02-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kuchunga Qur-aan na Kutahadharishwa Kupelekea Kwenye Kuisahau

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب الأمر بتعهد القرآن والتحذير عن تعريضه للنسيان

02-Mlango Wa Kuchunga Qur-aan na Kutahadharishwa Kupelekea Kwenye Kuisahau

 

Alhidaaya.com

 

Hadiyth – 1

عن أَبي موسى رضي اللهُ عنه، عن النبيِّ صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  تعاهدوا هَذَا القُرْآنَ ، فَوَالَّذِي نَفْسُ مُحَمَّدٍ بِيَدِهِ لَهُوَ أشَدُّ تَفَلُّتاً مِنَ الإبلِ فِي عُقُلِهَا )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abu Muwsaa Al-Ash'ariy (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Ichungeni hii Qur-aan naapa kwa ambaye nafsi ya Muhammad iko mikononi mwake hakika hii Qur-aan inaponyoka haraka mno kuliko ngamia kutoka kwenye kamba yake aliyefungiwa." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Hadiyth – 2

وعن ابن عمر رضي الله عنهما : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، قَالَ : ((  إنَّمَا مَثَلُ صَاحبِ الْقُرْآنِ كَمَثَلِ الإِبِلِ المُعَقَّلَةِ ، إنْ عَاهَدَ عَلَيْهَا أمْسَكَهَا ، وَإنْ أطْلَقَهَا ذَهَبَتْ )) متفقٌ عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Ibn 'Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Hakika mfano wa mwenye kuhifadhi Qur-aan ni sawa na mwenye ngamia waliofungwa kama ataendelea kuwafunga atakuwa nao na kama atawaachilia wataondoka na kukimbia." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Share