Asbaabun-Nuzuwl

Asbaabun-Nuzuwl

Asbaabun-Nuzuwl

 

 

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

(Sababu Za Kuteremshwa Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

033-Asbaabun-Nuzuwl Al-Ahzaab Aayah 23

 

 

Kauli Yake Allaah (سبحانه وتعالى)

 

مِّنَ الْمُؤْمِنِينَ رِجَالٌ صَدَقُوا مَا عَاهَدُوا اللَّـهَ عَلَيْهِ ۖ فَمِنْهُم مَّن قَضَىٰ نَحْبَهُ وَمِنْهُم مَّن يَنتَظِرُ ۖ وَمَا بَدَّلُوا تَبْدِيلًا ﴿٢٣﴾

Miongoni mwa Waumini, wapo wanaume waliokuwa wakweli kutimiza waliyoahidiana na Allaah; basi miongoni mwao waliotimiza nadhiri yao; (wamekufa shahidi), na miongoni mwao wanaongojea na hawakubadilisha (ahadi) hata kidogo.  [Al-Ahzaab (33:23)]

 

Sababun-Nuzuwl: 

 

حَدَّثَنَا مُحَمَّدُ بْنُ سَعِيدٍ الْخُزَاعِيُّ، حَدَّثَنَا عَبْدُ الأَعْلَى، عَنْ حُمَيْدٍ، قَالَ سَأَلْتُ أَنَسًا‏.‏ حَدَّثَنَا عَمْرُو بْنُ زُرَارَةَ، حَدَّثَنَا زِيَادٌ، قَالَ حَدَّثَنِي حُمَيْدٌ الطَّوِيلُ، عَنْ أَنَسٍ ـ رضى الله عنه ـ قَالَ غَابَ عَمِّي أَنَسُ بْنُ النَّضْرِ عَنْ قِتَالِ بَدْرٍ فَقَالَ يَا رَسُولَ اللَّهِ، غِبْتُ عَنْ أَوَّلِ قِتَالٍ قَاتَلْتَ الْمُشْرِكِينَ، لَئِنِ اللَّهُ أَشْهَدَنِي قِتَالَ الْمُشْرِكِينَ لَيَرَيَنَّ اللَّهُ مَا أَصْنَعُ، فَلَمَّا كَانَ يَوْمُ أُحُدٍ وَانْكَشَفَ الْمُسْلِمُونَ قَالَ ‏"‏ اللَّهُمَّ إِنِّي أَعْتَذِرُ إِلَيْكَ مِمَّا صَنَعَ هَؤُلاَءِ ـ يَعْنِي أَصْحَابَهُ ـ وَأَبْرَأُ إِلَيْكَ مِمَّا صَنَعَ هَؤُلاَءِ ‏"‏ ـ يَعْنِي الْمُشْرِكِينَ ـ ثُمَّ تَقَدَّمَ، فَاسْتَقْبَلَهُ سَعْدُ بْنُ مُعَاذٍ، فَقَالَ يَا سَعْدُ بْنَ مُعَاذٍ، الْجَنَّةَ، وَرَبِّ النَّضْرِ إِنِّي أَجِدُ رِيحَهَا مِنْ دُونِ أُحُدٍ‏.‏ قَالَ سَعْدٌ فَمَا اسْتَطَعْتُ يَا رَسُولَ اللَّهِ مَا صَنَعَ‏.‏ قَالَ أَنَسٌ فَوَجَدْنَا بِهِ بِضْعًا وَثَمَانِينَ ضَرْبَةً بِالسَّيْفِ أَوْ طَعْنَةً بِرُمْحٍ أَوْ رَمْيَةً بِسَهْمٍ، وَوَجَدْنَاهُ قَدْ قُتِلَ وَقَدْ مَثَّلَ بِهِ الْمُشْرِكُونَ، فَمَا عَرَفَهُ أَحَدٌ إِلاَّ أُخْتُهُ بِبَنَانِهِ‏.‏ قَالَ أَنَسٌ كُنَّا نَرَى أَوْ نَظُنُّ أَنَّ هَذِهِ الآيَةَ نَزَلَتْ فِيهِ وَفِي أَشْبَاهِهِ ‏((‏مِنَ الْمُؤْمِنِينَ رِجَالٌ صَدَقُوا مَا عَاهَدُوا اللَّهَ عَلَيْهِ‏))‏ إِلَى آخِرِ الآيَةِ‏.‏

 

