ الْمَسْجِدَ فَإِذَا النَّاسُ يَنْكُتُونَ بِالْحَصَى وَيَقُولُونَ: طَلَّقَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم نِسَاءَهُ وَذَلِكَ قَبْلَ أَنْ يُؤْمَرْنَ بِالْحِجَابِ فَقَالَ عُمَرُ: فَقُلْتُ لأَعْلَمَنَّ ذَلِكَ الْيَوْمَ قَالَ فَدَخَلْتُ عَلَى عَائِشَةَ فَقُلْتُ: يَا بِنْتَ أَبِي بَكْرٍ أَقَدْ بَلَغَ مِنْ شَأْنِكِ أَنْ تُؤْذِي رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم؟ فَقَالَتْ: مَا لِي وَمَا لَكَ يَا ابْنَ الْخَطَّابِ عَلَيْكَ بِعَيْبَتِكَ ‏.‏ قَالَ: فَدَخَلْتُ عَلَى حَفْصَةَ بِنْتِ عُمَرَ فَقُلْتُ لَهَا: يَا حَفْصَةُ أَقَدْ بَلَغَ مِنْ شَأْنِكِ أَنْ تُؤْذِي رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم وَاللَّهِ لَقَدْ عَلِمْتِ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم لاَ يُحِبُّكِ ‏ وَلَوْلاَ أَنَا لَطَلَّقَكِ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏.‏ فَبَكَتْ أَشَدَّ الْبُكَاءِ فَقُلْتُ لَهَا: أَيْنَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم؟ قَالَتْ: هُوَ فِي خِزَانَتِهِ فِي الْمَشْرُبَةِ ‏.‏ فَدَخَلْتُ فَإِذَا أَنَا بِرَبَاحٍ غُلاَمِ رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَاعِدًا عَلَى أُسْكُفَّةِ الْمَشْرُبَةِ مُدَلٍّ رِجْلَيْهِ عَلَى نَقِيرٍ مِنْ خَشَبٍ وَهُوَ جِذْعٌ يَرْقَى عَلَيْهِ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم وَيَنْحَدِرُ فَنَادَيْتُ: يَا رَبَاحُ اسْتَأْذِنْ لِي عِنْدَكَ عَلَى رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏.‏ فَنَظَرَ رَبَاحٌ إِلَى الْغُرْفَةِ ثُمَّ نَظَرَ إِلَىَّ فَلَمْ يَقُلْ شَيْئًا ثُمَّ قُلْتُ: يَا رَبَاحُ اسْتَأْذِنْ لِي عِنْدَكَ عَلَى رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏.‏ فَنَظَرَ رَبَاحٌ إِلَى الْغُرْفَةِ ثُمَّ نَظَرَ إِلَىَّ فَلَمْ يَقُلْ شَيْئًا ثُمَّ رَفَعْتُ صَوْتِي فَقُلْتُ: يَا رَبَاحُ اسْتَأْذِنْ لِي عِنْدَكَ عَلَى رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَإِنِّي أَظُنُّ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم ظَنَّ أَنِّي جِئْتُ مِنْ أَجْلِ حَفْصَةَ وَاللَّهِ لَئِنْ أَمَرَنِي رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم بِضَرْبِ عُنُقِهَا لأَضْرِبَنَّ عُنُقَهَا ‏.‏ وَرَفَعْتُ صَوْتِي فَأَوْمَأَ إِلَىَّ أَنِ ارْقَهْ فَدَخَلْتُ عَلَى رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم وَهُوَ مُضْطَجِعٌ عَلَى حَصِيرٍ فَجَلَسْتُ فَأَدْنَى عَلَيْهِ إِزَارَهُ وَلَيْسَ عَلَيْهِ غَيْرُهُ وَإِذَا الْحَصِيرُ قَدْ أَثَّرَ فِي جَنْبِهِ فَنَظَرْتُ بِبَصَرِي فِي خِزَانَةِ رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَإِذَا أَنَا بِقَبْضَةٍ مِنْ شَعِيرٍ نَحْوِ الصَّاعِ وَمِثْلِهَا قَرَظًا فِي نَاحِيَةِ الْغُرْفَةِ وَإِذَا أَفِيقٌ مُعَلَّقٌ – قَالَ: فَابْتَدَرَتْ عَيْنَاىَ قَالَ: ((مَا يُبْكِيكَ يَا ابْنَ الْخَطَّابِ)) ‏.‏ قُلْتُ: يَا نَبِيَّ اللَّهِ وَمَا لِي لاَ أَبْكِي وَهَذَا الْحَصِيرُ قَدْ أَثَّرَ فِي جَنْبِكَ وَهَذِهِ خِزَانَتُكَ لاَ أَرَى فِيهَا إِلاَّ مَا أَرَى وَذَاكَ قَيْصَرُ وَكِسْرَى فِي الثِّمَارِ وَالأَنْهَارِ وَأَنْتَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم وَصَفْوَتُهُ وَهَذِهِ خِزَانَتُكَ ‏.‏ فَقَالَ: ((يَا ابْنَ الْخَطَّابِ أَلاَ تَرْضَى أَنْ تَكُونَ لَنَا الآخِرَةُ وَلَهُمُ الدُّنْيَا)) ‏.‏ قُلْتُ: بَلَى - قَالَ : وَدَخَلْتُ عَلَيْهِ حِينَ دَخَلْتُ وَأَنَا أَرَى فِي وَجْهِهِ الْغَضَبَ فَقُلْتُ: يَا رَسُولَ اللَّهِ مَا يَشُقُّ عَلَيْكَ مِنْ شَأْنِ النِّسَاءِ فَإِنْ كُنْتَ طَلَّقْتَهُنَّ فَإِنَّ اللَّهَ مَعَكَ وَمَلاَئِكَتَهُ وَجِبْرِيلَ وَمِيكَائِيلَ وَأَنَا وَأَبُو بَكْرٍ وَالْمُؤْمِنُونَ مَعَكَ وَقَلَّمَا تَكَلَّمْتُ وَأَحْمَدُ اللَّهَ بِكَلاَمٍ إِلاَّ رَجَوْتُ أَنْ يَكُونَ اللَّهُ يُصَدِّقُ قَوْلِي الَّذِي أَقُولُ وَنَزَلَتْ هَذِهِ الآيَةُ آيَةُ التَّخْيِيرِ: ((عَسَى رَبُّهُ إِنْ طَلَّقَكُنَّ أَنْ يُبْدِلَهُ أَزْوَاجًا خَيْرًا مِنْكُنَّ...)) ))وَإِنْ تَظَاهَرَا عَلَيْهِ فَإِنَّ اللَّهَ هُوَ مَوْلاَهُ وَجِبْرِيلُ وَصَالِحُ الْمُؤْمِنِينَ وَالْمَلاَئِكَةُ بَعْدَ ذَلِكَ ظَهِيرٌ‏(( وَكَانَتْ عَائِشَةُ بِنْتُ أَبِي بَكْرٍ وَحَفْصَةُ تَظَاهَرَانِ عَلَى سَائِرِ نِسَاءِ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم فَقُلْتُ يَا رَسُولَ اللَّهِ أَطَلَّقْتَهُنَّ؟ قَالَ: ((لاَ))   قُلْتُ يَا رَسُولَ اللَّهِ إِنِّي دَخَلْتُ الْمَسْجِدَ وَالْمُسْلِمُونَ يَنْكُتُونَ بِالْحَصَى يَقُولُونَ طَلَّقَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم نِسَاءَهُ أَفَأَنْزِلُ فَأُخْبِرَهُمْ أَنَّكَ لَمْ تُطَلِّقْهُنَّ؟ قَالَ: ((نَعَمْ إِنْ شِئْتَ))‏ فَلَمْ أَزَلْ أُحَدِّثُهُ حَتَّى تَحَسَّرَ الْغَضَبُ عَنْ وَجْهِهِ وَحَتَّى كَشَرَ فَضَحِكَ وَكَانَ مِنْ أَحْسَنِ النَّاسِ ثَغْرًا ثُمَّ نَزَلَ نَبِيُّ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم وَنَزَلْتُ فَنَزَلْتُ أَتَشَبَّثُ بِالْجِذْعِ وَنَزَلَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم كَأَنَّمَا يَمْشِي عَلَى الأَرْضِ مَا يَمَسُّهُ بِيَدِهِ فَقُلْتُ يَا رَسُولَ اللَّهِ إِنَّمَا كُنْتَ فِي الْغُرْفَةِ تِسْعَةً وَعِشْرِينَ ‏.‏ قَالَ: ((إِنَّ الشَّهْرَ يَكُونُ تِسْعًا وَعِشْرِينَ)) فقُمْتُ عَلَى بَابِ الْمَسْجِدِ فَنَادَيْتُ بِأَعْلَى صَوْتِي لَمْ يُطَلِّقْ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم نِسَاءَهُ ‏.‏ وَنَزَلَتْ هَذِهِ الآيَةُ :‏ ((وَإِذَا جَاءَهُمْ أَمْرٌ مِنَ الأَمْنِ أَوِ الْخَوْفِ أَذَاعُوا بِهِ وَلَوْ رَدُّوهُ إِلَى الرَّسُولِ وَإِلَى أُولِي الأَمْرِ مِنْهُمْ لَعَلِمَهُ الَّذِينَ يَسْتَنْبِطُونَهُ مِنْهُمْ‏))‏ فَكُنْتُ أَنَا اسْتَنْبَطْتُ ذَلِكَ الأَمْرَ وَأَنْزَلَ اللَّهُ عَزَّ وَجَلَّ آيَةَ التَّخْيِيرِ ‏.‏

