Asbaabun-Nuzuwl

Asbaabun-Nuzuwl

Asbaabun-Nuzuwl

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

 

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

048-Al-Fat-h: Aayah 1 - 5

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّا فَتَحْنَا لَكَ فَتْحًا مُّبِينًا﴿١﴾

Hakika Tumekupa ushindi (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم), ushindi bayana.

 

لِّيَغْفِرَ لَكَ اللَّـهُ مَا تَقَدَّمَ مِن ذَنبِكَ وَمَا تَأَخَّرَ وَيُتِمَّ نِعْمَتَهُ عَلَيْكَ وَيَهْدِيَكَ صِرَاطًا مُّسْتَقِيمًا﴿٢﴾

Ili Allaah Akughufurie yale yaliyotangulia katika madhambi yako na yale yanayofuatia; na Akutimizie neema Yake juu yako na Akuongoze njia iliyonyooka.

 

وَيَنصُرَكَ اللَّـهُ نَصْرًا عَزِيزًا﴿٣﴾

Na Akunusuru Allaah nusura yenye nguvu kabisa.

 

هُوَ الَّذِي أَنزَلَ السَّكِينَةَ فِي قُلُوبِ الْمُؤْمِنِينَ لِيَزْدَادُوا إِيمَانًا مَّعَ إِيمَانِهِمْ ۗ وَلِلَّـهِ جُنُودُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۚ وَكَانَ اللَّـهُ عَلِيمًا حَكِيمًا﴿٤﴾

Yeye Ndiye Aliyeteremsha utulivu katika nyoyo za Waumini ili Awazidishie iymaan pamoja na iymaan zao. Na ni ya Allaah Pekee majeshi ya mbinguni na ardhini, na Allaah ni daima Mjuzi wa yote, Mwenye hikmah wa yote.

 

لِّيُدْخِلَ الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا وَيُكَفِّرَ عَنْهُمْ سَيِّئَاتِهِمْ ۚ وَكَانَ ذَٰلِكَ عِندَ اللَّـهِ فَوْزًا عَظِيمًا﴿٥﴾

Ili Awaingize Waumini wa kiume na Waumini wa kike Jannaat zipitazao chini yake mito, ni wenye kudumu humo, na Awafutie maovu yao; na kukawa huko mbele ya Allaah, ni kufuzu adhimu.

 [[Al-Fat-h: 1 – 5]

 

 

Sababun-Nuzuwl: 

 

 

عَنْ أَنَسٍ ابن مالك رضى الله عنه  قَالَ لَمَّا نَزَلَتْ: ((إِنَّا فَتَحْنَا لَكَ فَتْحًا مُبِينًا * لِيَغْفِرَ لَكَ اللَّهُ‏))  إِلَى قَوْلِهِ: ((‏فَوْزًا عَظِيمًا‏))‏ مَرْجِعَهُ مِنَ الْحُدَيْبِيَةِ وَهُمْ يُخَالِطُهُمُ الْحُزْنُ وَالْكَآبَةُ وَقَدْ نَحَرَ الْهَدْىَ بِالْحُدَيْبِيَةِ فَقَالَ ‏"‏ لَقَدْ أُنْزِلَتْ عَلَىَّ آيَةٌ هِيَ أَحَبُّ إِلَىَّ مِنَ الدُّنْيَا جَمِيعًا ‏"‏ ‏.‏

 Anas bin Maalik (رضي الله عنه) amesema:  Ilipoteremka:

 

إِنَّا فَتَحْنَا لَكَ فَتْحًا مُّبِينًا﴿١﴾

Mpaka kauli Yake:

فَوْزًا عَظِيمًا

Alipokuwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) na Maswahaba  wanarudi kutoka Hudaybiyah wakiwa katika hali ya kuzidiwa na  ghadhabu, huzuni na dhiki (kwa kuzuiliwa na Makafiri Quryash kuingia Makkah) Wakawa wamechinja Hady (mnyana wa Hajj) wao. (Hapo zikateremshwa Aayah hizo) na Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: “Hakika nimeteremshiwa Aayah ambazo ni vipenzi zaidi kuliko dunia nzima.”  [Muslim Kitaab Al-Jihaad Was Sayr]    

 

 

Pia,

 

عَنْ أَنَسٍ ابن مالك رضى الله عنه:  ((إِنَّا فَتَحْنَا لَكَ فَتْحًا مُّبِينًا))  قالَ الْحُدَيْبِيَةُ‏.‏ قَالَ أَصْحَابُهُ هَنِيئًا مَرِيئًا فَمَا لَنَا?  فَأَنْزَلَ اللَّهُ : ‏ ‏((لِيُدْخِلَ الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ جَنَّاتٍ‏))  قَالَ شُعْبَةُ فَقَدِمْتُ الْكُوفَةَ فَحَدَّثْتُ بِهَذَا كُلِّهِ عَنْ قَتَادَةَ ثُمَّ رَجَعْتُ فَذَكَرْتُ لَهُ فَقَالَ أَمَّا:  ‏((‏إِنَّا فَتَحْنَا لَكَ‏))‏ فَعَنْ أَنَسٍ، وَأَمَّا هَنِيئًا مَرِيئًا فَعَنْ عِكْرِمَةَ‏.