Ametuhadithia Muhammaad bin Sa’iyd Al-Khuzaaiy, ametuhadithia ‘Abdul-A-‘alaa toka kwa Humayd, amesema, nilimuuliza Anas, amesema, na amenihadithia ‘Amri bin Zaraarah, ametuhadithia Ziyaad amesema, amenihadithia Humayd At-Twawiyl toka kwa Anas (Radhwiya Allaah ‘anhu) amesema: Ami yangu Anas bin An-Nadhwr alikosekana kwenye Vita vya Badr, akamwambia Rasuli: Ee Rasuli wa Allaah! Nilikosekana katika vita vya kwanza ulivyopambana na washirikina. Na ikiwa Allaah Ataniwezesha kushiriki vita vya kupambana na washirikina, basi hakika Allaah Ataona vipi nitakavyopambana kishujaa. Ilipokuwa Siku ya (Vita vya) Uhud, na Waislamu wakalemewa na kukimbia alisema: Ee Allaah! Naomba udhuru kwa waliyoyafanya hawa – yaani wenzake Swahaba - (walenga mishale ambao walikaidi agizo la Rasuli kwao la kutoondoka pale alipowapanga juu ya mlima, wakateremka chini kukusanya ngawira), na najitakasa na kujivua Kwako kutokana na waliyoyafanya hawa – yaani washirikina- (ya kuwapiga vita Waislamu na kumuudhi Rasuli wa Allaah Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Kisha akasonga mbele (na upanga wake), na akakutana na Sa’ad bin Mu’aadh (akikimbia vita). Akamwambia: Ee Sa’ad bin Mu’aadh (mimi naihisi) Jannah (Pepo). Naapa kwa Rabb wa An-Nadhwr, hakika mimi nainusa harufu yake mbele ya Jabal Uhud. Sa’ad akasema: Sikuweza ee Rasuli wa Allaah kufanya aliyoyafanya (ya kusonga mbele na kupambana kishujaa na washirikina). Anas anasema: Tukamkuta ameuawa (kishahidi) na ana zaidi ya majeraha themanini ya kati ya kupigwa panga, kuchomwa mkuki na kulengwa mishale, na washirikina wamemkata baadhi ya viungo vyake na kuitweza maiti yake.  Hakuna aliyeweza kumtambua isipokuwa dada yake kwa ncha za vidole vyake. Anas amesema: Tulikuwa tunaona au tunadhani kuwa Aayah hii imeteremka kumzungumzia yeye na wenye msimamo na ushujaa kama wake:

مِّنَ الْمُؤْمِنِينَ رِجَالٌ صَدَقُوا مَا عَاهَدُوا اللَّـهَ عَلَيْهِ 

Miongoni mwa Waumini, wapo wanaume waliokuwa wakweli kutimiza waliyoahidiana na Allaah… mpaka mwisho wa Aayah” [Al-Bukhaariy katika Mujallad wa Sita ukurasa wa 361]

 

 

Asbaabun-Nuzuwl

 

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

(Sababu Za Kuteremshwa Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

033-Asbaabun-Nuzuwl Al-Ahzaab Aayah 05

 

 

Kauli Yake Allaah (سبحانه وتعالى):

 

ادْعُوهُمْ لِآبَائِهِمْ هُوَ أَقْسَطُ عِندَ اللَّـهِ ۚ فَإِن لَّمْ تَعْلَمُوا آبَاءَهُمْ فَإِخْوَانُكُمْ فِي الدِّينِ وَمَوَالِيكُمْ ۚ وَلَيْسَ عَلَيْكُمْ جُنَاحٌ فِيمَا أَخْطَأْتُم بِهِ وَلَـٰكِن مَّا تَعَمَّدَتْ قُلُوبُكُمْ ۚ وَكَانَ اللَّـهُ غَفُورًا رَّحِيمًا ﴿٥﴾

Waiteni kwa (majina ya) baba zao, huo ndio uadilifu zaidi mbele ya Allaah. Na ikiwa hamuwajui baba zao, basi ni ndugu zenu katika Dini, na walio katika ulinzi wenu, na wala hakuna dhambi juu yenu katika yale mliyoyakosea, lakini isipokuwa katika yale yaliyoyakusudia nyoyo zenu; na Allaah daima ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu. [Al-Ahzaab 33: 5]

 

Sababun-Nuzuwl: 

 

حَدَّثَنَا مُعَلَّى بْنُ أَسَدٍ، حَدَّثَنَا عَبْدُ الْعَزِيزِ بْنُ الْمُخْتَارِ، حَدَّثَنَا مُوسَى بْنُ عُقْبَةَ، قَالَ حَدَّثَنِي سَالِمٌ، عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عُمَرَ ـ رضى الله عنهما ـ أَنَّ زَيْدَ بْنَ حَارِثَةَ، مَوْلَى رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم مَا كُنَّا نَدْعُوهُ إِلاَّ زَيْدَ ابْنَ مُحَمَّدٍ حَتَّى نَزَلَ الْقُرْآنُ ‏((‏ادْعُوهُمْ لآبَائِهِمْ هُوَ أَقْسَطُ عِنْدَ اللَّهِ))‏

