Pilau Ya Mpunga Kwa Nyama Ya Ng’ombe

Pilau Ya Mpunga Kwa Nyama Ya Ng’ombe

 

Vipimo

Mchele (mpunga unaonukia)   - 4 vikombe

Nyama  - 1 kilo moja

Kitunguu maji  -  3

Mbatata/viazi - 7 vidogodogo

Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi ilosagwa  3 vijiko cha supu

Bizari nzima/ya pilau/uzile/cumin  - 3 vijiko vya supu

Mdalasini  - 3 vipande

Hiliki  - 7 punje

Pilipili manga nzima  - 1 kijiko cha supu

Chumvi kiasi

Mafuta  -   ½ kikombe

 

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

  1. Osha mchele weka kando
  2. Katakataka vitunguu slice ndogo ndogo.
  3. Weka mafuta katika sufuria kisha ukaange vitunguu pamoja na mdalasini, hiliki pilipilimanga.
  4. Vitunguu vikigeuka rangi unatia kitunguu thomu na tangawizi.
  5. Tia supu kidogo na nyama, kisha tia bizari ya pilau/uzile, na viazi/mbatata.
  6. Maliza kutia supu yote, na ikiwa ni kidogo ongeze maji kiasi cha kuivisha mchele. kisha tia mchele ufunike hadi wali uwe tayari.
  7. Ikiwa unatumia mkaa palia juu yake, ikiwa hutumii uache uive kwa moto mdogo mdogo.

 

Share