17-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Mawaidha Kwenye Kaburi

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب الموعظة عند القبر

17-Mlango Wa Mawaidha Kwenye Kaburi

 

Alhidaaya.com

 

 

عن عَلِيٍّ رضي الله عنه ، قَالَ : كُنَّا فِي جَنَازَةٍ في بَقيعِ الغَرْقَدِ ، فَأتَانَا رسولُ الله صلى الله عليه وسلم فَقَعَدَ ، وَقَعَدْنَا حَوْلَهُ وَمَعَهُ مِخْصَرَةٌ فَنَكَّسَ وَجَعَلَ يَنْكُتُ بِمِخْصَرَتِهِ ، ثُمَّ قَالَ : (( مَا مِنْكُمْ مِنْ أحَدٍ إِلاَّ وَقَدْ كُتِبَ مَقْعَدُهُ مِنَ النَّارِ وَمَقْعَدُهُ مِنَ الجَنَّةِ )) فقالوا : يَا رسولَ الله ، أفَلا نَتَّكِلُ عَلَى كِتَابنَا ؟ فَقَالَ : (( اعْمَلُوا ؛ فكلٌّ مُيَسرٌ لِمَا خُلِقَ لَهُ ... )) وذكَر تَمَامَ الحديث . متفقٌ عَلَيْهِ .

'Aliy (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Tulikuwa na jeneza makaburi ya Baqi' Al-Gharqad. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akatujia akakaa, tukakaa pembeni yake akiwa na bakora, Akainamisha kichwa chake na anakwaruza ardhi kwa fimbo yake. Kisha akasema: "Hakuna yoyote miongoni mwenu ila ameandikiwa kikao chake motoni na kikao chake Peponi." Wakauliza: "Ee Rasuli wa Allaah! Tutegemee katika vitabu vyetu?", Akasema: "Fanyeni kwani kila mmoja amerahisishiwa alioumbiwa (na kukuduriwa)." Na akataja Hadiyth hiyo kwa ukamilifu wake. [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Share