Ametuhadithia Ma’-alaa bin Asad, ametuhadithia ‘Abdul-‘Aziyz bin Al-Mukhtaar, ametuhadithia Muwsaa bin ‘Uqbah, amenihadithia Saalim toka kwa ‘Abdullaah bin ‘Umar (Radhwiya Allaah ‘anhumaa) kwamba Zayd bin Haaritha mwachwa huru wa Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihii wa sallam) hatukuwa tukimuita isipokuwa Zayd bin Muhammad mpaka Allaah [Ta’aalaa] Alipoteremsha:

ادْعُوهُمْ لِآبَائِهِمْ هُوَ أَقْسَطُ عِندَ اللَّـهِ 

Waiteni kwa (majina ya) baba zao, huo ndio uadilifu zaidi mbele ya Allaah.

[Al-Ahzaab (33:5) - Al-Bukhaariy katika Mujallad wa Kumi ukurasa wa 136]

 

Na pia...

 

 

Asbaabun-Nuzuwl

 

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

(Sababu Za Kuteremshwa Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

032-Asbaabun-Nuzuwl: As-Sajdah Aayah 16

 

 

Kauli Yake Allaah (سبحانه وتعالى):

 

تَتَجَافَىٰ جُنُوبُهُمْ عَنِ الْمَضَاجِعِ يَدْعُونَ رَبَّهُمْ خَوْفًا وَطَمَعًا وَمِمَّا رَزَقْنَاهُمْ يُنفِقُونَ ﴿١٦﴾ فَلَا تَعْلَمُ نَفْسٌ مَّا أُخْفِيَ لَهُم مِّن قُرَّةِ أَعْيُنٍ جَزَاءً بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿١٧﴾

Mbavu zao zinatengana na vitanda, wanamuomba Rabb wao kwa khofu na matumaini, na katika yale Tuliyowaruzuku wanatoa. Basi nafsi yoyote haijui yaliyofichiwa katika yanayoburudisha macho. Ni jazaa kwa yale waliyokuwa wakiyatenda. [As-Sajdah (32:16)]

 

 

Sababun-Nuzuwl:

 

حَدَّثَنَا عَبْدُ اللَّهِ بْنُ أَبِي زِيَادٍ، حَدَّثَنَا عَبْدُ الْعَزِيزِ بْنُ عَبْدِ اللَّهِ الأُوَيْسِيُّ، عَنْ سُلَيْمَانَ بْنِ بِلاَلٍ، عَنْ يَحْيَى بْنِ سَعِيدٍ، عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ، أَنَّ هَذِهِ الآيَةَ ‏:‏ ((تتَجَافَى، جُنُوبُهُمْ عَنِ الْمَضَاجِعِ))نَزَلَتْ فِي انْتِظَارِ هَذِهِ الصَّلاَةِ الَّتِي تُدْعَى الْعَتَمَةَ ‏.‏ قَالَ أَبُو عِيسَى هَذَا حَدِيثٌ حَسَنٌ صَحِيحٌ غَرِيبٌ لاَ نَعْرِفُهُ إِلاَّ مِنْ هَذَا الْوَجْهِ

Ametuhadithia ‘Abdullaah bin Abiy Ziyaad, ametuhadithia ‘Abdul-‘Aziyz bin ‘Abdillaah Al-Uwaysiy toka kwa Sulaymaan bin Bilaal toka kwa Yahyaa bin Sa’iyd toka kwa Anas bin Maalik kuhusiana na Aayaah hii:

تَتَجَافَىٰ جُنُوبُهُمْ عَنِ الْمَضَاجِعِ

Mbavu zao zinatengana na vitanda

 

Ni kuwa iliteremka kuzungumzia kuisubiri Swalaah iitwayo Al-‘Atamah. [At-Tirmidhiy katika Mujallad wa Nne ukurasa wa 161.  Hii ni Hadiyth Hasan Swahiyh, hatuijui ila kwa picha hii. Ibn Jariyr ameikhariji katika Mujallad wa Kumi na Mbili ukurasa wa 100. Na Al-Haafidh Ibn Kathiyr amesema katika Tafsiyr yake kuwa Sanad yake ni Jayyid].