 

Kutoka kwa ‘Umar bin Al-Khatwaab (رضي الله عنه) amesema: Pindi Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)  alipojitenga na wake zake, niliingia Msikitini nikaona watu wanapiga ardhi kwa vijiwe huku wakisema: “Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  amewataliki wake zake.” Hivyo ilikuwa kabla ya kuamrishwa kwao hijaab. Nikasema ndani ya nafsi yangu: “Nitalijua hilo leo.” Akasema: Akaingia kwa ‘Aaishah akasema: “Ee binti wa Abuu Bakr hivi umefikia kumuudhi Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)?”  ‘Aaishah akasema:  “Una nini ee Ibn Al-Khatwaab  shughulika na ya kwako.” (Yaani kampe mawaidha haya mwanao Hafswa). Akasema: “Nikaingia kwa Hafswah nikamwambia: “Ee Hafswah, hivi umefikia kumuudhi Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم), na ilhali umeshajua kuwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  hakupendi na lau si mimi basi Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) angelikutaliki.”   Hafswah akalia kilio kikubwa (cha uchungu) nikamuuliza: “Yuko wapi Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)?” Akasema: “Yupo darini.” Nikaingia nikamkuta Rabaah ghulamu wa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akiwa amekaa katika ukingo wa dirisha akining’iniza mguu wake katika kipande cha mbao cha gogo la mtende ambacho huwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  akilitumia na kupandia (kuingia chumbanii mwake) na kuteremkia. Nikaita: “Ee Rabaah! Niombee ruhusa kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم).” Rabaah akaangalia chumbani kisha akaniangalia mimi na hakusema kitu. Kisha nikamuita tena nikasema: “Ee Rabaah niombee ruhusa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم).”  Rabaah akaangalia chumbani kisha akaniangalia mimi na hakusema chochote. Kisha nikanyanyua sauti  yangu na kusema: “Ee Rabaah niombee ruhusa kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  kwa hakika mimi nadhani kuwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) anajua kuwa nimekuja kuhusiana na  Hafaswah,  Wa-Allaahi pindi Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akiniamrisha niikate shingo yake (nimuue), basi hakika mimi nitaikata!” Nikapandisha sauti yangu akaniashiria nipande, nikaingia kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  (nikamkuta) akiwa amelala kwa ubavu juu ya mkeka. Nikakaa, na (Rabaah) akamsogezea izari yake, na hana nyingine zaidi ya hiyo. Nikagutuka kuona alama za mkeka zimechora kwenye ubavu wake. Halafu nikapembua kwa jicho langu kwenye stoo ya Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  na nikastuka kuona shayiri kiasi cha pishi moja ya kujaa kiganja cha mkono na kiasi kama hicho hicho cha gundi upande wa chumba ambako kuna ngozi mbichi imetundikwa (upande mmoja). Hapo hapo macho yangu yakatiririka machozi. Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema:   ((Kinakuliza nini ee Ibn Al-Khattwaab?)) Nikasema: “Ee Nabiy wa Allaah, kwanini nisilie ilhali huu mkeka umekufanyia alama mwilini mwako na khazana (stoo) yako sioni kilichomo ila kile ninachokiona na ilhali kule kuna (Wafalme) Qayswar (Ceaser) na  Kisraa  wana matunda na mito (wanaishi kifakhari), basi vipi iwe wewe Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  ambaye Allaah Amekuchagua (huna lolote)  hii ndio khazana yako?”  Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: ((Ee Ibn Al-Khattwaab  je huridhii sisi tukawa na Aakhirah na wao wakawa na dunia?)). Nikasema: “Naam!” (nakubaliana nawe). Nilipoingia kwake nikaona ghadhabu usoni mwake. Nikasema: “Ee Rasuli wa Allaah  je, umepata  matatizo gani na wake zako?  Ikiwa  umewataliki basi Allaah Yu pamoja nawe na Malaika na Jibriyl na Mikaaiyl na mimi na Abuu Bakr na Waumini tu pamoja nawe.” Na  mara chache nilipozungumza na kumshukuru Allaah kwa maneno yangu, basi hutarajia Allaah Asadikishe kauli yangu ninayosema, Ikateremka Aayah hii Aayah ya At-Takh-yiyr (chaguo):   

 

عَسَىٰ رَبُّهُ إِن طَلَّقَكُنَّ أَن يُبْدِلَهُ أَزْوَاجًا خَيْرًا مِّنكُنَّ  

 Akikutalikini, asaa Rabb Wake Akambadilishia wake bora kuliko nyinyi; 

 

وَإِن تَظَاهَرَا عَلَيْهِ فَإِنَّ اللَّـهَ هُوَ مَوْلَاهُ وَجِبْرِيلُ وَصَالِحُ الْمُؤْمِنِينَ ۖ وَالْمَلَائِكَةُ بَعْدَ ذَٰلِكَ ظَهِيرٌ

Na mkisaidiana dhidi yake, basi hakika Allaah Ndiye Mlinzi Msaidizi wake na Jibriyl na Waumini wema, na zaidi ya hayo, Malaika pia watasaidia.

 

Na ilikuwa ni ‘Aaishah bint wa Abuu Bakr na Hafswah ndio walioshikilia kuliko wake wengineo  wa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) (kumtia dhiki katika kuomba mali). Nikasema: “Ee Rasuli wa Allaah! Je umewataliki?” Akasema: ((Hapana!)). Nikasema: “Ee Rasuli wa Allaah, mimi niliingia Msikitini na Waislamu wanafanya mchezo wa kurushiana vijiwe (wakiwa mawazoni) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amewataliki wake zake. Je niende kuwajulisha kuwa hukuwataliki?”  Akasema:  ((Naam ukipenda)).  Basi nikaendelea kuongea naye mpaka ghadhabu ikapotea usoni mwake na uso wake ukawa na utulivu wa maumbile yake, akacheka na meno yake yakaonekana naye alikuwa na mwanya mzuri zaidi kuliko watu wengineo.  Kisha Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akateremka, nami nikateremka huku nikikamata  gogo la mtende  na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akiteremka chini (kwa wepesi kabisa) kama vile anavyotembea  ardhini bila ya kukamata chochote (cha sapoti). Nikasema: “Ee Rasuli wa Allaah. Ulibakia chumbani kwako siku ishirini na tisa.” Akasema: ((Miezi (hutokea kuwa) ni siku ishiri na tisa.) Nikasimama mlangoni mwa Msikiti nikanadi kwa sauti ya juu kabisa:  “Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) hakuwataliki wake zake!”  Hapo ikateremka: 

 

وَإِذَا جَاءَهُمْ أَمْرٌ مِّنَ الْأَمْنِ أَوِ الْخَوْفِ أَذَاعُوا بِهِ ۖ وَلَوْ رَدُّوهُ إِلَى الرَّسُولِ وَإِلَىٰ أُولِي الْأَمْرِ مِنْهُمْ لَعَلِمَهُ الَّذِينَ يَسْتَنبِطُونَهُ مِنْهُمْ ۗ  

 Na linapowafikia jambo lolote la amani au la khofu hulitangaza. Na lau wangelirudisha kwa Rasuli na kwa wenye madaraka kati yao, wangelijua wale wanaotafiti wakabainisha ya sahihi miongoni mwao. [An-Nisaa: 83] 

 

Ikawa ni mimi niliyeifahamu kwa kina  amri hiyo na Allaah (عزّ وجلّ) Akateremsha Aayah ya At-Takh-yiyr.”

 

[Muslim Kitaab Atw-Twalaaq]

 

Riwaayah nyenginezo za Asbaab Nuzuwl katika Hadiyth zifuatazo:

 

Asbaabun-Nuzuwl

 أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

 

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

066-At-Tahriym Aayah 1-5

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

يَا أَيُّهَا النَّبِيُّ لِمَ تُحَرِّمُ مَا أَحَلَّ اللَّـهُ لَكَ ۖ تَبْتَغِي مَرْضَاتَ أَزْوَاجِكَ ۚ وَاللَّـهُ غَفُورٌ رَّحِيمٌ﴿١﴾

1. Ee Nabiy! Kwanini unaharamisha kile Alichokuhalalishia Allaah? Unataka kuwaridhisha wake zako; na Allaah ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu.

 

قَدْ فَرَضَ اللَّـهُ لَكُمْ تَحِلَّةَ أَيْمَانِكُمْ ۚ وَاللَّـهُ مَوْلَاكُمْ ۖ وَهُوَ الْعَلِيمُ الْحَكِيمُ﴿٢﴾

2. Allaah Amekwishakufaridhishieni ukomboaji kwa viapo vyenu, na Allaah ni Mola wenu Naye Ndiye Mjuzi wa yote, Mwenye hikmah wa yote.

 

وَإِذْ أَسَرَّ النَّبِيُّ إِلَىٰ بَعْضِ أَزْوَاجِهِ حَدِيثًا فَلَمَّا نَبَّأَتْ بِهِ وَأَظْهَرَهُ اللَّـهُ عَلَيْهِ عَرَّفَ بَعْضَهُ وَأَعْرَضَ عَن بَعْضٍ ۖ فَلَمَّا نَبَّأَهَا بِهِ قَالَتْ مَنْ أَنبَأَكَ هَـٰذَا ۖ قَالَ نَبَّأَنِيَ الْعَلِيمُ الْخَبِيرُ﴿٣﴾

 

3. Na pale Nabiy alipompa mmoja wa wake zake jambo la siri, na huyo mke alipoipasha habari na Allaah Akamdhihirishia (Nabiy صلى الله عليه وآله وسلم), akataarifu baadhi yake na akaacha nyingine. Basi alipomjulisha hayo, akasema: “Nani aliyekujulisha haya?” Akasema: “Amenijulisha Mjuzi wa yote, Mwenye upeo wa khabari za dhahiri na za kufichika.”