Anas bin Maalik (رضي الله عنه) amesema kuhusu:

إِنَّا فَتَحْنَا لَكَ فَتْحًا مُّبِينًا

Inahusiana na (Bay’ah) ya Hudaybiyah.  Maswahaba wa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) wakasema kumwambia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): “Hongera na furaha kwako, lakini je sisi tunapata nini?” Hapo Allaah Akateremsha:

 

لِّيُدْخِلَ الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا وَيُكَفِّرَ عَنْهُمْ سَيِّئَاتِهِمْ ۚ وَكَانَ ذَٰلِكَ عِندَ اللَّـهِ فَوْزًا عَظِيمًا﴿٥﴾

Ili Awaingize Waumini wa kiume na Waumini wa kike Jannaat zipitazao chini yake mito, ni wenye kudumu humo, na Awafutie maovu yao; na kukawa huko mbele ya Allaah, ni kufuzu adhimu. [Al-Bukhaariy]

 

Pia,

 

Bonyeza Endelea...

 

Asbaabun-Nuzuwl

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

 

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

049-Al-Hujuraat  11

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا يَسْخَرْ قَوْمٌ مِّن قَوْمٍ عَسَىٰ أَن يَكُونُوا خَيْرًا مِّنْهُمْ وَلَا نِسَاءٌ مِّن نِّسَاءٍ عَسَىٰ أَن يَكُنَّ خَيْرًا مِّنْهُنَّ ۖ وَلَا تَلْمِزُوا أَنفُسَكُمْ وَلَا تَنَابَزُوا بِالْأَلْقَابِ ۖ بِئْسَ الِاسْمُ الْفُسُوقُ بَعْدَ الْإِيمَانِ ۚ وَمَن لَّمْ يَتُبْ فَأُولَـٰئِكَ هُمُ الظَّالِمُونَ﴿١١﴾

Enyi walioamini! Wanaume wasiwafanyie dhihaka na kudharau wanaume wengineo asaa wakawa bora kuliko wao, wala wanawake kwa wanawake wengineo, asaa wakawa bora kuliko wao. Na wala msifedheheshane na kutukanana na wala msiitane majina ya kejeli. Ubaya ulioje kuita jina la ufasiki baada ya iymaan. Na yeyote asiyetubu, basi hao ndio madhalimu. [Al-Hujuraat: 11]

 

 

Sababun-Nuzuwl: 

 

حَدَّثَنَا مُوسَى بْنُ إِسْمَاعِيلَ، حَدَّثَنَا وُهَيْبٌ، عَنْ دَاوُدَ، عَنْ عَامِرٍ، قَالَ حَدَّثَنِي أَبُو جُبَيْرَةَ بْنُ الضَّحَّاكِ،  قَالَ فِينَا نَزَلَتْ هَذِهِ الآيَةُ فِي بَنِي سَلِمَةَ: ((وَلاَ تَنَابَزُوا بِالأَلْقَابِ بِئْسَ الاِسْمُ الْفُسُوقُ بَعْدَ الإِيمَانِ))قَالَ قَدِمَ عَلَيْنَا رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم وَلَيْسَ مِنَّا رَجُلٌ إِلاَّ وَلَهُ اسْمَانِ أَوْ ثَلاَثَةٌ فَجَعَلَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم يَقُولُ ‏"‏ يَا فُلاَنُ ‏"‏ ‏.‏ فَيَقُولُونَ مَهْ يَا رَسُولَ اللَّهِ إِنَّهُ يَغْضَبُ مِنْ هَذَا الاِسْمِ فَأُنْزِلَتْ هَذِهِ الآيَةُ: ((وَلاَ تَنَابَزُوا بِالأَلْقَابِ))

 

Ametuhadithia Muwsaa ibn Ismaa’iyl, ametuhadithia Wuhayb, kutoka kwa Daawuwd, kutoka kwa ‘Aamir amesema: ametuhadithia Jubayrah ibn Adhw-Dhwahaak ambaye amesema:  Aayah hii imeteremshwa kwa ajili yetu Bani Salimah:

 

وَلاَ تَنَابَزُوا بِالأَلْقَابِ بِئْسَ الاِسْمُ الْفُسُوقُ بَعْدَ الإِيمَان

Na wala msiitane majina ye kejeli. Ubaya ulioje kuita jina la ufasiki baada ya iymaan.

 

Akasema: Pindi Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alipotufikia, kila mmoja wetu alikuwa ana majina mawili au matatu.  Basi Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akawa Anasema:  “Ee fulani!” Lakini wao husema: Ee Rasuli wa Allaah (Usimwite kwa jina hilo), hakika yeye hughadhibika kuitwa kwa jina hilo!  Basi hapo ikateremshwa Aayah hii:

وَلاَ تَنَابَزُوا بِالأَلْقَابِ  

Na wala msiitane majina ya kejeli. 

 

[Abuu Daawuwd, Ibn Maajah, At-Tirmidhiy, ameisahihisha Al-Albaaniy: Swahiyh Abiy Daawuwd (4962), Swahiyh Ibn Maajah (3030), Swahiyh At-Tirmidhiy (3268),Swahiyh Adab Al-Mufrad (251)]

 

Asbaabun-Nuzuwl

 

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

 

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

049-Al-Hujuraat  Aayah 9

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

  وَإِن طَائِفَتَانِ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ اقْتَتَلُوا فَأَصْلِحُوا بَيْنَهُمَا ۖ فَإِن بَغَتْ إِحْدَاهُمَا عَلَى الْأُخْرَىٰ فَقَاتِلُوا الَّتِي تَبْغِي حَتَّىٰ تَفِيءَ إِلَىٰ أَمْرِ اللَّـهِ ۚ فَإِن فَاءَتْ فَأَصْلِحُوا بَيْنَهُمَا بِالْعَدْلِ وَأَقْسِطُوا ۖ إِنَّ اللَّـهَ يُحِبُّ الْمُقْسِطِينَ﴿٩﴾

Na ikiwa makundi mawili ya Waumini yakipigana, basi suluhisheni baina yao. Lakini mojawapo likikandamiza jengine, basi piganeni na ambalo linakandamiza mpaka lielemee kwenye amri ya Allaah. Likishaelemea, basi suluhisheni baina yao kwa uadilifu, na timizeni haki. Hakika Allaah Anapenda wanaotimiza haki.

