Fiqh Ya Kuwaita Majina Watoto

 

Fiqh Ya Majina Ya Watoto

 

Alhidaaya.com

 

 

Ni Sunnah kutunza jina zuri, na katika majina mazuri ni:

 

'Abdullaah (Mja wa Allaah Subhanahu wa Ta'aala)

na

'Abdur-Rahmaan (Mja wa Mwingi wa Rahmah);

 

na majina ya ki kweli hasa ni:

 

Al- Haarith (Anayezaa)

na

Humaam (Hodari);

 

*na majina mabaya zaidi ni:*

 

Harb (Vita)

na

Murrah (Chungu)

 

 

Hadiyth ifuatayo imethibitisha:

 

((Majina yanayopendezewa kwa Allaah (Subhaana wa Ta'aalaa) ni 'Abdullaah na Abdur-Rahmaan.)) [imeripotiwa na Muslim.

 

 

Kwa Abu Daawuud kuna nyongeza ((Na majina ya ki kweli hasa ni Al-Haarith na Humaam, na mabaya zaidi ni Harb na Murrah)).

 

 

Na majina mabaya, na yale ambayo yanamaanisha vitu vibaya katika kutokuwepo kwao, ni makuruhu (Yasiyopendeza), kama vile:

 

Nujayh (fanikiwa),

 

Barakah (baraka),

 

Kulayb (kijimbwa),

 

Harb (vita),

 

Murrah (chungu),

 

Shihaab (kimondo),

 

Himaar (punda),

 

Aflah (fanikiwa sana),

 

Yasaar (wepesi),

 

Rabaah (faida), na

 

Naafi` (kunufaika)

 

na majina kama:

 

Sittun-nisaa (mwanamke wa wanawake wote)  ni yanayogombezewa sana. 

 

Na Mfalme wa Wafalme limekatazwa, kama ilivyokuwa:

 

'Shahenshaah',

 

na

 

Aqdhwaal-Qudhwaat (hakimu wa mahakimu).

 

 

Na inapendelewa kubadilisha majina mabaya na ambayo yanamaanisha vitu vibaya katika kutokuwepo kwao.

 

 

Na inapendelewa kwa mtoto wa kiume, mwanafunzi au mfanyakazi kutomwita kwa jina lake, na kwamba watu wazuri (wanaume na wanawake) wawe wana kun-yah, hata ikiwa hawana watoto wa kiume, na kun-yah huhusiana na mtoto wa kiume wa mwanzo.

 

 

Na imekatazwa kuwa na Kun-yah ya 'Abul-Qaasim kwa mtu ambaye jina lake ni Muhammad na vile vile kwa watu wengine, katika kipindi cha Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  na vile vile baadae ya hapo.

 

 

Tanbihi:

 

Kuna khitilafu baina ya madhehebu juu katika nukta hii- wengine wameshika kwamba katazo lake (kutumia kun-yah ya Abul-Qaasim) liliwekwa katika kipindi cha uhai wa Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) tu na si baada ya kufariki.

 

 

Na aliyeruka mipaka (faasiq) au mzushi asipewe kun-yah mpaka kukiwepo hofu ya fitnah, au ikiwa kwa sababu ya utambulishi, (kama vile Abu Lahab).

 

 

Na inapendelewa kwamba mtu asitumie kun-yah yake pekee (yaani bila ya kutimiza jina lake pia), isipokuwa akiwa anajulikana kwa kun-yah yake na sio kwa jina lolote isipokuwa hilo.

 

 

Na pia imekatazwa (Haraam) kumtania mtu kwa jina ambalo halipendi. Kama ikiwa anajulikana kwa jina jengine (ambalo halimchukizi) na hata kama jina hilo lina dhamiria kitu ambacho kinamhusu yeye ambacho ni cha kweli.

 

 

Kun-yah (Lakabu au Jina la kupachika)

Ushahidi uliombwa wa kuchukuliwa kun-yah kuwa ni Sunnah. Kuna vidokezo mbali mbali juu ya hili katika Hadiyth.

 

 

Mtume  (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa na kun-yah, na hakuna ushahidi wowote wa kuonyesha kwamba kuwa na kun-yah ilikuwa kwa yeye pekee, na hii ndio inayoamua ni Sunnah (kumfuata mtu katika kitu ambacho hakikua kwa ajili yake pekee (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam).

 

 

 

Zaidi, kuna Hadiyth iliyoripotiwa na At-Tirmidhiy katika "Ash-Shamaail"

 

 

Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimwita mvulana mdogo kwa kun-yah, kuonyesha kwamba si muhimu kuwa na mtoto kabla ya kutumia kun-yah.

 

 

Mazungumzo zaidi ya Hadiyth hizi yanapatikana katika Fat-h al-Baariy (maelezo ya Swahiyh Al-Bukhaariy).

 

 

 

 

 

Share