Shaykh Fawzaan: Si Kila Anayedai Usalafi Ni Salafi

 

Si Kila Anayedai Usalafi Ni Salafi

 

Shaykh Swaalih Al-Fawzaan (Hafidhwahu Allaah)

 

Alhidaaya.com

 

 

Shaykh Swaalih Al-Fawzaan (Hafidhwahu Allaah) amesema:

 

“Si kila anayedai Usalafi, anakuwa (Salafi).

Wameudai (Usalafi) watu (Wajinga) wasiojua Manhaj ya Salafi.

Na wakadai (Usalafi) watu (wanaopiga vita) wanaojihusisha na Manhaj ya Khawaarij kwa kumwaga damu na kuleta ufisadi ardhini.

Na wakadai (Usalafi) watu (wanaojidai wana elimu) ambao hawajachukua elimu kutoka kwa ‘Ulamaa, bali wamechukua kutoka kwenye vitabu na kujisomea na kuhifadhi Nuswuwsw (maandiko) kwa ufahamu tu (binafsi).

 

Na Allaah (Subhaanahu) Anasema:

 

وَالسَّابِقُونَ الْأَوَّلُونَ مِنَ الْمُهَاجِرِينَ وَالْأَنصَارِ وَالَّذِينَ اتَّبَعُوهُم بِإِحْسَانٍ

 Na wale waliotangulia awali (katika Uislamu) miongoni mwa Muhajirina na Answaar na wale waliowafuata kwa ihsaan

 

 (Kwa ihsaan) yaani: kwa itqaan (usahihi, ufanisi)

 

[Haqiyqatu Al-Manhaj As-Salafiy, uk. 65]

 

 

 

 

Share