 

إِنَّمَا الْمُؤْمِنُونَ إِخْوَةٌ فَأَصْلِحُوا بَيْنَ أَخَوَيْكُمْ ۚ وَاتَّقُوا اللَّـهَ لَعَلَّكُمْ تُرْحَمُونَ﴿١٠﴾

Hakika Waumini ni ndugu, basi suluhisheni baina ya ndugu zenu. Na mcheni Allaah ili mpate kurehemewa.  [Al-Hujuraat: 9-10]

 

Sababun-Nuzuwl: 

 

عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ قَالَ قِيلَ لِلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم لَوْ أَتَيْتَ عَبْدَ اللَّهِ بْنَ أُبَىٍّ قَالَ فَانْطَلَقَ إِلَيْهِ وَرَكِبَ حِمَارًا وَانْطَلَقَ الْمُسْلِمُونَ وَهِيَ أَرْضٌ سَبِخَةٌ فَلَمَّا أَتَاهُ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم قَالَ إِلَيْكَ عَنِّي فَوَاللَّهِ لَقَدْ آذَانِي نَتْنُ حِمَارِكَ ‏.‏ قَالَ فَقَالَ رَجُلٌ مِنَ الأَنْصَارِ وَاللَّهِ لَحِمَارُ رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم أَطْيَبُ رِيحًا مِنْكَ - قَالَ - فَغَضِبَ لِعَبْدِ اللَّهِ رَجُلٌ مِنْ قَوْمِهِ - قَالَ - فَغَضِبَ لِكُلِّ وَاحِدٍ مِنْهُمَا أَصْحَابُهُ - قَالَ - فَكَانَ بَيْنَهُمْ ضَرْبٌ بِالْجَرِيدِ وَبِالأَيْدِي وَبِالنِّعَالِ - قَالَ - فَبَلَغَنَا أَنَّهَا نَزَلَتْ فِيهِمْ ‏   ((وَإِنْ طَائِفَتَانِ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ اقْتَتَلُوا فَأَصْلِحُوا بَيْنَهُمَا))

Imepokelewa kutoka kwa Anas bin Maalik (رضي الله عنه) kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) aliambiwa: Unaonaje umwendee ‘Abdullaah bin Ubayy (umlinganie Uislamu). Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akamwendea akiwa amepanda punda, na (kundi la) Waislamu walienda (naye) wakitembea katika ardhi kavu iliyo na chumvi. Pindi Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alipomfikia, (‘Abdullaah bin Ubayy) alisema:  “Jiepushe mbali nami! Naapa kwa Allaah harufu mbaya ya punda wako imenikera.”  Mtu mmoja katika Answaariy akasema (kumwambia ‘Abdullaah bin ‘Ubayy): “Naapa kwa Allaah punda wa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) ana harufu nzuri zaidi kulikoni yako!” Hapo mtu mmoja katika kabila ya ‘Abdullaah akaghadhibika kwa ajili ya aliyoaambiwa ‘Abdullaah, kisha hao watu wawili wakawa wanashutumiana ikasababisha maswahibu wa hao wawili kughadhibika. Makundi mawili ya watu hao  yakaanza kupigana kwa vitawi, viatu na makofi.  Tukajulishwa kwamba imeteremshwa:

 

وَإِن طَائِفَتَانِ مِنَ الْمُؤْمِنِينَ اقْتَتَلُوا فَأَصْلِحُوا بَيْنَهُمَا ۖ  

Na ikiwa makundi mawili ya Waumini yakipigana, basi suluhisheni baina yao….

 

 

Asbaabun-Nuzuwl

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

049-Al-Hujuraat: 2

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

  

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَرْفَعُوا أَصْوَاتَكُمْ فَوْقَ صَوْتِ النَّبِيِّ وَلَا تَجْهَرُوا لَهُ بِالْقَوْلِ كَجَهْرِ بَعْضِكُمْ لِبَعْضٍ أَن تَحْبَطَ أَعْمَالُكُمْ وَأَنتُمْ لَا تَشْعُرُونَ﴿٢﴾

Enyi walioamini! Msipandishe sauti zenu juu ya sauti ya Nabiy, na wala msiseme naye kwa sauti ya juu, kama mnavyosemezana wenyewe kwa wenyewe kwa sauti za juu; zisije zikaporomoka ‘amali zenu nanyi hamhisi. [Al-Hujuraat: 2]

 

Sababun-Nuzuwl: 

 

حَدَّثَنَا يَسَرَةُ بْنُ صَفْوَانَ بْنِ جَمِيلٍ اللَّخْمِيُّ، حَدَّثَنَا نَافِعُ بْنُ عُمَرَ، عَنِ ابْنِ أَبِي مُلَيْكَةَ، قَالَ كَادَ الْخَيِّرَانِ أَنْ يَهْلِكَا ـ أَبَا بَكْرٍ وَعُمَرَ ـ رضى الله عنهما ـ رَفَعَا أَصْوَاتَهُمَا عِنْدَ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم حِينَ قَدِمَ عَلَيْهِ رَكْبُ بَنِي تَمِيمٍ، فَأَشَارَ أَحَدُهُمَا بِالأَقْرَعِ بْنِ حَابِسٍ أَخِي بَنِي مُجَاشِعٍ، وَأَشَارَ الآخَرُ بِرَجُلٍ آخَرَ ـ قَالَ نَافِعٌ لاَ أَحْفَظُ اسْمَهُ فَقَالَ أَبُو بَكْرٍ لِعُمَرَ مَا أَرَدْتَ إِلاَّ خِلاَفِي‏.‏ قَالَ مَا أَرَدْتُ خِلاَفَكَ‏.‏ فَارْتَفَعَتْ أَصْوَاتُهُمَا فِي ذَلِكَ، فَأَنْزَلَ اللَّهُ: ((يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَرْفَعُوا أَصْوَاتَكُمْ فَوْقَ صَوْتِ النَّبِيِّ))   الآيَةَ‏.‏ قَالَ ابْنُ الزُّبَيْرِ:  فَمَا كَانَ عُمَرُ يُسْمِعُ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم بَعْدَ هَذِهِ الآيَةِ حَتَّى يَسْتَفْهِمَهُ‏.‏ وَلَمْ يَذْكُرْ ذَلِكَ عَنْ أَبِيهِ، يَعْنِي أَبَا بَكْرٍ‏.‏