 

 

إِن تَتُوبَا إِلَى اللَّـهِ فَقَدْ صَغَتْ قُلُوبُكُمَا ۖ وَإِن تَظَاهَرَا عَلَيْهِ فَإِنَّ اللَّـهَ هُوَ مَوْلَاهُ وَجِبْرِيلُ وَصَالِحُ الْمُؤْمِنِينَ ۖ وَالْمَلَائِكَةُ بَعْدَ ذَٰلِكَ ظَهِيرٌ﴿٤﴾

4. Ikiwa nyinyi wawili mtatubia kwa Allaah (ni kheri kwenu) kwani kwa hakika nyoyo zenu zimeelemea (yanayomchukiza Nabiy صلى الله عليه وآله وسلم). Na mkisaidiana dhidi yake, basi hakika Allaah Ndiye Mlinzi Msaidizi wake na Jibriyl na Waumini wema, na zaidi ya hayo, Malaika pia watasaidia.

 

 

عَسَىٰ رَبُّهُ إِن طَلَّقَكُنَّ أَن يُبْدِلَهُ أَزْوَاجًا خَيْرًا مِّنكُنَّ مُسْلِمَاتٍ مُّؤْمِنَاتٍ قَانِتَاتٍ تَائِبَاتٍ عَابِدَاتٍ سَائِحَاتٍ ثَيِّبَاتٍ وَأَبْكَارًا﴿٥﴾

 

5. Akikutalikini, asaa Rabb Wake Akambadilishia wake bora kuliko nyinyi; Waislamu, Waumini, watiifu na wanyenyekevu, wanaotubia, wenye kufanya ‘ibaadah, wanaofunga Swiyaam au wanaohajiri kwa ajili ya Allaah, wajane, na walio bikra.

 

 

Sababun-Nuzuwl (1):

 

حَدَّثَنِي الْحَسَنُ بْنُ مُحَمَّدِ بْنِ صَبَّاحٍ، حَدَّثَنَا حَجَّاجٌ، عَنِ ابْنِ جُرَيْجٍ، قَالَ زَعَمَ عَطَاءٌ أَنَّهُ سَمِعَ عُبَيْدَ بْنَ عُمَيْرٍ، يَقُولُ سَمِعْتُ عَائِشَةَ  رضى الله عنها   أَنَّ النَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم كَانَ يَمْكُثُ عِنْدَ زَيْنَبَ ابْنَةِ جَحْشٍ، وَيَشْرَبُ عِنْدَهَا عَسَلاً، فَتَوَاصَيْتُ أَنَا وَحَفْصَةُ أَنَّ أَيَّتَنَا دَخَلَ عَلَيْهَا النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم فَلْتَقُلْ إِنِّي أَجِدُ مِنْكَ رِيحَ مَغَافِيرَ، أَكَلْتَ مَغَافِيرَ فَدَخَلَ عَلَى إِحْدَاهُمَا فَقَالَتْ لَهُ ذَلِكَ، فَقَالَ ‏"‏ لاَ بَلْ شَرِبْتُ عَسَلاً عِنْدَ زَيْنَبَ ابْنَةِ جَحْشٍ وَلَنْ أَعُودَ لَهُ ‏"‏‏.‏ فَنَزَلَتْ:‏ ((‏يَا أَيُّهَا النَّبِيُّ لِمَ تُحَرِّمُ مَا أَحَلَّ اللَّهُ لَكَ‏)) إِلَى: ((إِنْ تَتُوبَا إِلَى اللَّهِ‏))‏ لِعَائِشَةَ وَحَفْصَةَ ‏  ((وَإِذْ أَسَرَّ النَّبِيُّ إِلَى بَعْضِ أَزْوَاجِهِ‏))‏ لِقَوْلِهِ ‏"‏ بَلْ شَرِبْتُ عَسَلاً ‏"‏‏.‏

 

Amenihadithia Al-Hassan bin Muhammad bin As-Swabbaah amenihadithia Hajaaj kutoka kwa Ibn Jurayj amesema: ‘Atwaa alisema kuwa alimsikia ‘Ubayd bin ‘Umayr akisema nimemsikia ‘Aaishah (Radhwiya Allahu ‘anhaa) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akikaa na kushinda kwa Zaynab bint Jahsh na huwa akinywa kwake asali. Mimi (‘Aaishah) nikakubaliana na Hafswah kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) atakapoingia kwa mmoja wetu basi   aseme: “Mimi nasikia kwako harufu ya Maghaafiyr (ubani unatoka katika mti), je umekunywa Maghaafiyir?” Akafika kwa mmoja wao na akamwambia yeye hivyo. Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  akasema: ((Hamna neno nilikunywa asali kwa Zaynab bint Jahsh na sitorudui kufanya hivyo tena)). Baada ya hapo ikateremka:

 

يَا أَيُّهَا النَّبِيُّ لِمَ تُحَرِّمُ مَا أَحَلَّ اللَّـهُ لَكَ ۖ

 

1. Ee Nabiy! Kwanini unaharamisha kile Alichokuhalalishia Allaah?

 

Hadi

إِن تَتُوبَا إِلَى اللَّـهِ

4. Ikiwa nyinyi wawili mtatubia kwa Allaah…  

 

(imekusudiwa ‘Aaishah na Hafswah)

 

Na ikateremka tena:

وَإِذْ أَسَرَّ النَّبِيُّ إِلَىٰ بَعْضِ أَزْوَاجِهِ حَدِيثًا  

3. Na pale Nabiy alipompa mmoja wa wake zake jambo la siri,  

 

Kuhusu kauli yake: ((Bali nilikunywa asali))

 

[Al-Bukhariy Kitaab Atw-Twalaaq]

 

 

Sababun-Nuzuwl (2):

 

 عَنْ أَنَسٍ، أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم كَانَتْ لَهُ أَمَةٌ يَطَؤُهَا فَلَمْ تَزَلْ بِهِ عَائِشَةُ وَحَفْصَةُ حَتَّى حَرَّمَهَا عَلَى نَفْسِهِ فَأَنْزَلَ اللَّهُ عَزَّ وَجَلَّ ‏: ‏ يَا أَيُّهَا النَّبِيُّ لِمَ تُحَرِّمُ مَا أَحَلَّ اللَّهُ لَكَ   ‏ إِلَى آخِرِ الآيَةِ ‏.‏

 

Imepokelewa kutoka kwa Anas (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa na kijakazi (Maariyah Mkoptic) ambaye alikuwa akimwingilia, lakini  ‘Aaishah na Hafswah (kutokana na wivu wa kiuke) waliendelea kumbana Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kwa vitimbi na visavisa) mpaka  akafanya kuwa ni haraam kwa nafsi yake, hapo Allaah Akateremsha:

 

يَا أَيُّهَا النَّبِيُّ لِمَ تُحَرِّمُ مَا أَحَلَّ اللَّـهُ لَكَ ۖ تَبْتَغِي مَرْضَاتَ أَزْوَاجِكَ ۚ وَاللَّـهُ غَفُورٌ رَّحِيمٌ﴿١﴾

1. Ee Nabiy! Kwanini unaharamisha kile Alichokuhalalishia Allaah? Unataka kuwaridhisha wake zako; na Allaah ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu.

 

[An-Nasaaiy kama ilivyo katika Tafsiyr Ibn Kathiyr (Juz 4 uk 386) na Al-Hakam (Juz 2 uk 493) na akasema ipo katika shuruti za Muslim na ikathibitishwa na Adh-Dhahabiy]

 

 

Pia:

 

Kutoka kwa Ibn ‘Abbas (Radhwiya Allaahu ‘ahumaa) kwamba Aayah

 

يَا أَيُّهَا النَّبِيُّ لِمَ تُحَرِّمُ مَا أَحَلَّ اللَّـهُ لَكَ ۖ تَبْتَغِي مَرْضَاتَ أَزْوَاجِكَ  

1. Ee Nabiy! Kwanini unaharamisha kile Alichokuhalalishia Allaah? Unataka kuwaridhisha wake zako;  

 

imeteremka hii kuhusu kijakazi wake:

 

[Majma’ Az-Zawaaid (Juz 7 uk 126) Imepokewa na Al-Bazzar kwa Isnaad mbili na At-Twabaraaniy na wapokezi wa Al-Bazzar ni wapokezi sahihi isipokuwa mmoja ambaye ni Bishri bin Adam nae ni Thiqqha (mwaminifu)].