 

 

Asbaabun-Nuzuwl

 

Sababu Za Kuteremshwa

(Baadhi Ya Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

Suwrah Al-Masad

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

 

 111-Suwratul-Masad:

 

تَبَّتْ يَدَا أَبِي لَهَبٍ وَتَبَّ ﴿١﴾

1. Imeteketea mikono miwili ya Abuu Lahab na ameteketea.

 

مَا أَغْنَىٰ عَنْهُ مَالُهُ وَمَا كَسَبَ ﴿٢﴾

2. Haikumfaa mali yake na yale aliyoyachuma.

 

سَيَصْلَىٰ نَارًا ذَاتَ لَهَبٍ ﴿٣﴾

3. Ataingia na kuungua moto wenye mwako.

 

وَامْرَأَتُهُ حَمَّالَةَ الْحَطَبِ ﴿٤﴾

4. Na mke wake mbebaji kuni za moto.

 

فِي جِيدِهَا حَبْلٌ مِّن مَّسَدٍ ﴿٥﴾

5. Katika shingo yake kamba ya mtende iliyosokotwa madhubuti.

 

 

عَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ ـ رضى الله عنهما ـ قَالَ: لَمَّا نَزَلَتْ: ((‏وَأَنْذِرْ عَشِيرَتَكَ الأَقْرَبِينَ)) صَعِدَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم عَلَى الصَّفَا فَجَعَلَ يُنَادِي:  ((يَا بَنِي فِهْرٍ، يَا بَنِي عَدِيٍّ))‏‏.‏ لِبُطُونِ قُرَيْشٍ حَتَّى اجْتَمَعُوا، فَجَعَلَ الرَّجُلُ إِذَا لَمْ يَسْتَطِعْ أَنْ يَخْرُجَ أَرْسَلَ رَسُولاً لِيَنْظُرَ مَا هُوَ، فَجَاءَ أَبُو لَهَبٍ وَقُرَيْشٌ فَقَالَ: ((أَرَأَيْتَكُمْ لَوْ أَخْبَرْتُكُمْ أَنَّ خَيْلاً بِالْوَادِي تُرِيدُ أَنْ تُغِيرَ عَلَيْكُمْ، أَكُنْتُمْ مُصَدِّقِيَّ))‏‏.‏ قَالُوا نَعَمْ، مَا جَرَّبْنَا عَلَيْكَ إِلاَّ صِدْقًا‏.‏ قَالَ: ((فَإِنِّي نَذِيرٌ لَكُمْ بَيْنَ يَدَىْ عَذَابٍ شَدِيدٍ)).‏ فَقَالَ أَبُو لَهَبٍ: "تَبًّا لَكَ سَائِرَ الْيَوْمِ، أَلِهَذَا جَمَعْتَنَا؟" فَنَزَلَتْ:  ‏((‏تَبَّتْ يَدَا أَبِي لَهَبٍ وَتَبَّ * مَا أَغْنَى عَنْهُ مَالُهُ وَمَا كَسَبَ))

 

Kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) amesema, Pindi ilipoteremka: “Na onya (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم) jamaa zako wa karibu”. Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alipanda juu ya mlima wa Asw-Swafaa akawa anaita na kulingania: “Enyi Baniy ‘Adiyy!” Kwa makabila na matumbo ya ki-Quraysh hadi yalipokusanyika na ikawa mtu siku hiyo ambayo hakuweza kutoka humtuma mtu ambaye atamuwakilisha ili ajue kuna nini. Abuu Lahab pamoja na ma-Quraysh wengine walifika na hapo Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: “Lau nikiwajulisha kuwa kuna msafara kwenye bonde unakuja kuwashambulia; je, mtanisadiki?” Wakasema: “Ndio, hatukuwahi kujaribu kutoka kwako isipokuwa ni kweli tupu!” Hapo Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: “Hakika mimi ni mwonyaji kwenu, kabla ya kufikia adhabu kali)).  Abuu Lahab akasema:  “Ole wako siku nzima ya leo, ni kwa hili ndilo ulilotukusanyia?” Baada ya hapo ikateremka: “Imeteketea mikono miwili ya Abuu Lahab na ameteketea. Haikumfaa mali yake na yale aliyoyachuma…” [Al-Masad: 111] [Al-Bukhaariy, Kitaab At-Tafsiyr]

 

Pia,

 

عَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ ـ رضى الله عنهما أَنَّ النَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم خَرَجَ إِلَى الْبَطْحَاءِ فَصَعِدَ إِلَى الْجَبَلِ فَنَادَى :((يَا صَبَاحَاهْ))‏ فَاجْتَمَعَتْ إِلَيْهِ قُرَيْشٌ قَالُوا: مَا لَكَ؟  قَالَ: (( أَرَأَيْتُمْ لَوْ أَخْبَرْتُكُمْ أَنَّ الْعَدُوَّ يُصَبِّحُكُمْ أَوْ يُمَسِّيكُمْ أَمَا كُنْتُمْ تُصَدِّقُونِي)) ‏  قَالُوا: "بَلَى‏!" ‏ قَالَ: (( فَإِنِّي نَذِيرٌ لَكُمْ بَيْنَ يَدَىْ عَذَابٍ شَدِيدٍ)) ‏ فَقَالَ أَبُو لَهَبٍ: "تَبًّا لَكَ أَلِهَذَا جَمَعْتَنَا فَأَنْزَلَ اللَّهُ: ((‏تَبَّتْ يَدَا أَبِي لَهَبٍ‏...)))

Amepokea Al-Bukhaariy kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما)  kuwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alitoka kwenda Al-Batw-haa akapanda juu ya jabali akaita kwa kusema: ((Ee, kumekucha!)) Wakakusanyika kwake Ma-Quraysh akasema: ((Je, mnaonaje iwapo nitawaeleza kwamba adui atawajieni asubuhi, au atawajieni jioni; je, mtakuwa ni wenye kunisadikisha?)) Wakasema; “Ndio” Akasema: ((Hakika mimi ni mwonyaji kwenu, kabla ya kufikia adhabu kali)) akasema Abuu Lahab: “Kwa ajili ya hili umetukusanya? Kuangamia ni kwako!” Allaah Akateremsha: “Imeteketea mikono miwili ya Abuu Lahab na ameteketea…”

 

Mpaka mwisho wa Suwrah (Taz. Fat-h Al-Baariy) na katika mapokezi mengine, akasimama na hali anaipukusa mikono yake na huku anasema, “Maangamivu ni yako siku zote, ni kwa ajili ya hili umetukusanya?” Allaah Akateremsha: “Imeteketea mikono miwili ya Abuu Lahab na ameteketea…”

 

Rejea pia:

 

026-Asbaabun-Nuzuwl:Ash-Shu'araa Aayah 214: وَأَنذِرْ عَشِيرَتَكَ الْأَقْرَبِينَ 

 

 

 

Asbaabun-Nuzuwl

 

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

 

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

014-Suwrah Ibraahiym Aayah: 27

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

يُثَبِّتُ اللَّـهُ الَّذِينَ آمَنُوا بِالْقَوْلِ الثَّابِتِ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَفِي الْآخِرَةِ ۖ وَيُضِلُّ اللَّـهُ الظَّالِمِينَ ۚ وَيَفْعَلُ اللَّـهُ مَا يَشَاءُ﴿٢٧﴾

Allaah Huwathibitisha wale walioamini kwa kauli thabiti katika uhai wa dunia na Aakhirah. Na Allaah Huwaacha kupotoka madhalimu. Na Allaah Anafanya Atakavyo. [Ibraahiym: 27]

 

 

Sababun-Nuzuwl: 

 

عَنِ الْبَرَاءِ بْنِ عَازِبٍ، عَنِ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ((يُثَبِّتُ اللَّهُ الَّذِينَ آمَنُوا بِالْقَوْلِ الثَّابِتِ‏)) قَالَ: ‏ نَزَلَتْ فِي عَذَابِ الْقَبْرِ فَيُقَالُ لَهُ: مَنْ رَبُّكَ فَيَقُولُ رَبِّيَ اللَّهُ وَنَبِيِّيَ مُحَمَّدٌ صلى الله عليه وسلم ‏.‏ فَذَلِكَ قَوْلُهُ عَزَّ وَجَلَّ: ((يُثَبِّتُ اللَّهُ الَّذِينَ آمَنُوا بِالْقَوْلِ الثَّابِتِ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَفِي الآخِرَةِ))

 

Al-Baraa bin ‘Aazib (رضي الله عنه) amehadithia kwamba: Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema (kuhusu kauli ya Allaah):

 

يُثَبِّتُ اللَّـهُ الَّذِينَ آمَنُوا بِالْقَوْلِ الثَّابِتِ  

Allaah Huwathibitisha wale walioamini kwa kauli thabiti…

 

Amesema: “Imeteremka kuhusiana na adhabu ya kaburini. Huulizwa mtu humo: “Nani Rabb wako?” Husema: “Rabb wangu ni Allaah, na Nabiy wangu ni Muhammad (صلى الله عليه وآله وسلم)”, basi hiyo ndio kauli Yake Allaah (عز وجل):

 

يُثَبِّتُ اللَّـهُ الَّذِينَ آمَنُوا بِالْقَوْلِ الثَّابِتِ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَفِي الْآخِرَةِ ۖ  

Allaah Huwathibitisha wale walioamini kwa kauli thabiti katika uhai wa dunia na Aakhirah.