Ametuhadithia Yasarah bin Swafwaan bin Jamiyl Al-Llakhmiyy, ametuhadithia Naafi’ ibn ‘Umar, kutoka kwa Ibn Abiy Mulaykah (رضي الله عنه) kwamba watu wema wawili  walikaribia kuangamia; nao ni Abuu Bakr na ‘Umar(رضي الله عنهما) , walipandisha sauti zao mbele ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) pindi walipomjia wajumbe kutoka Baniy Tamiym.  Mmoja wao kati ya wawili hao alipendelea (achaguliwe) Al-Aqra’ bin Haabis kaka yake Baniy Mujaashi’ (awe gavana wao), na wa pili alipendelea mtu mwengine. (Naafi’ mmoja wa msimuliaji alisema “Sikumbuki jina lake.”) Abuu Bakr alimwambia ‘Umar: ’Hukukusudia isipokuwa kunipinga.’ ‘Umar akasema ’Sikukusudia kukupinga.’ Basi sauti zao zikapaza katika kubishana kwao huko; hapo Allaah  Akateremsha:

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَرْفَعُوا أَصْوَاتَكُمْ  

Enyi walioamini! Msipandishe sauti zenu juu ya sauti ya Nabiy...    

 

Ibn Zubayr akasema: “Tokea ilipoteremka Aayah hii, ‘Umar akawa anaongea kwa sauti ndogo mno kiasi kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alikuwa akimuomba arudie kauli yake (apate kumfahamu). Ibn Zubayr hakutaja hivyo kuhusu babu yake wa (upande wa mama) yaani Abuu Bakr.”  [Al-Bukhaariy]

 

Na pia,

 

عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ، أَنَّهُ قَالَ لَمَّا نَزَلَتْ هَذِهِ الآيَةُ: ((يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَرْفَعُوا أَصْوَاتَكُمْ فَوْقَ صَوْتِ النَّبِيِّ))   إِلَى آخِرِ الآيَةِ جَلَسَ ثَابِتُ بْنُ قَيْسٍ فِي بَيْتِهِ وَقَالَك أَنَا مِنْ أَهْلِ النَّارِ ‏.‏ وَاحْتَبَسَ عَنِ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم فَسَأَلَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم سَعْدَ بْنَ مُعَاذٍ فَقَالَ: ‏"‏يَا أَبَا عَمْرٍو مَا شَأْنُ ثَابِتٍ أَشْتَكَى‏"‏ ‏.‏ قَالَ سَعْدٌ إِنَّهُ لَجَارِي وَمَا عَلِمْتُ لَهُ بِشَكْوَى‏.‏ قَالَ: فَأَتَاهُ سَعْدٌ فَذَكَرَ لَهُ قَوْلَ رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ ثَابِتٌ: أُنْزِلَتْ هَذِهِ الآيَةُ وَلَقَدْ عَلِمْتُمْ أَنِّي مِنْ أَرْفَعِكُمْ صَوْتًا عَلَى رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَأَنَا مِنْ أَهْلِ النَّارِ‏.‏ فَذَكَرَ ذَلِكَ سَعْدٌ لِلنَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم: ‏"‏بَلْ هُوَ مِنْ أَهْلِ الْجَنَّةِ ‏"‏ ‏.‏

 

Anas bin Maalik amehadithia kuwa pindi ilipoteremka Aayah hii:

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَرْفَعُوا أَصْوَاتَكُمْ فَوْقَ صَوْتِ النَّبِيِّ وَلَا تَجْهَرُوا لَهُ بِالْقَوْلِ كَجَهْرِ بَعْضِكُمْ لِبَعْضٍ أَن تَحْبَطَ أَعْمَالُكُمْ وَأَنتُمْ لَا تَشْعُرُونَ﴿٢﴾

Enyi walioamini! Msipandishe sauti zenu juu ya sauti ya Nabiy, na wala msiseme naye kwa sauti ya juu, kama mnavyosemezana wenyewe kwa wenyewe kwa sauti za juu; zisije zikaporomoka ‘amali zenu nanyi hamhisi. [Al-Hujuraat: 2]

 

Thaabit bin Qays alijizuia nyumbani kwake akasema: “Mimi ni katika watu wa Motoni.” Akawa anamwepuka Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم), naye akamuuliza Mu’aadh akasema: ((Ee Abaa ‘Amruw, vipi Thaabit, je anaumwa?)) Sa’ad akasema: “Yeye ni jirani yangu lakini sijui kuhusu kuumwa kwake.”  Sa’ad akamwendea (Thaabit) akamtajia kuhusu alivyouliziwa na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم), Thaabit akasema: “Aayah hii imeteremshwa na ilhali nyote mnatambua kwamba sauti yangu inapaza zaidi mbele ya Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) kulikoni sauti zenu, na hivyo mimi ni miongoni mwa watu wa Motoni.”  Sa’ad akamtajia hivyo Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) basi Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: ((Hapana, yeye ni katika watu wa Jannah [Peponi])). [Muslim]

