Du'aa Gani Kuomba Unapokunywa Maji Ya Zamzam?

 

Du'aa Gani Kuomba Unapokunywa Maji Ya Zamzam?

 

Alhidaaya.com

 

Swali:

 

Asalam Aleikum wa Rahmatullah wa Barakat
 
Fadhli ni ya Subhanahu wa Ta'aalaa alojalia Ahli Alhidaaya ujuzi wa ku elimisha Umati Muhammad Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa salam.
 
Maombi yangu, ni ilimishwe "DUA" ya kuomba kabla ya kunywa maji ya zamzam wakati mtu yupo Hajj?
 
Jazakum Allaahu Kul Khair wa Asalam Aleikum wa Rahmatullah wa Barakatuh.

 
Jibu:
 

AlhamduliLLaah - Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Rabb wa walimwengu, Swalaah na salamu zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho.
 

 

Hakuna du'aa maalumu iliyopatikana kutoka katika Hadiyth Sahihi ya kuomba wakati wa kunywa maji ya zamzam. Baadhi ya du'aa zilizonukuliwa zimechambuliwa kwa dalili kuwa ni kutoka katika zile Hadiyth dhaifu. Iliyopatikana kuwa ni Swahiyh ni kwamba unaomba chochote utakacho mwenyewe wakati kunywa. Hii ni kutokana na dalili ifuatayo: 

 

(( ماء زمزم لما شرب له)) صحيح ابن ماجه  

((Maji ya zamzam kwa (jambo liloombewa) wakati wa kunywa)) [Swahiyh Ibn Maajah na imepewa daraja ya Swahiyh na Shaykh Al-Albaaniy]  
 

Na Allaah Anajua zaidi

 

Share