Zingatio

Zingatio La Wiki,

Zingatio

 

 

Ni kutokana na ujinga na dharau zetu ndio tumeufikisha Uislamu kwenye hali iliyopo sasa. Sio tu kwa kukosa dira ya kufuata au Kitabu cha kusoma, la sivyo! Bali pia ni kwa kuwafanya maadui wa Uislamu kuwa ni wenzetu wa karibu mno kuliko hata ndugu wa Kiislamu walio na imani thabiti.

Zingatio

Kwa maisha ya leo yalivyo, ustaarabu ambao unafanana na wa mnyama, utaonekana ni mtu wa maajabu kutoa kauli ya kwamba muziki haufai kabisa kabisa. Badala yake, ndio kwanza wanatengeneza matamasha na kuyaita: "Save The Music" yaani "Linda/Hifadhi Muziki (usipotee)". Na si wengine wenye kuyaandaa hayo isipokuwa wanaojiita Waislamu!