 

Na pia,

 

عن عبد الله بن زبير رضي الله عنه:  أَنَّ الأَقْرَعَ بْنَ حَابِسٍ، قَدِمَ عَلَى النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ أَبُو بَكْرٍ يَا رَسُولَ اللَّهِ اسْتَعْمِلْهُ عَلَى قَوْمِهِ ‏.‏ فَقَالَ عُمَرُ لاَ تَسْتَعْمِلْهُ يَا رَسُولَ اللَّهِ ‏.‏ فَتَكَلَّمَا عِنْدَ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم حَتَّى ارْتَفَعَتْ أَصْوَاتُهُمَا فَقَالَ أَبُو بَكْرٍ لِعُمَرَ مَا أَرَدْتَ إِلاَّ خِلاَفِي ‏.‏ فَقَالَ عُمَرُ مَا أَرَدْتُ خِلاَفَكَ قَالَ فَنَزَلَتْ هَذِهِ الآيَةُ يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَرْفَعُوا أَصْوَاتَكُمْ فَوْقَ صَوْتِ النَّبِيِّ وَلَا تَجْهَرُوا لَهُ بِالْقَوْلِ كَجَهْرِ بَعْضِكُمْ لِبَعْضٍ أَن تَحْبَطَ أَعْمَالُكُمْ وَأَنتُمْ لَا تَشْعُرُونَ﴿٢﴾    فَكَانَ عُمَرُ بْنُ الْخَطَّابِ بَعْدَ ذَلِكَ إِذَا تَكَلَّمَ عِنْدَ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم لَمْ يُسْمِعْ كَلاَمَهُ حَتَّى يَسْتَفْهِمَهُ ‏.‏ قَالَ وَمَا ذَكَرَ ابْنُ الزُّبَيْرِ جَدَّهُ يَعْنِي أَبَا بَكْرٍ ‏.‏ قَالَ أَبُو عِيسَى هَذَا حَدِيثٌ حَسَنٌ غَرِيبٌ ‏.‏ وَقَدْ رَوَى بَعْضُهُمْ عَنِ ابْنِ أَبِي مُلَيْكَةَ مُرْسَلٌ وَلَمْ يَذْكُرْ فِيهِ عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ الزُّبَيْرِ ‏.‏

‘Abdullaah bin Zubayr (رضي الله عنه) amehadithia kwamba: “Al-Aqra’ bin Haabis  alimjia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) basi Abuu Bakr akasema: ‘Ee Rasuli wa Allaah, mteuwe awaongoze watu wake.’ ‘Umar naye akasema: ‘Usimteuwe ee Rasuli wa Allaah.”  Sauti zao zikapaza kisha Abuu Bakr akamwambia ‘Umar: ‘Hukukusudia isipokuwa unipinge.’ Naye ‘Umar akasema: ‘Sikukusudia kukupinga.’ Hapo ikateremka Aayah hii:

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَرْفَعُوا أَصْوَاتَكُمْ فَوْقَ صَوْتِ النَّبِيِّ وَلَا تَجْهَرُوا لَهُ بِالْقَوْلِ كَجَهْرِ بَعْضِكُمْ لِبَعْضٍ أَن تَحْبَطَ أَعْمَالُكُمْ وَأَنتُمْ لَا تَشْعُرُونَ﴿٢﴾

Enyi walioamini! Msipandishe sauti zenu juu ya sauti ya Nabiy, na wala msiseme naye kwa sauti ya juu, kama mnavyosemezana wenyewe kwa wenyewe kwa sauti za juu; zisije zikaporomoka ‘amali zenu nanyi hamhisi.

 

‘Umar akawa anapoongea mbele ya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)   sauti yake haikuwa inasikika mpaka ikawa  hakuwa anamfahamu.  Akasema (Mmoja wa msimuliaji): ”Ibn Zubayr hakumtaja babu yake yaani Abuu Bakr.”  [At-Tirmidhiy ameisaihihisha Al-Albaaniy (3266)]

 

Asbaabun-Nuzuwl

 

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

 

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

049-Al-Hujuraat: 1

 

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تُقَدِّمُوا بَيْنَ يَدَيِ اللَّـهِ وَرَسُولِهِ ۖ وَاتَّقُوا اللَّـهَ ۚ إِنَّ اللَّـهَ سَمِيعٌ عَلِيمٌ﴿١﴾

Enyi walioamini! Msikadimishe (lolote) mbele ya Allaah na Rasuli Wake. Na mcheni Allaah; hakika Allaah ni Mwenye kusikia yote, Mjuzi wa yote. [Al-Hujuraat: 1]

 

 

Sababun-Nuzuwl: 

 

عن عبد الله بن زبير رضي الله عنه: قَدِمَ رَكْبٌ مِنْ بَنِي تَمِيمٍ عَلَى النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ أَبُو بَكْرٍ: أَمِّرِ الْقَعْقَاعَ بْنَ مَعْبَدٍ‏.‏ وَقَالَ عُمَرُ: بَلْ أَمِّرِ الأَقْرَعَ بْنَ حَابِسٍ‏.‏ فَقَالَ أَبُو بَكْرٍ: مَا أَرَدْتَ إِلَى ـ أَوْ إِلاَّ ـ خِلاَفِي‏.‏ فَقَالَ عُمَرُ: مَا أَرَدْتُ خِلاَفَكَ‏.‏ فَتَمَارَيَا حَتَّى ارْتَفَعَتْ أَصْوَاتُهُمَا، فَنَزَلَ فِي ذَلِكَ: ((‏يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لاَ تُقَدِّمُوا بَيْنَ يَدَىِ اللَّهِ وَرَسُولِهِ‏))‏ حَتَّى انْقَضَتِ الآيَةُ‏.‏

