04-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kuhifadhi Aliyozoea Katika Mambo ya Kheri

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب المحافظة عَلَى مَا اعتاده من الخير

03-Mlango Wa Kuhifadhi Aliyozoea Katika Mambo ya Kheri

 

Alhidaaya.com

 

قَالَ الله تَعَالَى:

إِنَّ اللَّـهَ لَا يُغَيِّرُ مَا بِقَوْمٍ حَتَّىٰ يُغَيِّرُوا مَا بِأَنفُسِهِمْ ۗ  ﴿١١﴾

Hakika Allaah Habadilishi yale yaliyoko kwa watu mpaka wao wenyewe wabadilishe yale yaliyomo katika nafsi zao. [Ar-Ra'd: 11]

 

وَلَا تَكُونُوا كَالَّتِي نَقَضَتْ غَزْلَهَا مِن بَعْدِ قُوَّةٍ أَنكَاثًا ﴿٩٢﴾

Na wala msiwe kama yule mwanamke aliyezongoa uzi wake vipande vipande baada ya (kuusokota na) kuwa mgumu [An-Nahl: 92]

 

وَلَا يَكُونُوا كَالَّذِينَ أُوتُوا الْكِتَابَ مِن قَبْلُ فَطَالَ عَلَيْهِمُ الْأَمَدُ فَقَسَتْ قُلُوبُهُمْ ۖ  ﴿١٦﴾

Na wala wasiwe kama wale waliopewa Kitabu kabla, ukawatawilikia muda, kisha zikawa ngumu nyoyo zao? [Al-Hadiyd: 16]

 

فَمَا رَعَوْهَا حَقَّ رِعَايَتِهَا ۖ  ﴿٢٧﴾

Lakini hawakuuchunga ipasavyo kuchungwa. [Al-Hadiyd: 27]

 

 

Hadiyth – 1

وعن عبد الله بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما ، قَالَ : قَالَ لي رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( يَا عبْدَ الله ، لاَ تَكُنْ مِثْلَ فُلانٍ ، كَانَ يَقُومُ اللَّيْلَ فَتَرَكَ قِيَامَ اللَّيْلِ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa 'Abdillaah usiwe mfano wa fulani ambaye alikuwa akiswali Swalaah ya usiku kisha akaacha kisimamo hicho cha usiku." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Share