Anaweza Kumlipia Mumewe Gharama Za Kwenda Hijjah?

 

Anaweza Kumlipia Mumewe Gharama Za Kwenda Hijjah?

 

Alhidaaya.com

 

 

Swali:

 

Assalaam Alaykum Warahmaturllaah Taallah  wabarakatu.

 

Namshukuru Allaah mtukufu aliyewapa uwezo wa kutuelimisha. Ninamuomba Rabb wetu mtukufu awajaalie kila la kheri. Nashukuru jibu lenu mlilonijibu limezaa matunda mema Allaah mtukufu awatilie wepesi. kwani kutokana na ushauli wenu nikaenda kumlingania mme wangu.alhamdu lillaah rabbi l'alamiina sasa ameacha pombe na anaswali swala tano. Allaah mtukufu awabarikiinshaallah amiin!.

 

Sasa swali langu naweza kwenda naye hijja kwa gharama zangu?.

 

 

Jibu:

 

AlhamduliLLaah - Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Rabb wa walimwengu, Swalaah na salamu zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

 

Tunashukuru kujua kwamba nasaha zetu zimekusaidia na umeweza kuwa sababu ya kuongoka mumeo kwa idhini ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa). Inapasa umshukuru Rabb Mtukufu kwani Yeye Ndiye Mwenye kuwahidi waja Wake, sisi ni njia tu za kupitia kupata uongofu kama huo.

 

 

Ama kuhusu kumlipia kwenda Hajj, na kwenda naye pamoja, inafaa ikiwa unao uwezo na umependa mwenyewe. Hili ni jambo jema kabisa khaswa kwa vile mumeo alitoka kwenye maasi na kuingia katika twaa'a (Uchaji Allaah). Kwa hiyo ni vizuri kukimbilia kutekeleza ibada/fardhi hiyo muhimu ili Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Azidi kumuongoza katika njia iliyonyooka.

 

 

Tunamuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Awazidishie iymaan ya dini Yenu na mzidi kubakia katika ridhaa Yake Rabb Mtukufu.

 

 

Na Allaah Anajua

 

 

Share