Kundi la watu katika Bani Tamiyim walimjia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) (kumtaka awateulie gavana wao). Abuu Bakr akasema: “Mteue Al-Qa’qaa’ bin Ma’bad.”  ‘Umar akasema: “Mteue Al-Aqra’ bin Haabis.” Hapo Abuu Bakr akamwambia (‘Umar). “Hukukusudia isipokuwa kunipinga mimi.” ‘Umar akasema: “Sikukusudia kukupinga.” Basi wawili hao wakabishana hadi sauti zao zikapanda juu, ndipo ikateremka:

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تُقَدِّمُوا بَيْنَ يَدَيِ اللَّـهِ وَرَسُولِهِ ۖ وَاتَّقُوا اللَّـهَ ۚ إِنَّ اللَّـهَ سَمِيعٌ عَلِيمٌ﴿١﴾

 

[Al-Bukhaariy]

 

 

Asbaabun-Nuzuwl

 

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

 

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

054-Al-Qamar Aayah 47-49

 

 

Kauli za Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّ الْمُجْرِمِينَ فِي ضَلَالٍ وَسُعُرٍ ﴿٤٧﴾

Hakika wahalifu wamo katika upotofu na wazimu.

 

يَوْمَ يُسْحَبُونَ فِي النَّارِ عَلَىٰ وُجُوهِهِمْ ذُوقُوا مَسَّ سَقَرَ ﴿٤٨﴾

Siku watakayoburutwa motoni kifudifudi: Onjeni mguso wa moto mkali mno.

 

إِنَّا كُلَّ شَيْءٍ خَلَقْنَاهُ بِقَدَرٍ ﴿٤٩﴾

Hakika sisi Tumekiumba kila kitu kwa Qadar (majaaliwa). [Al-Qamar: 49]

 

 

Sababun-Nuzuwl:

 

 

 

كان مُشركو قريشٍ عندَ رسولِ اللهِ صلَّى اللهُ عليه وسلَّم يُخالِفونَه في القدَرِ فنزَلتْ هذه الآيةُ: ((إِنَّ الْمُجْرِمِينَ فِي ضَلَالٍ وَسُعُرٍ * يَوْمَ يُسْحَبُونَ فِي النَّارِ عَلَى وُجُوهِهِمْ ذُوقُوا مَسَّ سَقَرَ * إِنَّا كُلَّ شَيْءٍ خَلَقْنَاهُ بِقَدَرٍ))

Abuu Hurayrah (رضي الله عنه) amehadithia kuwa Washirikina wa ki-Quraysh walikuwa wakimpinga Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) kuhusu Al-Qadar. Zikateremka Aayah hizi:

 

إِنَّ الْمُجْرِمِينَ فِي ضَلَالٍ وَسُعُرٍ ﴿٤٧﴾

Hakika wahalifu wamo katika upotofu na wazimu.

 

يَوْمَ يُسْحَبُونَ فِي النَّارِ عَلَىٰ وُجُوهِهِمْ ذُوقُوا مَسَّ سَقَرَ ﴿٤٨﴾

Siku watakayoburutwa motoni kifudifudi: Onjeni mguso wa moto mkali mno.

 

إِنَّا كُلَّ شَيْءٍ خَلَقْنَاهُ بِقَدَرٍ ﴿٤٩﴾

Hakika sisi Tumekiumba kila kitu kwa Qadar (majaaliwa). [Al-Qamar: 49]

 

[Ibn Hibbaan na ameisahihisha Al-Albaaniy katika Swahiyh Ibn Hibbaan (6139), na As-Silsilah Asw-Swahiyhah (4/53)]

 

 

Asbaabun-Nuzuwl

 

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

 

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

054-Al-Qamar Aayah 1 -2

 

 

Kauli za Allaah (سبحانه وتعالى):

اقْتَرَبَتِ السَّاعَةُ وَانشَقَّ الْقَمَرُ ﴿١﴾

Saa imekaribia na mwezi umepasuka. 

 

وَإِن يَرَوْا آيَةً يُعْرِضُوا وَيَقُولُوا سِحْرٌ مُّسْتَمِرٌّ ﴿٢﴾

Na wanapoona Aayah (ishara, dalili) hukengeuka na husema: Sihiri inayoendelea [Al-Qamar: 1-2]

 

Sababun-Nuzuwl:

 

عَنْ أَنَسٍ، قَالَ سَأَلَ أَهْلُ مَكَّةَ النَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم آيَةً فَانْشَقَّ الْقَمَرُ بِمَكَّةَ مَرَّتَيْنِ فَنَزَلَت: ((‏اقتَرَبَتِ السَّاعَةُ وَانْشَقَّ الْقَمَرُ))  إِلَى قَوْلِهِ ‏:‏ ‏ ((‏سحْرٌ مُسْتَمِرٌّ))  يَقُولُ ذَاهِبٌ ‏.‏ قَالَ أَبُو عِيسَى هَذَا حَدِيثٌ حَسَنٌ صَحِيحٌ ‏.

Imepokelewa kutoka kwa Anas (رضي الله عنه) kwamba watu wa Makkah walimuomba  Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) awaletee Aayah (Ishara, muujiza), basi mwezi ukapasuka Makkah mara mbili (Yaani sehemu mbili), kisha ikateremka:

اقْتَرَبَتِ السَّاعَةُ وَانشَقَّ الْقَمَرُ ﴿١﴾

Saa imekaribia na mwezi umepasuka

 

Mpaka kauli Yake:

  سِحْرٌ مُّسْتَمِرٌّ  

Sihiri inayoendelea [Al-Qamar: 1-2]

 

Yaani Sihiri (Uchawi) inayootoweka.