 

 

Pia:

 

Kutoka kwa Ibn ‘Umar (Radhwiya Allaahu ‘anhu) amesema kuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  alimwambia Hafswa, “Usimwambie mtu kwa hakika Ummu Ibraahiym ni haraam kwangu.” Hafswah akasema: Unaharamisha Alilokuhalalishia Allaah? Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  akasema, “Wa-Allahi simkurubii.” Akasema: Hivyo hakumkurubia hadi (Hafswah) akamwelezea ‘Aaishah akasema baada ya hapo Allaah Akateremsha:

 

قَدْ فَرَضَ اللَّـهُ لَكُمْ تَحِلَّةَ أَيْمَانِكُمْ ۚ وَاللَّـهُ مَوْلَاكُمْ ۖ وَهُوَ الْعَلِيمُ الْحَكِيمُ﴿٢﴾

2. Allaah Amekwishakufaridhishieni ukomboaji kwa viapo vyenu. 

[Imepokewa na Al-Haytham bin Kuleyb katika musnad yake kama ilivyo katika tafsiri ya Ibn Kathiyr (Juz 4 uk 386)]

 

Al-Haafidhw amesema katika Al-Fat-h (Juz 10 Uk 283): “Inayumkinika Aayah ikawa imeteremka kwa sababu mbili mpigo; yaani kujiharamishia asali na kujiharamishia kijakazi wake.”

 

Ash-Shawkaaniy amesema katika tafsiri yake (Juz 5 Uk 252): “Na hizi ni sababu mbili sahihi za kuteremka Aayah, na kuzikusanya pamoja kunawezekana kwa kutokea visa viwili; kisa cha asali na kisa cha kijakazi (Maariyah Al-Qubtwiyyah), na kwamba Qur-aan iliteremka kuhusiana na visa hivyo viwili kwa pamoja, na katika kila kisa kati ya viwili, yeye alizungumza kwa siri kwa baadhi ya wakeze.”

 

 

Asbaabun-Nuzuwl

 

 أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

074-Al-Muddath-thir Aayah 11 - 31

 

 

Kauli Zake Allaah (سبحانه وتعالى):

ذَرْنِي وَمَنْ خَلَقْتُ وَحِيدًا﴿١١﴾

Niache Mimi na yule Niliyemuumba Pekee.

 

وَجَعَلْتُ لَهُ مَالًا مَّمْدُودًا﴿١٢﴾

Na Nikamjaalia mali tele.

 

وَبَنِينَ شُهُودًا﴿١٣﴾

Na watoto wanaoonekana.

 

وَمَهَّدتُّ لَهُ تَمْهِيدًا﴿١٤﴾

Na Nikamuandalia kwa sahali maandalizi mazuri.

 

ثُمَّ يَطْمَعُ أَنْ أَزِيدَ﴿١٥﴾

Kisha anatumaini Nimuongezee.

 

كَلَّا ۖ إِنَّهُ كَانَ لِآيَاتِنَا عَنِيدًا﴿١٦﴾

Laa, hasha!  Hakika yeye amekuwa anidi na mpinzani wa Aayaat Zetu. [Al-Muddaththir: 11-16]

 

(mpaka Aayah 31)

 

Sababun-Nuzuwl:

 

قال إسحاق: حدثنا عبد الرزاق عن معمر عن أيوب السختياني عن عكرمة عن ابن عباس أن الوليد بن المغيرة جاء رسول الله صلى الله عليه وعلى آله وسلم فقرأ عليه القرآن فكأنه رق له، فبلغ ذلك أبا جهل فأتاه، فقال: "يا عم إن قومك يريدون أن يجمعوا لك مالا". قال: لم؟ قال: ليعطوكه فأنت أتيت محمد لتعرض ما قبله، قال: قد علمت قريش أني من أكثرها مالا، قال: فقل فيه قولا يبلغ قومك أنك منكر له. قال: وماذا أقول، فوالله ما منكم رجل أعرف بالأشعار مني ولا أعلم برجزه ولا بقصيده مني ولا بأشعار الجن، والله ما يشبه الذي يقول شيئا من هذا. ووالله إن لقوله الذي يقوله حلاوة، وإن عليه لطلاوة، وإنه لمثمر أعلاه، مغدق أسفله، وإنه ليعلو ولا يعلى، وإنه ليحطم ما تحته. قال: لا يرضي عنك قومك حتى تقول فيه. قال: قف عني حتى أفكر فيه. فلما فكر قال: إن هذا إلا سحر يؤثر يأثره عن غيره فنزلت: {ذَرْنِي وَمَنْ خَلَقْتُ وَحِيدًا، وَجَعَلْتُ لَهُ مَالًا مَمْدُودًا، وَبَنِينَ ...

 

Is-haaq amesema Abdur-Razaaq ametuhadithia kutoka kwa Ma’mar kutoka kwa Ayyuwb As-Sakhtiyaaniy kutoka kwa ‘Ikrimah kutoka kwa Ibn ‘Abbaas kuwa Al-Waliyd bin Al-Mughiyrah alikwenda kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  akamsomea Qur-an akawa Waliyd kama kwamba ameathiriwa nayo na kulainika. Habari hiyo ikamfikia Abuu Jahal akamjia akasema: “Ee ‘ammi  yangu, kwa hakika watu wako wanataka wakukusanyie mali.” Akasema: “Kwa nini?” Akasema: “Ili wakupatie kwani wewe umemwendea Muhammad ukamuaridhie upate (chakula au mali) yaliyoko  kwake!”  Akasema: “Ma-Quraysh wote wanajua kuwa mimi ni mtu mwenye mali nyingi.” Akasema: “Basi useme maneno ambayo yatawafikia kuwa wewe unampinga.” Akasema: “Niseme nini? Wa-Allaahi hakuna mtu mwenye kujua mashairi kuliko mimi wala kuliko yeyote katika majini! Na naapa kwa Allaah Ayasemayo (Muhammad) hayafanani na chochote katika haya! Wa-Allaahi kwa hakika maneno ayasemayo (Qur-aan), yana haiba na yanavutia mno! Sehemu yake ya juu kabisa ni neemefu na chini yake inabubujika kwa baraka, na inaangamiza kilicho chini yake!” Abuu Jahl akasema: “Hawatakuwa radhi kwako watu wako hadi useme yaliyo dhidi yake.” Akasema: “Niondokee mbali hadi nifikirie!” Baada ya kufikiri,  akasema: “Kwa hakika huu ni uchawi unaoathiri na huathiri wengineo!”   Ikateremka:

 

ذَرْنِي وَمَنْ خَلَقْتُ وَحِيدًا﴿١١﴾

Niache Mimi na yule Niliyemuumba Pekee.

وَجَعَلْتُ لَهُ مَالًا مَّمْدُودًا﴿١٢﴾

Na Nikamjaalia mali tele.

وَبَنِينَ شُهُودًا﴿١٣﴾

Na watoto wanaoonekana.

وَمَهَّدتُّ لَهُ تَمْهِيدًا﴿١٤﴾

Na Nikamuandalia kwa sahali maandalizi mazuri.

ثُمَّ يَطْمَعُ أَنْ أَزِيدَ﴿١٥﴾

Kisha anatumaini Nimuongezee.

كَلَّا ۖ إِنَّهُ كَانَ لِآيَاتِنَا عَنِيدًا﴿١٦﴾

Laa, hasha!  Hakika yeye amekuwa anidi na mpinzani wa Aayaat Zetu.

 

[Hadiyth ameinukuu Al-Haakim katika Al-Mustadrak (2/506-507) na Atw-Twabariy katika Jaami’ Al-Bayaan (29/156) ni Swahiyh] Na pia angalia Al-Bidaayah Wan-Nihaayah (3/60)

 

Aayah zinazoendelea kuhusiana na tukio hilo:

 

 

Asbaabun-Nuzuwl

 

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

 

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

 

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

 

 

074-Al-Muddath-thir Aayah 1-7

 

بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ

 

يَا أَيُّهَا الْمُدَّثِّرُ﴿١﴾

1. Ee mwenye kujigubika!

قُمْ فَأَنذِرْ﴿٢﴾

2. Simama na uonye 

وَرَبَّكَ فَكَبِّرْ﴿٣﴾

3. Na Rabb wako mtukuze. 

وَثِيَابَكَ فَطَهِّرْ﴿٤﴾

4. Na nguo zako toharisha.

وَالرُّجْزَ فَاهْجُرْ﴿٥﴾

5. Na najisi (masanamu( epukana nayo.

وَلَا تَمْنُن تَسْتَكْثِرُ﴿٦﴾

6. Na wala usifanye fadhila kwa ajili ya kutaraji kukithirishiwa.

 

وَلِرَبِّكَ فَاصْبِرْ﴿٧﴾

7. Na kwa ajili ya Rabb wako subiri.

 