 

[Muslim - Kitabu Cha Jannah, Sifa Zake, Neema Zake na Wakazi Wake]

 

Riwaayah ya Muslim na Sunan An-Nasaaiy imesema:

 

يُقَالُ لَهُ مَنْ رَبُّكَ فَيَقُولُ رَبِّيَ اللَّهُ وَدِينِي دِينُ مُحَمَّدٍ صلى الله عليه وسلم

“Huulizwa mtu kaburini: Nani Rabb wako? Hujibu: Rabb wangu ni Allaah, na Dini yangu ni Dini ya Muhammad (صلى الله عليه وآله وسلم)…”

 

Na pia,

 

عنِ الْبَرَاءِ بْنِ عَازِبٍ، أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ: ‏"‏الْمُسْلِمُ إِذَا سُئِلَ فِي الْقَبْرِ يَشْهَدُ أَنْ لاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ وَأَنَّ مُحَمَّدًا رَسُولُ اللَّهِ، فَذَلِكَ قَوْلُهُ: ((‏يُثَبِّتُ اللَّهُ الَّذِينَ آمَنُوا بِالْقَوْلِ الثَّابِتِ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَفِي الآخِرَةِ‏))

 

Imehadithiwa na Al-Baraa bin ‘Aazib (رضي الله عنه) kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Muislamu atakapoulizwa kaburini ashuhudie kwamba:

لاَ إِلَهَ إِلاَّ اللَّهُ وَأَنَّ مُحَمَّدًا رَسُولُ اللَّهِ

Hapana mwabudiwa wa haki isipokuwa Allaah na kwamba Muhammad ni Rasuli wa Allaah

 

Basi hiyo ndio maana ya Kauli Yake (Allaah):

 

يُثَبِّتُ اللَّـهُ الَّذِينَ آمَنُوا بِالْقَوْلِ الثَّابِتِ فِي الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَفِي الْآخِرَةِ ۖ  

Allaah Huwathibitisha wale walioamini kwa kauli thabiti katika uhai wa dunia na Aakhirah.

 

[Al-Bukhaariy – Kitaab Cha Tafsiyr]

 

Asbaabun-Nuzuwl

 

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

 

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

013-Suwrah Ar-Ra’d Aayah: 13

 

 

Kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَيُسَبِّحُ الرَّعْدُ بِحَمْدِهِ وَالْمَلَائِكَةُ مِنْ خِيفَتِهِ وَيُرْسِلُ الصَّوَاعِقَ فَيُصِيبُ بِهَا مَن يَشَاءُ وَهُمْ يُجَادِلُونَ فِي اللَّـهِ وَهُوَ شَدِيدُ الْمِحَالِ ﴿١٣﴾

Na radi inamsabihi (Allaah) kwa Himidi Zake na Malaika pia kwa kumkhofu, na Anatuma mingurumo ya radi, humsibu kwayo Amtakaye nao huku (makafiri) wakiwa wanabishana kuhusu Allaah Naye ni Mkali na Mwenye nguvu za kuhujumu. [Ar-Ra’d: 13]

 

Sababun-Nuzuwl: 

 

عن أنس بن مالك، أن رسول الله صلى الله عليه وسلم بعث رجلا مرّة إلى رجل من فراعنة العرب، فقال: "اذهب فادعه لي"، فقال:   "يا رسول الله إنه أعتى من ذلك"، قال: "اذهب فادعه لي"، قال: فذهب إليه فقال: " يدعوك رسول الله" قال:  "وما الله أمن ذهب هو أو من فضة أو من نحاس؟" قال فرجع إلى رسول الله صلى الله عليه وسلم فأخبره، وقال: " قد أخبرتك أنه أعتى من ذلك قال لي كذا وكذا"  فقال : "ارجع إليه الثانية فادعه"، فرجع إليه، فعاد عليه مثل الكلام الأول، فرجع إلى النبيّ صلى الله عليه وسلم فأخبره، فقال: "ارجع إليه"، فرجع الثالثة فأعاد عليه ذلك الكلام، فبينا هو يكلمني إذ بعثت إليه سحابة حيال رأسه فرعدت فوقعت منها صاعقة فذهبت بقحف رأسه، فأنـزل الله تعالى: ((وَيُرْسِلُ الصَّوَاعِقَ فَيُصِيبُ بِهَا مَنْ يَشَاءُ وَهُمْ يُجَادِلُونَ فِي اللَّهِ وَهُوَ شَدِيدُ الْمِحَالِ))