[Amesema Abuu ‘Iysaa (at-Tirmidhiy) Hii ni Hadiyth Hasan Swahiyh]

 

Pia,

 عن ابن عباس رضي الله عنهما قال كسف القمر على عهد رسول الله صلى الله عليه وعلى آله وسلم فقالوا: سحر القمر، فنزلت ((اقْتَرَبَتِ السَّاعَةُ وَانْشَقَّ الْقَمَرُ، وَإِنْ يَرَوْا آيَةً يُعْرِضُوا وَيَقُولُوا سِحْرٌ مُسْتَمِرٌّ))  

Imepokelewa kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) kwamba mwezi ulipatwa katika zama za Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) basi (makafiri) wakasema: “Sihiri (uchawi) unaoendelea.”  Ikateremka:

اقْتَرَبَتِ السَّاعَةُ وَانشَقَّ الْقَمَرُ ﴿١﴾

Saa imekaribia na mwezi umepasuka. 

وَإِن يَرَوْا آيَةً يُعْرِضُوا وَيَقُولُوا سِحْرٌ مُّسْتَمِرٌّ ﴿٢﴾

Na wanapoona Aayah (ishara, dalili) hukengeuka na husema: Sihiri inayoendelea [Al-Qamar: 1-2]

 

[Atw-Twabaraniy na Al-Haafidhw Ibn Kathiyr amesema katika Al-Bidaayah Wan-Nihaayah:  Isnaad yake ni Jayyid]

 

Asbaabun-Nuzuwl

 

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

056-Al-Waaqi’ah: Aayah: 75-82

 

 

Kauli za Allaah (سبحانه وتعالى):

 

فَلَا أُقْسِمُ بِمَوَاقِعِ النُّجُومِ ﴿٧٥﴾

Basi Naapa kwa maangukio ya nyota.

 

وَإِنَّهُ لَقَسَمٌ لَّوْ تَعْلَمُونَ عَظِيمٌ ﴿٧٦﴾

Na hakika hicho ni kiapo adhimu lau mngelijua.

 

إِنَّهُ لَقُرْآنٌ كَرِيمٌ ﴿٧٧﴾

Hakika hii bila shaka ni Qur-aan tukufu.

 

فِي كِتَابٍ مَّكْنُونٍ ﴿٧٨﴾

Katika Kitabu kilichohifadhiwa.

 

لَّا يَمَسُّهُ إِلَّا الْمُطَهَّرُونَ ﴿٧٩﴾

Haigusi isipokuwa waliotakaswa kabisa.

 

تَنزِيلٌ مِّن رَّبِّ الْعَالَمِينَ ﴿٨٠﴾

Ni uteremsho kutoka kwa Rabb wa walimwengu.

 

أَفَبِهَـٰذَا الْحَدِيثِ أَنتُم مُّدْهِنُونَ ﴿٨١﴾

Je, kwa maneno haya nyinyi ni wenye kuikanusha na kuibeza?

 

وَتَجْعَلُونَ رِزْقَكُمْ أَنَّكُمْ تُكَذِّبُونَ ﴿٨٢﴾

Na mnafanya badala (shukurani za) riziki zenu kuwa nyinyi mnakadhibisha.

 

وَتَجْعَلُونَ رِزْقَكُمْ أَنَّكُمْ تُكَذِّبُونَ ﴿٨٢﴾

Na mnafanya badala (shukurani za) riziki zenu kuwa nyinyi mnakadhibisha. [Al-Waaqi’ah: 75-82]

 

Sababun-Nuzuwl:

 

 

عن ابْنِ عَبَّاسٍ، قَالَ مُطِرَ النَّاسُ عَلَى عَهْدِ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم ‏"‏ أَصْبَحَ مِنَ النَّاسِ شَاكِرٌ وَمِنْهُمْ كَافِرٌ قَالُوا هَذِهِ رَحْمَةُ اللَّهِ ‏.‏ وَقَالَ بَعْضُهُمْ لَقَدْ صَدَقَ نَوْءُ كَذَا وَكَذَا ‏"‏ ‏.‏ قَالَ فَنَزَلَتْ هَذِهِ الآيَةُ: ((‏فَلاَ أُقْسِمُ بِمَوَاقِعِ النُّجُومِ‏))‏ حَتَّى بَلَغَ ‏ ((وَتَجْعَلُونَ رِزْقَكُمْ أَنَّكُمْ تُكَذِّبُونَ‏))

Imepokelewa kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) kwamba kulitokea mvua zama za Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) ambapo Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alisema: “Baadhi ya watu wamepambukiwa asubuhi wakiwa wenye kushukuru, na wengineo wenye kukufuru (kukosa shukurani kwa Allaah).” Walioshukuru walisema: “Hii ni Rahmah ya Allaah.” Na wale waliokufuru walisema: “Nyota kadhaa na kadhaa zimesadikisha.” Hapo ikateremka Aayah hii:

فَلَا أُقْسِمُ بِمَوَاقِعِ النُّجُومِ ﴿٧٥﴾

Basi Naapa kwa maangukio ya nyota.