حَدَّثَنَا يَحْيَى، حَدَّثَنَا وَكِيعٌ، عَنْ عَلِيِّ بْنِ الْمُبَارَكِ،  عَنْ يَحْيَى بْنِ أَبِي كَثِيرٍ، سَأَلْتُ أَبَا سَلَمَةَ بْنَ عَبْدِ الرَّحْمَنِ عَنْ أَوَّلِ، مَا نَزَلَ مِنَ الْقُرْآنِ‏.‏ قَالَ: ((‏يَا أَيُّهَا الْمُدَّثِّرُ))  ‏قُلْتُ يَقُولُونَ ‏((‏اقْرَأْ بِاسْمِ رَبِّكَ الَّذِي خَلَقَ‏))‏ فَقَالَ أَبُو سَلَمَةَ: سَأَلْتُ جَابِرَ بْنَ عَبْدِ اللَّهِ رضى الله عنهما عَنْ ذَلِكَ وَقُلْتُ لَهُ مِثْلَ الَّذِي قُلْتَ فَقَالَ جَابِرٌ: لاَ أُحَدِّثُكَ إِلاَّ مَا حَدَّثَنَا رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ ‏((جَاوَرْتُ بِحِرَاءٍ، فَلَمَّا قَضَيْتُ جِوَارِي هَبَطْتُ فَنُودِيتُ فَنَظَرْتُ عَنْ يَمِينِي فَلَمْ أَرَ شَيْئًا، وَنَظَرْتُ عَنْ شِمَالِي فَلَمْ أَرَ شَيْئًا، وَنَظَرْتُ أَمَامِي فَلَمْ أَرَ شَيْئًا، وَنَظَرْتُ خَلْفِي فَلَمْ أَرَ شَيْئًا، فَرَفَعْتُ رَأْسِي فَرَأَيْتُ شَيْئًا، فَأَتَيْتُ خَدِيجَةَ فَقُلْتُ دَثِّرُونِي وَصُبُّوا عَلَىَّ مَاءً بَارِدًا)) قَالَ: ((فَدَثَّرُونِي وَصَبُّوا عَلَىَّ مَاءً بَارِدًا)) قَالَ:   فَنَزَلَتْ ((‏‏يَا أَيُّهَا الْمُدَّثِّرُ * قُمْ فَأَنْذِرْ * وَرَبَّكَ فَكَبِّرْ))

 

Yahyaa amenihadithia, ametuhadithia Waki’y bin ‘Aliy bin Al-Mubaarak kutoka kwa Yahyaa bin Abiy Kathiyr nimemuuliza Abaa Salamah bin Abdir-Rahmaah kutoka katika ya mwanzo iliyoteremka katika Qur-aan, amesema:

 

 يَا أَيُّهَا الْمُدَّثِّرُ﴿١﴾

1. Ee mwenye kujigubika!

 

Nikasema: wanasema

 اقْرَأْ بِاسْمِ رَبِّكَ الَّذِي خَلَقَ ﴿١﴾

1. Soma kwa Jina la Rabb wako Aliyeumba.

 

Akasema Abuu Salamah: Nilimuuliza Jaabir kutoka kwa Abdullaah (رضي لله عنهما)  kuhusu hilo, na nikamwambia yale niliyosema, Jaabir akasema: Sikuambii isipokuwa lile ambalo ametuhadithia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) kwamba: “Nilifika (pango la) Al-Hiraa, nilipomaliza haja yangu nikaondoka. Mara nikasikia naitwa, nikageuka upande wangu wa kuume sikuona kitu, nikageuka kushoto sikuona kitu, kisha nikageuka nyuma yangu sikuona kitu, nikanyanyua kichwa changu nikaona kitu, nikaenda kwa Khadiyjah nikamwambia: Dath-thiruwniy (Nigubikeni) na nimwagieni maji baridi!” Akasema: “Wakanigubika na wakanimwagia maji baridi.” Akasema ikateremka:

 

يَا أَيُّهَا الْمُدَّثِّرُ﴿١﴾

1. Ee mwenye kujigubika!

 

قُمْ فَأَنذِرْ﴿٢﴾

2. Simama na uonye 

 

[Al-Bukhaariy Kitaab At-Tafsiyr]

 

Al-Hafidhw Ibn Kathiyr amesema katika Tafsiyr (4/440) kwa maana yake: Jaabir bin Abdilaah aliikhalifu jamhuri kwa kauli yake: Kuwa ya mwanzo kushuka ilikuwa ni Suwrah Al-Muddath-thir. Na wengine walisema ya kwanza ilikuwa ni Suwrah Iqraa (Al-‘Alaq). Kisha akataja Hadiyth  katika Swahiyh mbili akasema:

 

Imepokewa na Muslim kwa njia ya ‘Uqayl kutoka kwa Ibn Shihaab kutoka kwa Abu Salamah amesema: Jaabir amenijulisha kuwa amesikia kutoka kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  akielezea kile kipindi cha kushuka Wahyi akasema katika Hadiyth  yake: “Pindi nilipokuwa nikitembea niliposikia sauti kutoka mbinguni, nikanyanyua macho yangu upande wa mbinguni, nikamuona yule Malaika aliyenijia katika pango la Hiraa akiwa amekaa katika kitu kati ya mbingu na ardhi, nikamuelekea naye akashuka ardhini, nikaenda kwa mke wangu, nikamwambia, “Zamiluwniy! Zamiluwniy!” yaani “Nifunikeni! Nifunikeni!” hapo Allaah Akateremsha:

 يَا أَيُّهَا الْمُدَّثِّرُ﴿١﴾

1. Ee mwenye kujigubika!

قُمْ فَأَنذِرْ﴿٢﴾

2. Simama na uonye 

 

Abuu Salamah amesema: Na rijz ni masanamu. Kisha baada ya hapo Wahyi ukaendelea kushuka na kufuatana. Hili ni tamko la Al-Bukhaariy na maelezo haya yamehifadhiwa nayo ndio yanayotarajiwa kuwa Wahyi umeteremka kabla ya kauli hii: “Mara nikamuona Malaika aliyekuwa pale pango la Hiraa” naye si mwingine bali ni Jibriyl alipomjia kwa kumteremshia: (Suwrah Al-‘Alaq : 96)

 

اقْرَأْ بِاسْمِ رَبِّكَ الَّذِي خَلَقَ ﴿١﴾

1. Soma kwa Jina la Rabb wako Aliyeumba.

 

خَلَقَ الْإِنسَانَ مِنْ عَلَقٍ ﴿٢﴾

2. Amemuumba mwana Aadam kutokana na pande la damu linaloning’inia.

 

اقْرَأْ وَرَبُّكَ الْأَكْرَمُ ﴿٣﴾

3. Soma na Rabb wako ni Mkarimu kushinda wote.

 

الَّذِي عَلَّمَ بِالْقَلَمِ ﴿٤﴾

4. Ambaye Aliyefunza kwa kalamu.

 

عَلَّمَ الْإِنسَانَ مَا لَمْ يَعْلَمْ ﴿٥﴾

5. Amemfunza mwana Aadam ambayo asiyoyajua.

 

Kisha baada ya hapo ikapita muda kisha Malaika akateremka baada ya hapo na makubaliano ni kuwa kilichoteremka baada ya muda wa Wahyi kukatika ni Suwrah hii (Al-Muddath-thir) kisha akatoa dalili ya hilo.

 

Na Haafidhw ametaja mfano wake katika Al-Fath (1/31)  na (10/304-305)

 

 

 Pia

 

وَحَدَّثَنَا زُهَيْرُ بْنُ حَرْبٍ، حَدَّثَنَا الْوَلِيدُ بْنُ مُسْلِمٍ، حَدَّثَنَا الأَوْزَاعِيُّ، قَالَ سَمِعْتُ يَحْيَى، يَقُولُ سَأَلْتُ أَبَا سَلَمَةَ أَىُّ الْقُرْآنِ أُنْزِلَ قَبْلُ قَالَ: ((يَا أَيُّهَا الْمُدَّثِّرُ)) ‏.‏ فَقُلْتُ أَوِ ((اقْرَأْ ))‏.‏ فَقَالَ سَأَلْتُ جَابِرَ بْنَ عَبْدِ اللَّهِ أَىُّ الْقُرْآنِ أُنْزِلَ قَبْلُ قَالَ ((يَا أَيُّهَا الْمُدَّثِّرُ)) ‏.‏ فَقُلْتُ أَوِ ((اقْرَأْ)) قَالَ جَابِرٌ أُحَدِّثُكُمْ مَا حَدَّثَنَا رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((جَاوَرْتُ بِحِرَاءٍ شَهْرًا فَلَمَّا قَضَيْتُ جِوَارِي نَزَلْتُ فَاسْتَبْطَنْتُ بَطْنَ الْوَادِي فَنُودِيتُ فَنَظَرْتُ أَمَامِي وَخَلْفِي وَعَنْ يَمِينِي وَعَنْ شِمَالِي فَلَمْ أَرَ أَحَدًا ثُمَّ نُودِيتُ فَنَظَرْتُ فَلَمْ أَرَ أَحَدًا ثُمَّ نُودِيتُ فَرَفَعْتُ رَأْسِي فَإِذَا هُوَ عَلَى الْعَرْشِ فِي الْهَوَاءِ )) يَعْنِي جِبْرِيلَ عَلَيْهِ السَّلاَمُ ((فَأَخَذَتْنِي رَجْفَةٌ شَدِيدَةٌ فَأَتَيْتُ خَدِيجَةَ فَقُلْتُ دَثِّرُونِي ‏.‏ فَدَثَّرُونِي فَصَبُّوا عَلَىَّ مَاءً فَأَنْزَلَ اللَّهُ عَزَّ وَجَلَّ: ((يَا أَيُّهَا الْمُدَّثِّرُ * قُمْ فَأَنْذِرْ * وَرَبَّكَ فَكَبِّرْ * وَثِيَابَكَ فَطَهِّرْ)) ‏.‏

 

Zuhayr bin Harb ametuhadithia na Waliyd bin Muslim kadhalika na Al-Awzaa’iy amesema kuwa nimemsikia Yahyaa. Anasema nimemuuliza Abaa Salamah ni Qur-aan ipi iliyoteremka kabla akasema ni:

 

يَا أَيُّهَا الْمُدَّثِّرُ﴿١﴾

1. Ee mwenye kujigubika!

 

Nikasema au ni ((Iqraa?)). Akasema Nimemuuliza Jaabir bin Abdillaah ni Qur-aan ipi iliyoteremka kabla ya

 