Kutoka kwa Anas bin Maalik amesema: Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alimtuma mtu amwendee mtu miongoni mwa firauni wa ki-Quraysh, Akamwambia “Nenda uniitie!” Akasema: “Ee Rasuli wa Allaah hakika yeye ni mtu jeuri kuliko hivyo (unavyotegemea kuwa ataitikia)” Akasema: “Nenda ukaniitie!” Akaenda (kwa firauni wa ki-Quraysh) akamwambia: “Rasuli Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) anakuita” Akajibu: “Ama Wallahi? Kwani yeye anatokana na dhahabu au fedha au anatokana na shaba?” Akarudi kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akamwambia: “Nilikuambia kuwa yeye ni jeuri mno kuliko hivyo, kwani ameniambia kadhaa wa kadhaa.” Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: “Mwendee tena mara ya pili na mwite.” Akamrudia tena naye yule firauni wa ki-Quraysh akampa maneno yaleyale kama ya mwanzo. akarudi kwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akamjulisha. Akamwambia: “Mrudie tena.” Akamrudia mara ya tatu naye yule jeuri akampa maneno yaleyale.  Akasema: “Basi pindi alipokuwa akinisemesha akateremshiwa wingu juu ya kichwa chake, mngurumo na radi ikampiga na kumuangusha na kusambaratisha fuvu la kichwa chake, hapo Allaah (سبحانه وتعالى) Akateremsha:   

وَيُرْسِلُ الصَّوَاعِقَ فَيُصِيبُ بِهَا مَن يَشَاءُ وَهُمْ يُجَادِلُونَ فِي اللَّـهِ وَهُوَ شَدِيدُ الْمِحَالِ ﴿١٣﴾

Anatuma mingurumo ya radi, humsibu kwayo Amtakaye nao huku (makafiri) wakiwa wanabishana kuhusu Allaah Naye ni Mkali na Mwenye nguvu za kuhujumu. [Ar-Ra’d 13]

 

Asbaabun-Nuzuwl

 

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

Suwrah Al-Mutwaffifiyn

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

 

083-Al-Mutwaffifiyn

 وَيْلٌ لِّلْمُطَفِّفِينَ ﴿١﴾

1. Ole kwa wanaopunja.

 

 

عَنَّ عِكْرِمَة، حَدَّثَهُ عَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ، قَالَ لَمَّا قَدِمَ النَّبِيُّ  صلى الله عليه وسلم الْمَدِينَةَ كَانُوا مِنْ أَخْبَثِ النَّاسِ كَيْلاً فَأَنْزَلَ اللَّهُ سُبْحَانَهُ: ((وَيْلٌ لِلْمُطَفِّفِينَ))‏ فَأَحْسَنُوا الْكَيْلَ بَعْدَ ذَلِكَ ‏.‏

Ikrimah kutoka kwa Ibn ‘Abbaas amehadithia kuwa pindi Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)  alipofika Madiynah alikuta watu wa Madiynah wakipunjiana kilo na walikuwa ni wenye tabia mbaya kabisa katika jambo hilo. Allaah (سبحانه وتعالى) Akateremsha:

 وَيْلٌ لِّلْمُطَفِّفِينَ ﴿١﴾

1. Ole kwa wanaopunja.

 

Na baada ya hapo wakafanya uzuri katika kupima na kuacha tabia yao hiyo mbaya kupunja katika kipimo  [bn Maajah Kitaab At-Tijaraat (2223)]

 

Ibn Kathiyr:

 

Kuongeza na kupunguza katika kupima kwa pishi au mizani ndio sababu ya adhabu kali na kupata hasara.

 

Amepokea An-Nasaaiy na Ibn Maajah kutoka kwa Ibn ‘Abbaas amesema: Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)  alipofika Madiynah walikuwa watu wa Madiynah ni waovu mno kuliko watu wote katika  kupunja Allaah (سبحانه وتعالى)  Akateremsha:

وَيْلٌ لِّلْمُطَفِّفِينَ ﴿١﴾

1. Ole kwa wanaopunja.

 

Wakapima vizuri baada ya hapo [An-Nasaaiy katika Al-Kubraa (6/508) na Ibn Maajah (2/748)]

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 وَيْلٌ لِّلْمُطَفِّفِينَ ﴿١﴾

1. Ole kwa wanaopunja.

 

الَّذِينَ إِذَا اكْتَالُوا عَلَى النَّاسِ يَسْتَوْفُونَ ﴿٢﴾

2. Ambao wanapopokea kipimo kwa watu wanataka wapimiwe kamilifu.

 