 

Mpaka kufikia:

 

وَتَجْعَلُونَ رِزْقَكُمْ أَنَّكُمْ تُكَذِّبُونَ ﴿٨٢﴾

Na mnafanya badala (shukurani za) riziki zenu kuwa nyinyi mnakadhibisha. [Al-Waaqi’ah: 75-82]

 

[Muslim Kitaabul-Iymaan, Mlango wa Kubainisha Kufru Kwa Anayesema Tumenyeshewa Mvua Kutokana Na Nyota]

 

Asbaabun-Nuzuwl

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

058-Suwrah Al-Mujaadalah: Aayah 14

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

أَلَمْ تَرَ إِلَى الَّذِينَ تَوَلَّوْا قَوْمًا غَضِبَ اللَّـهُ عَلَيْهِم مَّا هُم مِّنكُمْ وَلَا مِنْهُمْ وَيَحْلِفُونَ عَلَى الْكَذِبِ وَهُمْ يَعْلَمُونَ﴿١٤﴾

14. Je, hukuona wale waliofanya urafiki na watu ambao Allaah Ameghadhibika nao, wao si miongoni mwenu na wala si miongoni mwao na wanaapia uongo nao wanajua.

 

أَعَدَّ اللَّـهُ لَهُمْ عَذَابًا شَدِيدًا ۖ إِنَّهُمْ سَاءَ مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ﴿١٥﴾

15. Allaah Amewaandalia adhabu kali, hakika uovu ulioje waliyokuwa wakiyatenda.

 

Sababun-Nuzuwl: 

  ثنا محمد بن جعفر ثنا شعبة عن سماك بن حرب عن سعيد بن جبير عن ابن عباس قال: قال رسول الله صلى الله عليه وعلى آله وسلم: "يدخل عليكم رجل ينظر بعين شيطان أو بعيني شيطان". قال فدخل رجل أزرق فقال: يا محمد علام سببتني أو شتمتني أو نحو هذا قال وجعل يحلف، قال: ونزلت هذه الآية في المجادلة ((وَيَحْلِفُونَ عَلَى الْكَذِبِ وَهُمْ يَعْلَمُونَ)) والآية الأخرى.

Ametuhadithia Muhammad bin Ja’far, ametuhadithia Shu’bah toka kwa Simaak bin Harb toka kwa Sa’iyd bin Jubayr toka kwa Ibn ‘Abbaas amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  amesema: ((Atawajieni mtu anayeangalia kwa jicho la shaytwaan au macho mawili ya shaytwaan)). Akasema: Akaingia mtu wa kibuluu akasema: Ee Muhammad! Umenitukania nini au umenitusia nini, au mfano wa hivi. Akasema: Akaendelea kuapa, na ikashuka Aayah hii katika Al-Mujaadalah:

 

أَلَمْ تَرَ إِلَى الَّذِينَ تَوَلَّوْا قَوْمًا غَضِبَ اللَّـهُ عَلَيْهِم مَّا هُم مِّنكُمْ وَلَا مِنْهُمْ وَيَحْلِفُونَ عَلَى الْكَذِبِ وَهُمْ يَعْلَمُونَ﴿١٤﴾

Je, hukuona wale waliofanya urafiki na watu ambao Allaah Ameghadhibika nao, wao si miongoni mwenu na wala si miongoni mwao na wanaapia uongo nao wanajua.

أَعَدَّ اللَّـهُ لَهُمْ عَذَابًا شَدِيدًا ۖ إِنَّهُمْ سَاءَ مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ﴿١٥﴾

Allaah Amewaandalia adhabu kali, hakika uovu ulioje waliyokuwa wakiyatenda.

 

Na pia,

 

Bonyeza Endelea...

 

Asbaabun-Nuzuwl

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

058-Suwrah Al-Mujaadalah: Aayah 8

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

  أَلَمْ تَرَ إِلَى الَّذِينَ نُهُوا عَنِ النَّجْوَىٰ ثُمَّ يَعُودُونَ لِمَا نُهُوا عَنْهُ وَيَتَنَاجَوْنَ بِالْإِثْمِ وَالْعُدْوَانِ وَمَعْصِيَتِ الرَّسُولِ وَإِذَا جَاءُوكَ حَيَّوْكَ بِمَا لَمْ يُحَيِّكَ بِهِ اللَّـهُ وَيَقُولُونَ فِي أَنفُسِهِمْ لَوْلَا يُعَذِّبُنَا اللَّـهُ بِمَا نَقُولُ ۚ حَسْبُهُمْ جَهَنَّمُ يَصْلَوْنَهَا ۖ فَبِئْسَ الْمَصِيرُ﴿٨﴾

8. Je, huwaoni wale waliokatazwa kunong’ona, kisha wanarudia yale waliyokatazwa nayo, na wananong’onezana kuhusu dhambi na uadui na kumuasi Rasuli na wanapokujia wanakuamkia kwa maamkizi Asiyokuamkia kwayo Allaah; na wanasema katika nafsi zao: Mbona Allaah Hatuadhibu kwa yale tunayoyasema? Jahannam inawatosheleza, wataingia waungue, basi ubaya ulioje mahali pa kuishia.

 

Sababun-Nuzuwl: 

  حدثنا عبد الصمد ثنا حماد عن عطاء بن السائب عن أبيه عن عبد الله بن عمرو أن اليهود كانوا يقولون لرسول الله صلى الله عليه وعلى آله وسلم: سام عليك، ثم يقولون في أنفسهم، لولا يعذبنا الله بما نقول، فنزلت هذه الآية: ((وَإِذَا جَاءُوكَ حَيَّوْكَ بِمَا لَمْ يُحَيِّكَ بِهِ اللَّهُ)) إلى آخر الآية.   .

Ametuhadithia ‘Abdu As Swamad, ametuhadithia Hammaad toka kwa ‘Atwaa bin As Saaib toka kwa baba yake toka kwa ‘Abdillaah bin ‘Amri ya kuwa Mayahudi walikuwa wakimwambia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم): “Saam ‘alayka” (Mauti yawe juu yako), kisha wanajiambia wenyewe: “Kwa nini basi Allaah hatuadhibu kwa haya tuyasemayo?’ Hapo ikateremka Aayah hii:

 

Bonyeza Endelea...