Skip to main content

11D-Swahiyh Fiqh As-Sunnah: كِتَابُ الفَرْق بَيْنَ الزَّوْجَيْنِ Kitabu Cha Kutengana Mke Na Mume: الطَّلَاقُ المُنَجَّزُ والمُضَافُ والمُعَلَّقُ Talaka Inayopita Hapo Hapo Inapotolewa, Talaka Inayofungamanishwa Na Wakati, Na Talaka Inayofungamani01-Swahiyh Fiqh As-Sunnah: كِتَابُ الفَرْق بَيْنَ الزَّوْجَيْنِ Kitabu Cha Kutengana Mke Na Mume: Talaka Inayopita Hapo Hapo Inapotolewa, Talaka Inayofungamanishwa Na Wakati, Na Talaka Inayofungamanishwa Na Jambo Fulani

Swahiyh Fiqh As-Sunnah

كِتَابُ الفَرْق بَيْنَ الزَّوْجَيْنِ

Kitabu Cha Kutengana Mke Na Mume 

الطَّلَاقُ المُنَجَّزُ والمُضَافُ والمُعَلَّقُ

Talaka Inayopita Hapo Hapo Inapotolewa, Talaka Inayofungamanishwa Na Wakati, Na Talaka Inayofungamanishwa Na Jambo Fulani 

Alhidaaya.com 

01: Talaka Inayopita Hapo Hapo"الطَّلّاقُ المُنَجَّزُ" :

Ni talaka ambayo kwenye tamko lake hakuna sharti lolote aliloliweka mume, au akaifungamanisha na wakati ujao, bali anaikusudia ipite hapo hapo.  Ni kama kumwambia mkewe:  "Nimekuacha". 

Hukmu Yake:

Talaka hii hupita, na huwa ni sababu ya mke na mume kuachana, na itafuatiwa moja kwa moja na athari za talaka.  Mume akimwambia mkewe: "Nimekutaliki", basi anakuwa moja kwa moja ameachika, na ataanza eda yake ikiwa ni katika wenye kupata hedhi.