يَا أَيُّهَا الْمُدَّثِّرُ﴿١﴾

1. Ee mwenye kujigubika!

 

Nikasema au ni ((Iqraa?))  Jaabir akasema: Niwahadithie alichohadithia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) ambaye amesema: “Nilikaa Hiraa muda wa mwezi mzima, nilipomaliza nikashuka Batwn Al-Waadiy nikawa ninaitwa nikaangalia upande wangu wa mbele kisha nyuma na kulia kisha kushoto sikuona chochote. Kisha nikaitwa tena nikaangalia sikuona yeyote kisha nikaitwa nikaangalia juu ya kichwa changu juu ya ‘Arsh hewani (yaaani Jibriyl عليه السلام) ikanipata mtetemeko mkubwa nikaenda kwa Khadiyjah nikamwambia: Dath-thiruwniy! (Yaani nigubikeni). Hivyo wakanigubika na wakanimwagia maji. Baada ya hapo Allaah 'Azza wa Jalla Akateremsha:

بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ

 

يَا أَيُّهَا الْمُدَّثِّرُ﴿١﴾

1. Ee mwenye kujigubika!

 

قُمْ فَأَنذِرْ﴿٢﴾

2. Simama na uonye 

 

وَرَبَّكَ فَكَبِّرْ﴿٣﴾

3. Na Rabb wako mtukuze. 

 

وَثِيَابَكَ فَطَهِّرْ﴿٤﴾

4. Na nguo zako toharisha.

 

 

 

[Muslim Kitaab Al-Iymaan]

 

 

Aayah zinazoendelea:

 

وَالرُّجْزَ فَاهْجُرْ﴿٥﴾

5. Na najisi (masanamu( epukana nayo.

 

 

وَلَا تَمْنُن تَسْتَكْثِرُ﴿٦﴾

6. Na wala usifanye fadhila kwa ajili ya kutaraji kukithirishiwa.

 

 

وَلِرَبِّكَ فَاصْبِرْ﴿٧﴾

7. Na kwa ajili ya Rabb wako subiri.

 

 

فَإِذَا نُقِرَ فِي النَّاقُورِ﴿٨﴾

8. Itakapopulizwa katika baragumu kwa sauti kali.

 

 

فَذَٰلِكَ يَوْمَئِذٍ يَوْمٌ عَسِيرٌ﴿٩﴾

9. Basi hiyo itakuwa ni Siku ngumu.

 

 

عَلَى الْكَافِرِينَ غَيْرُ يَسِيرٍ﴿١٠﴾

10. Kwa makafiri si nyepesi.

 

 

 

 

Asbaabun-Nuzuwl

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

 

075-Al-Qiyaamah:

 

لَا تُحَرِّكْ بِهِ لِسَانَكَ لِتَعْجَلَ بِهِ﴿١٦﴾

16. Usiutikisie (huu Wahy) ulimi wako ili kuiharakiza (Qur-aan ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم)..

 

إِنَّ عَلَيْنَا جَمْعَهُ وَقُرْآنَهُ﴿١٧﴾

17. Hakika ni juu Yetu kuikusanya na kukuwezesha kuisoma kwake.

 

فَإِذَا قَرَأْنَاهُ فَاتَّبِعْ قُرْآنَهُ﴿١٨﴾

18. Basi Tunapoisoma (kupitia Jibriyl), fuata kusomwa kwake.

 

ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا بَيَانَهُ﴿١٩﴾

19. Kisha ni juu Yetu kuibainisha (kwako).

 

 

حَدَّثَنَا قُتَيْبَةُ بْنُ سَعِيدٍ، حَدَّثَنَا جَرِيرٌ، عَنْ مُوسَى بْنِ أَبِي عَائِشَةَ، عَنْ سَعِيدِ بْنِ جُبَيْرٍ، عَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ، فِي قَوْلِهِ: ((لاَ تُحَرِّكْ بِهِ لِسَانَكَ لِتَعْجَلَ بِهِ‏)) قَالَ كَانَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم: ((إِذَا نَزَلَ جِبْرِيلُ بِالْوَحْىِ، وَكَانَ مِمَّا يُحَرِّكُ بِهِ لِسَانَهُ وَشَفَتَيْهِ فَيَشْتَدُّ عَلَيْهِ وَكَانَ يُعْرَفُ مِنْهُ، فَأَنْزَلَ اللَّهُ الآيَةَ الَّتِي فِي: ((‏لاَ أُقْسِمُ بِيَوْمِ الْقِيَامَةِ))  ...((‏لاَ تُحَرِّكْ بِهِ لِسَانَكَ لِتَعْجَلَ بِهِ * إِنَّ عَلَيْنَا جَمْعَهُ وَقُرْآنَهُ‏))‏ قَالَ عَلَيْنَا أَنْ نَجْمَعَهُ فِي صَدْرِكَ، وَقُرْآنَهُ ‏‏((فَإِذَا قَرَأْنَاهُ فَاتَّبِعْ قُرْآنَهُ‏))‏ فَإِذَا أَنْزَلْنَاهُ فَاسْتَمِعْ ‏((‏ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا بَيَانَهُ‏))‏ عَلَيْنَا أَنْ نُبَيِّنَهُ بِلِسَانِكَ ـ قَالَ ـ فَكَانَ إِذَا أَتَاهُ جِبْرِيلُ أَطْرَقَ، فَإِذَا ذَهَبَ قَرَأَهُ كَمَا وَعَدَهُ اللَّهُ‏.‏

 

Qutaybah bin Sa’iyd ametuhadithia: Ametuhadithia Jariyr, kutoka kwa Muwsaa bin Abiy ‘Aaishah kutoka kwa Sa’iyd bin Jubayr kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) , kuhusu kauli yake Allaah (سبحانه وتعالى):

لَا تُحَرِّكْ بِهِ لِسَانَكَ لِتَعْجَلَ بِهِ﴿١٦﴾

16. Usiutikisie (huu Wahy) ulimi wako ili kuiharakiza (Qur-aan ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم).

 

Amesema, Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  alikuwa pindi anaposhuka Jibriyl na Wahyi, alikuwa akitikisa ulimi wake haraka haraka pamoja na midomo yake (kufanya haraka kusoma) na hali hiyo ilikuwa ngumu kwake, na ilikuwa inafahamika kuwa ni kuteremshwa kwa Wahyi. Basi Allaah Akateremsha katika Suwratul-Qiyaamah inayoanza na:

 

لَا أُقْسِمُ بِيَوْمِ الْقِيَامَةِ﴿١﴾

1. Naapa kwa siku ya Qiyaamah.

 

Akateremsha:

 

لَا تُحَرِّكْ بِهِ لِسَانَكَ لِتَعْجَلَ بِهِ﴿١٦﴾

 

16. Usiutikisie (huu Wahy) ulimi wako ili kuiharakiza (Qur-aan ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم).

 

إِنَّ عَلَيْنَا جَمْعَهُ وَقُرْآنَهُ﴿١٧﴾

17. Hakika ni juu Yetu kuikusanya na kukuwezesha kuisoma kwake.

 

Akasema: Ni juu Yetu kuikusanya katika kifua chako na kukusomea hiyo Qur-aan hivyo basi,

 

فَإِذَا قَرَأْنَاهُ فَاتَّبِعْ قُرْآنَهُ﴿١٨﴾

18. Basi Tunapoisoma (kupitia Jibriyl), fuata kusomwa kwake.

 

Basi pindi tutakaposoma wewe fuatiliza kisomo chetu, na usikilize kwa makini, na pindi tutakapoteremsha sikiliza vizuri.

 

ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا بَيَانَهُ﴿١٩﴾

19. Kisha ni juu Yetu kuibainisha (kwako).

 

Ni juu yetu kukubainishia katika ulimi wako. Amesema: Ikawa kila Jibriy akifika hugonga na akiondoka husoma kama vile ambavyo Allaah Amemuahidi.

[Al-Bukhaariy Kitaab Al-Wahyi na pia usimulizi kama huo katika Kitaab Fadhwaail Al-Qur-aan, Baab At-Tartiyl fiy Al-Qiraa-ah

 

Bonyeza Endelea upate faida ziyada...

 

 

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

 

 

 

079-An-Naaziaat 

 

يَسْأَلُونَكَ عَنِ السَّاعَةِ أَيَّانَ مُرْسَاهَا ﴿٤٢﴾

42. Wanakuuliza (Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) kuhusu Saa lini kufika kwake?

 

 

فِيمَ أَنتَ مِن ذِكْرَاهَا ﴿٤٣﴾

43. Huna ujuzi wewe hata utaje lolote.

 

 

 

 
 

Ibn Jariyr (30/49) amesema: Amenihadithia Ya’quwb bin Ibraahiym amesema: Ametuhadithia Sufyaan bin ‘Uyaynah kutoka kwa Az-Zuhriy kutoka kwa ‘Urwah kutoka kwa ‘Aaishah amesema: Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) aliendelea kuulizia kuhusu Saa hadi Allaah Alipoteremsha:
 

فِيمَ أَنتَ مِن ذِكْرَاهَا ﴿٤٣﴾

43. Huna ujuzi wewe hata utaje lolote.

 

 

Hadiyth imepokewa na Al-Hakam katika Al-Mustadrak (1/5) na Abuu Nu’aym katika Al-Hilyah (7/314) na akasema Al-Hakam Hadiyth hii haikuwepo katika Asw-Swahihayn nayo ni mahfuwdhw Swahiyh juu ya sharti zao wawili. Na akasema ni Swahiyh kwa sharti zao na hawakuipokea kwa sababu Ibn ‘Uyaynah aliifanyia Irsaal kwa mwingine na Al-Khatwiyb (11/321).