وَإِذَا كَالُوهُمْ أَو وَّزَنُوهُمْ يُخْسِرُونَ ﴿٣﴾

3. Na wanapowapimia (watu) kwa kipimo au wanawapimia kwa mizani wanapunja.

 

أَلَا يَظُنُّ أُولَـٰئِكَ أَنَّهُم مَّبْعُوثُونَ ﴿٤﴾

4. Je, hawadhanii kwamba wao watafufuliwa?

 

لِيَوْمٍ عَظِيمٍ ﴿٥﴾

5. Kwenye Siku adhimu.

 

يَوْمَ يَقُومُ النَّاسُ لِرَبِّ الْعَالَمِينَ ﴿٦﴾

6. Siku watakayosimama watu kwa Rabb wa walimwengu.

 

 

Asbaabun-Nuzuwl

 

 أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

 

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

048-Al-Fat-h Aayah 5

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

  لِّيُدْخِلَ الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا وَيُكَفِّرَ عَنْهُمْ سَيِّئَاتِهِمْ ۚ وَكَانَ ذَٰلِكَ عِندَ اللَّـهِ فَوْزًا عَظِيمًا﴿٥﴾

Ili Awaingize Waumini wa kiume na Waumini wa kike Jannaat zipitazao chini yake mito, ni wenye kudumu humo, na Awafutie maovu yao; na kukawa huko mbele ya Allaah, ni kufuzu adhimu. [Al-Fat-h: 5]

 

Sababun-Nuzuwl: 

 

عَنْ أَنَسٍ، رضى الله عنه قَالَ أُنْزِلَتْ عَلَى النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلمَ ‏:‏ ‏((ليغْفِرَ لَكَ اللَّهُ مَا تَقَدَّمَ مِنْ ذَنْبِكَ وَمَا تَأَخَّر))َ  مَرْجِعَهُ مِنَ الْحُدَيْبِيَةِ فَقَالَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم ‏"‏ لَقَدْ أُنْزِلَتْ عَلَىَّ آيَةٌ أَحَبُّ إِلَىَّ مِمَّا عَلَى الأَرْضِ ثُمَّ قَرَأَهَا النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم عَلَيْهِمْ فَقَالُوا هَنِيئًا مَرِيئًا يَا نَبِيَّ اللَّهِ قَدْ بَيَّنَ اللَّهُ لَكَ مَاذَا يُفْعَلُ بِكَ فَمَاذَا يُفْعَلُ بِنَا فَنَزَلَتْ عَلَيْهِ: ((ليُدْخِلَ الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِنْ تَحْتِهَا الأَنْهَارُ))  حَتَّى بَلَغَ ‏:‏ ‏((‏فوزًا عَظِيمًا ))‏  قَالَ هَذَا حَدِيثٌ حَسَنٌ صَحِيحٌ  ‏.‏

 

Anas bin Maalik amehadithia kwamba: Tulipokuwa tunarudi kutoka Hudaybiyah, iliteremshwa kwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم):

لِّيَغْفِرَ لَكَ اللَّـهُ مَا تَقَدَّمَ مِن ذَنبِكَ وَمَا تَأَخَّرَ وَيُتِمَّ نِعْمَتَهُ عَلَيْكَ وَيَهْدِيَكَ صِرَاطًا مُّسْتَقِيمًا﴿٢﴾

Ili Allaah Akughufurie yale yaliyotangulia katika madhambi yako na yale yanayofuatia; na Akutimizie neema Yake juu yako na Akuongoze njia iliyonyooka.

 

Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: “Hakika nimeteremshiwa Aayah ambayo ni kipenzi mno kuliko chochote kilichoko duniani.” Kisha Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akawasomea Aayah hiyo, wakasema: Hongera kwako ee Nabiy wa Allaah, hakika Allaah Amekubainishia Atakalokufanyia, lakini je Atatufanyia nini sisi? Hapo ikateremshwa: 

 

لِّيُدْخِلَ الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا وَيُكَفِّرَ عَنْهُمْ سَيِّئَاتِهِمْ ۚ وَكَانَ ذَٰلِكَ عِندَ اللَّـهِ فَوْزًا عَظِيمًا﴿٥﴾

Ili Awaingize Waumini wa kiume na Waumini wa kike Jannaat zipitazao chini yake mito, ni wenye kudumu humo, na Awafutie maovu yao; na kukawa huko mbele ya Allaah, ni kufuzu adhimu. [Al-Fat-h: 5]

 [At-Tirmidhiy Amesema Hadiyth Hasan Swahiyh]