09-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Heshima na Utulivu

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب الوقار والسكينة

09-Mlango Wa Heshima na Utulivu

 

Alhidaaya.com

 

 

قَالَ الله تَعَالَى:

وَعِبَادُ الرَّحْمَـٰنِ الَّذِينَ يَمْشُونَ عَلَى الْأَرْضِ هَوْنًا وَإِذَا خَاطَبَهُمُ الْجَاهِلُونَ قَالُوا سَلَامًا ﴿٦٣﴾

Na waja wa Ar-Rahmaan ni wale wanaotembea katika ardhi kwa unyenyekevu na upole, na majahili wanapowasemesha, wao husema: Salaam! [Al-Furqaan: 63]

 

 

وعن عائشة رضي الله عنها ، قالت : مَا رَأيْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم مُسْتَجْمِعاً قَطُّ ضَاحِكاً حَتَّى تُرَى مِنهُ لَهَوَاتُهُ ، إنَّمَا كَانَ يَتَبَسَّمُ . متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa 'Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema: "Sijamuona Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akicheka sana mpaka nyama ya ndani kabisa katika mdomo ikaonekana. Hakika alikuwa anatabasamu tu." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Share