Skip to main content

11A-Swahiyh Fiqh As-Sunnah: Kitabu Cha كتاب الفرق بين الزوجين - Kitabu Cha Kutengana Mke Na Mume16-Swahiyh Fiqh As-Sunnah: Kitabu Cha Talaka Kutengana Mke Na Mume: Aina Za Talaka

Swahiyh Fiqh As-Sunnah

كِتَابُ الفَرْق بَيْنَ الزَّوْجَيْنِ

Kitabu Cha Kutengana Mke Na Mume 

الطَّلَاقُ

Talaka

Alhidaaya.com 

16:  Aina Za Talaka:

Kwa jinsi picha yake ilivyo, talaka inaweza kugawanywa katika aina mbalimbali.

1-  Kwa upande wa tamko linalotumika, iko aina mbili: 

(a) Talaka ya tamko wazi. 

(b) Talaka ya tamko fumbo.  Hili lishazungumzwa nyuma. 

2- Kwa upande wa athari inayotokana nayo, iko aina mbili pia. 

(a) Talaka rejea "طَلَاقٌ رَجْعِي"

(b)  Talaka mtengano, utengano mdogo au mkubwa "طَلَاقٌ بَائِنٌ بَيْنُونَةٌ صُغْرَى أَوْ كُبْرَى"

3- Kwa upande wa sifa yake, iko vilevile aina mbili. 

(a) Ya kisunnah   "طَلَاقٌ سُنِّيٌّ"(ya kishari'ah).

(b) Ya kibid-'ah "طَلَاقٌ بِدْعِيٌّ" (iliyo kinyume na shari'ah). 

4- Kwa upande wa wakati wa kutokea athari itokanayo kwayo, iko ya aina tatu: 

(a) Inayopita hapo hapo inapotolewa.  (Kwa mfano mume akimwambia mkewe:  "Nimekutaliki", mke anakuwa hapo hapo ashaachika).

(b)  Iliyofungamanishwa na sharti.  (Ni kama mume kumwambia mkewe:  "Ukifanya jambo fulani basi umeachika", ikiwa atafanya jambo hilo, basi anakuwa ameachika). 

(c) Iliyotegemezwa na wakati ujao.  (Ni kama mume kumwambia mkewe:  "Nimekutaliki kesho").

Na hebu sasa tuangalie uchanganuzi wa aina zote hizi na hukumu za kila moja.