 

Na Al-Haafidhw ameitaja Hadiyth hii ibn Abiy Haatim katika kitabu chake Al-‘Ilal, na akasema nimemsikia Aba Zur’ah  na akataja Hadiyth ya Az-Zuhriy kutoka kwa ‘Urwah kutoka kwa ‘Aaishah amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) aliendelea kuuliza kuhusu Qiyaamah hadi ilipoteremka kwake:

 فِيمَ أَنتَ مِن ذِكْرَاهَا ﴿٤٣﴾

43. Huna ujuzi wewe hata utaje lolote.

 

 

 

Na amesema Ibn Jariyr (رحمه الله) :Ametuhadithia Abuu Kurayb, ametuhadithia Waki’y kutoka kwa Ismaa’iyl kutoka kwa Twaariq bin Shihaab amesema: Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alikuwa anaendelea kutaja mambo ya Qiyaamah hadi ilipoteremka:

 يَسْأَلُونَكَ عَنِ السَّاعَةِ أَيَّانَ مُرْسَاهَا ﴿٤٢﴾

42. Wanakuuliza (Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) kuhusu Saa lini kufika kwake?

 

Hadi kauli yake:

   مَن يَخْشَاهَا ﴿٤٥﴾

wa yule anayeikhofu.

 

 

Adh-Dhahabiy Al-Haythamiy (رحمه الله)  amesema: Ameipokea Al-Bazaar na watu wake ni Swahiyh (7/133) kutoka katika Al-Majma’ na akasema Al-Hafidhw Ibn Kathiyr (رحمه الله) katika tafsiyr yake (2/273) baada ya kutaja kwake sanad na isnad hii ni nzuri na yenye nguvu.

 

 

Aayah Husika Za Asbaabun-Nuzwul:

 

 

 

يَسْأَلُونَكَ عَنِ السَّاعَةِ أَيَّانَ مُرْسَاهَا ﴿٤٢﴾

42. Wanakuuliza (Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) kuhusu Saa lini kufika kwake?

 

 

فِيمَ أَنتَ مِن ذِكْرَاهَا ﴿٤٣﴾

43. Huna ujuzi wewe hata utaje lolote.

 

 

إِلَىٰ رَبِّكَ مُنتَهَاهَا ﴿٤٤﴾

44. Kwa Rabb wako ndio kuishia (ujuzi) wake.

 

 

إِنَّمَا أَنتَ مُنذِرُ مَن يَخْشَاهَا ﴿٤٥﴾

45. Hakika wewe ni muonyaji wa yule anayeikhofu.

 

كَأَنَّهُمْ يَوْمَ يَرَوْنَهَا لَمْ يَلْبَثُوا إِلَّا عَشِيَّةً أَوْ ضُحَاهَا ﴿٤٦﴾

46. Siku watakapoiona, watakuwa kama kwamba hawakubaki (duniani) isipokuwa jioni moja au mchana wake.

 

 

Asbaabun-Nuzuwl

 

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

 

080-'Abasa

 

عَبَسَ وَتَوَلَّىٰ ﴿١﴾

1. Alikunja kipaji na akageuka.

 

أَن جَاءَهُ الْأَعْمَىٰ ﴿٢﴾

2. Alipomjia kipofu.

 

وَمَا يُدْرِيكَ لَعَلَّهُ يَزَّكَّىٰ ﴿٣﴾

3. Na nini kitakachokujulisha (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) huenda akatakasika?

 

أَوْ يَذَّكَّرُ فَتَنفَعَهُ الذِّكْرَىٰ ﴿٤﴾

4. Au atawaidhika na yamfae mawaidha?

 

أَمَّا مَنِ اسْتَغْنَىٰ ﴿٥﴾

5. Ama yule ajionaye amejitosheleza.

 

فَأَنتَ لَهُ تَصَدَّىٰ ﴿٦﴾

6. Nawe unamgeukia kumshughulikia.

 

وَمَا عَلَيْكَ أَلَّا يَزَّكَّىٰ ﴿٧﴾

7. Na si juu yako asipotakasika.

 

وَأَمَّا مَن جَاءَكَ يَسْعَىٰ ﴿٨﴾

8. Ama yule aliyekujia kwa kukimbilia.

 

وَهُوَ يَخْشَىٰ ﴿٩﴾

9. Naye anakhofu.

 

فَأَنتَ عَنْهُ تَلَهَّىٰ ﴿١٠﴾

10. Basi wewe unampuuza.

 

 

حَدَّثَنَا سَعِيدُ بْنُ يَحْيَى بْنِ سَعِيدٍ الأُمَوِيُّ، حَدَّثَنِي أَبِي قَالَ، هَذَا مَا عَرَضْنَا عَلَى هِشَامِ بْنِ عُرْوَةَ عَنْ أَبِيهِ، عَنْ عَائِشَةَ، قَالَتْ أُنْزِلَ ‏:‏((عبَسَ وَتَوَلَّى))‏ فِي ابْنِ أُمِّ مَكْتُومٍ الأَعْمَى أَتَى رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَجَعَلَ يَقُولُ يَا رَسُولَ اللَّهِ أَرْشِدْنِي وَعِنْدَ رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم رَجُلٌ مِنْ عُظَمَاءِ الْمُشْرِكِينَ فَجَعَلَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم يُعْرِضُ عَنْهُ وَيُقْبِلُ عَلَى الآخَرِ وَيَقُولُ أَتَرَى بِمَا أَقُولُ بَأْسًا فَيُقَالُ لاَ ‏.‏ فَفِي هَذَا أُنْزِلَ

 

Ametuhadithia said bin Yahyya bin Sa’iyd Al-Amawiy amesema amenihadithia baba yangu amesema: Hili tulimtajia Hishaam bin ‘Urwat kutoka kwa baba yake kutoka kwa ‘Aaishah imeteremka:

عَبَسَ وَتَوَلَّىٰ ﴿١﴾

1. Alikunja kipaji na akageuka.

 

Kwa ibn Ummi Maktuwm aliyekuwa kipofu alikuwa kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) mara akaingia mmoja wa watu wakubwa miongoni mwa washirikina, Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akawa anamuelezea Yule mshirikina kuhusiana naye, na anamuelekea akisema:  “Je, ninalolisema unaliona baya”  kwa ajili hii ikateremka.

 

[Hadiyth hii ni Hasan Ghariyb na wengine wamepokea Hadiyth hii kutoka kwa Hishaam bin ‘Urwah kutoka kwa baba yakekuwa amesema kuwa:

 

Alikunja kipaji na akageuka”

 

Imeteremka kwa Ibn Ummi Maktuwm na hakumtaja ‘Aaishah. [At-Tirmidhiy – Kitaab At-Tafiyr Al-Qur-aan kutoka kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم

 

Wametaja wafasiri wengi kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) siku moja alikuwa akizungumza na viongozi wa ma-Quraysh na alikuwa ametaraji katika kusilimu kwa baadhi ya viongozi hao. Wakati akiwa katika mazungumzo nao, ghafla akatokezea Ibnu Ummi Maktuwm ambaye alikuwa miongoni mwa watu waliosilimu hapo kabla akawa anamuuliza Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) kuhusu jambo na huku akishikilia hilo la muhimu. Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alitaraji  kuwa atamuongoa kiongozi huyo wa Quraysh. Akamwambia ibn Maktuwm asubiri ili amalize maongezi nao. Akakunja uso na akampa mgongo na akaelekea kwa yule mwingine hapo Allaah Akateremsha:

عَبَسَ وَتَوَلَّىٰ ﴿١﴾

1. Alikunja kipaji na akageuka.

أَن جَاءَهُ الْأَعْمَىٰ ﴿٢﴾

2. Alipomjia kipofu.

 

Asbaabun-Nuzuwl

 

 

 

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

 

093-Adhw-Dhwuhaa:

 

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

 

وَالضُّحَىٰ ﴿١﴾

1. Naapa kwa dhuha.

 

وَاللَّيْلِ إِذَا سَجَىٰ ﴿٢﴾

2. Na Naapa kwa usiku unapotanda kiza na kutulia.

 

مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ ﴿٣﴾

3. Rabb wako Hakukutelekeza na wala Hakukuchukia (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم).

 

 

حَدَّثَنَا إِسْحَاقُ بْنُ إِبْرَاهِيمَ، أَخْبَرَنَا سُفْيَانُ، عَنِ الأَسْوَدِ بْنِ قَيْسٍ، أَنَّهُ سَمِعَ جُنْدُبًا، يَقُولُ أَبْطَأَ جِبْرِيلُ عَلَى رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ الْمُشْرِكُونَ: قَدْ وُدِّعَ مُحَمَّدٌ فَأَنْزَلَ اللَّهُ عَزَّ وَجَلَّ: ((وَالضُّحَى * وَاللَّيْلِ إِذَا سَجَى * مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَى‏))‏

 

Ametuhadithia Is-haaq bin Ibraahiym, ametujulisha Sufyaan kutoka kwa Al-Aswad bin Qays kuwa amemsikia Jundub akisema: Jibriyl alichelewa kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم), washirikina wakasema kuwa Jibriyl amemtelekeza Muhammad hivyo Allaah Akateremsha:

 

وَالضُّحَىٰ ﴿١﴾

1. Naapa kwa dhuha.

 

وَاللَّيْلِ إِذَا سَجَىٰ ﴿٢﴾

2. Na Naapa kwa usiku unapotanda kiza na kutulia.

 

مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ ﴿٣﴾

3. Rabb wako Hakukutelekeza na wala Hakukuchukia (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم).

 

[Muslim: Kitaab Al-Jihaad Was-Siyar - Mlango wa maudhi aliyoyapata Nabiy kutoka kwa Washirikina na wanafiki]‏‏.

