Skip to main content

Mukhtasari Wa ‘Aqiydah Ya Muislamu

Maswali Na Majibu Pamoja Na Dalili Kutoka Qur-aan Na Sunnah.

Imetarjumiwa na: Alhidaaya.com

54-Je, Ipo Sunnatun-hasanah katika Uislamu?

Naam, ipo Sunnatun-hasanah (Sunnah nzuri) katika Uislamuu kama vile anayeanza kufanya kitendo chema cha kheri akafuatwa.

 وَاجْعَلْنَا لِلْمُتَّقِينَ إِمَامًا ﴿٧٤﴾

Na Tujaalie kuwa waongozi kwa wenye taqwa.  [Al-Furqaan: 74]

((مَنْ سَنَّ فِي الإِسْلامِ سُنَّةً حَسَنَةً فَلَهُ أَجْرُهَا وَأَجْرُ مَنْ عَمِلَ بِهَا مِنْ بَعْدِه )) مسلم

"Atakayeanzisha mwenendo mwema " سُنَّةً حَسَنَةً katika Uislamu atapata ujira wake na ujira wa atakayetenda wema huo." [Muslim]