 

Pia,

 

حَدَّثَنَا أَحْمَدُ بْنُ يُونُسَ، حَدَّثَنَا زُهَيْرٌ، حَدَّثَنَا الأَسْوَدُ بْنُ قَيْسٍ، قَالَ سَمِعْتُ جُنْدُبَ بْنَ سُفْيَانَ رضى الله عنه قَالَ: اشْتَكَى رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَلَمْ يَقُمْ لَيْلَتَيْنِ أَوْ ثَلاَثًا، فَجَاءَتِ امْرَأَةٌ فَقَالَتْ:  يَا مُحَمَّدُ! إِنِّي لأَرْجُو أَنْ يَكُونَ شَيْطَانُكَ قَدْ تَرَكَكَ، لَمْ أَرَهُ قَرِبَكَ مُنْذُ لَيْلَتَيْنِ أَوْ ثَلاَثًا‏.‏ فَأَنْزَلَ اللَّهُ عَزَّ وَجَلَّ: ((وَالضُّحَى * وَاللَّيْلِ إِذَا سَجَى * مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَى‏))

Ahmad bin Yuwnus ametuhadithia na Zuhayr pamoja na Al-Aswad ametuhadithia kuwa, Nimemsikia Jundub bin Sufyaan (رضي الله عنه) kwamba:  Wakati fulani Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alionesha masikitiko yake (ya kutoteremka kwake Jibriyl) au kuumwa na hakusimama kwa muda wa siku mbili au tatu, akatokea mwanamke akasema: Yaa Muhammad! Mimi nadhani shaytwaan wako amekuacha, sijamuona akikukurubia kwa muda wa siku mbili au tatu. Allaah (عزّ وجلّ) Akateremsha:

وَالضُّحَىٰ ﴿١﴾

1. Naapa kwa dhuha.

 

وَاللَّيْلِ إِذَا سَجَىٰ ﴿٢﴾

2. Na Naapa kwa usiku unapotanda kiza na kutulia.

 

مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ ﴿٣﴾

3. Rabb wako Hakukutelekeza na wala Hakukuchukia (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم).

 

[Al-Bukhaariy: Kitaab At-Tafsiyr]

 

Kauli Yake Allaah (سبحانه وتعالى):

وَلَسَوْفَ يُعْطِيكَ رَبُّكَ فَتَرْضَىٰ ﴿٥﴾

5. Na bila shaka Rabb wako Atakupa na utaridhika.

 

 

Ibn Kathiyr katika Tafsiyr  yake (4/522) amesema:

 

Abuu ‘Umar Al-Awzaa’iyy kutoka kwa Ismaa’iyl bin ‘Ubaydillaah bin Abiy Al-Muhaajir Al-Makhzuwmiyy kutoka kwa ‘Aliy bin ‘Abbaas kutoka kwa baba yake amesema kuwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alimdhihirishia kilichofunguliwa katika Ummah wake hazina baada ya hazina, akafurahishwa kwa hilo na Allaah Akateremsha:

 

5. Na bila shaka Rabb wako Atakupa na utaridhika.

Allaah Akampa Jannah kuna kasri elfu na elfu na katika kila kasri kuna unachotaka katika wake na wahudumu. [Imepokewa na Ibn Jurayj na Ibn Abiy Haatim kutoka katika njia yake na hii ni Isnaad Swahiyh hadi kwa Ibn ‘Abbaas].

 

Hadiyth imepokelewa na Ibn Jurayj kama alivyosema Al-Haafidhw Ibn Kathiyr (30/232) kutoka katika njia mbili kutoka kwa Al-Awzaa’iy katika mojawapo njia hizo yupo ‘Amru bin Hishaam Al-Bayruwniy mpokezi kutoka kwa Al-Awza’iy nayo ni dhaifu.

 

Na imepokewa na Al-Haakim na kusema kuwa ni Swahiyh (2/526)  imefuatiwa na maneno ya Adh-Dhahabiy: amepwekeka nayo ‘Iswaam bin Rawaad kutoka kwa baba yake na imepokewa na kudhoofishwa na Atw-Twabaraaniy katika kitabu chake Al-Kabiyr na Al-Awsatw. Al-Haythamiy amesema: na riwaayah kwenye Al-AwsatwRasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Nilionyeshwa yale ambayo Ummah wangu utafunguliwa baada ya kuondoka kwangu nikafurahishwa Allaah Akateremsha:
 

وَلَلْآخِرَةُ خَيْرٌ لَّكَ مِنَ الْأُولَىٰ ﴿٤﴾

4. Na bila shaka Aakhirah ni khayr kwako kuliko ya awali (dunia).

 

Akataja mfano wake na ndani yake Muaawiyah bin Abiy Al-‘Abbaas na sikumjua, na baki ya watu wake ni waaminifu, na Isnaad kwenye Al-Kabiyr ni Hassan, na imepokewa na Abuu Nu’aym katika Al-Hilyah (3/212) kutoka kwa Atw-Tabaraaniy na ndani yake yupo ‘Amru bin Hishaam Al-Bayruwniy kasha akasema kuwa Hadiyth ni Ghbariy (ngeni) miongoni mwa Hadiyth za ‘Aliy bin ‘Abdillaah bin ‘Abbaas na haikupokewa kutoka kwake isipokuwa Ismaa’iyl na Sufyaan Ath-Thawriy kutoka kwa Al-Awzaa’iy kutoka kwa Ismaa’iyl mfano wake.

 

Amepokea Imaam Ahmad kutoka kwa Jundub amesema, Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) aliumwa wakati fulani na hakupata kusimama ila baada ya siku moja au mbili hivi akaja mwanamke mmoja akasema, ‘Ee Muhammad simuoni shaytwaan wako isipokuwa amekuacha, Allaah Akateremsha:

 

وَالضُّحَىٰ ﴿١﴾

1. Naapa kwa dhuha.

 

وَاللَّيْلِ إِذَا سَجَىٰ ﴿٢﴾

2. Na Naapa kwa usiku unapotanda kiza na kutulia.

 

 

مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ ﴿٣﴾

3. Rabb wako Hakukutelekeza na wala Hakukuchukia (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم).

 

[Al-Bukhaariy, Muslim, At-Tirmidhiy, an-Nasaaiy, Ibn Abiy Haatim, Ibn Jariyr (Fat-h Al-Baariy (7:23) kutoka kwa Jundub huyo ni Ibn 'Abdillaah Al-Bajaliyy kisha Al-‘Alaqiyy.

 

Anasema Al-‘Awfiyy kutoka kwa Ibn ‘Abbaas, kuwa kuna wakati Qur-aan ilichelewa kumteremkia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) kwa masiku kadhaa. Mushrikina wakasema: Bwana wake Amemuacha na Amemchukia.  Allaah Akateremsha:  

 

وَالضُّحَىٰ ﴿١﴾

1. Naapa kwa dhuha.

 

وَاللَّيْلِ إِذَا سَجَىٰ ﴿٢﴾

2. Na Naapa kwa usiku unapotanda kiza na kutulia.

 

 

مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ ﴿٣﴾

3. Rabb wako Hakukutelekeza na wala Hakukuchukia (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم).

 

بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيم

 

وَالضُّحَىٰ ﴿١﴾

1. Naapa kwa dhuha.

 

وَاللَّيْلِ إِذَا سَجَىٰ ﴿٢﴾

2. Na Naapa kwa usiku unapotanda kiza na kutulia.

 

مَا وَدَّعَكَ رَبُّكَ وَمَا قَلَىٰ ﴿٣﴾

3. Rabb wako Hakukutelekeza na wala Hakukuchukia (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم).

 

وَلَلْآخِرَةُ خَيْرٌ لَّكَ مِنَ الْأُولَىٰ ﴿٤﴾

4. Na bila shaka Aakhirah ni kheri kwako kuliko ya awali (dunia).

 

وَلَسَوْفَ يُعْطِيكَ رَبُّكَ فَتَرْضَىٰ ﴿٥﴾

5. Na bila shaka Rabb wako Atakupa na utaridhika.

 

أَلَمْ يَجِدْكَ يَتِيمًا فَآوَىٰ ﴿٦﴾

6. Je, kwani Hakukukuta yatima, Akakupa makazi?

 

وَوَجَدَكَ ضَالًّا فَهَدَىٰ ﴿٧﴾

7. Na Akakukuta mpotevu Akakuongoza?

 

وَوَجَدَكَ عَائِلًا فَأَغْنَىٰ ﴿٨﴾

8. Na Akakukuta mhitaji, Akakutosheleza?

 

فَأَمَّا الْيَتِيمَ فَلَا تَقْهَرْ ﴿٩﴾

9. Kwa hivyo basi yatima usimuonee.

 

وَأَمَّا السَّائِلَ فَلَا تَنْهَرْ ﴿١٠﴾

10. Na muulizaji usimkaripie.

وَأَمَّا بِنِعْمَةِ رَبِّكَ فَحَدِّثْ ﴿١١﴾

11. Na neema ya Rabb wako ihadithie.