048-Asbaabun-Nuzuwl: Al-Fat-h Aayah 01-5: إِنَّا فَتَحْنَا لَكَ فَتْحًا مُّبِينًا

 

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

 

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

048-Al-Fat-h: Aayah 1 - 5

 

 

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّا فَتَحْنَا لَكَ فَتْحًا مُّبِينًا﴿١﴾

Hakika Tumekupa ushindi (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم), ushindi bayana.

 

لِّيَغْفِرَ لَكَ اللَّـهُ مَا تَقَدَّمَ مِن ذَنبِكَ وَمَا تَأَخَّرَ وَيُتِمَّ نِعْمَتَهُ عَلَيْكَ وَيَهْدِيَكَ صِرَاطًا مُّسْتَقِيمًا﴿٢﴾

Ili Allaah Akughufurie yale yaliyotangulia katika madhambi yako na yale yanayofuatia; na Akutimizie neema Yake juu yako na Akuongoze njia iliyonyooka.

 

وَيَنصُرَكَ اللَّـهُ نَصْرًا عَزِيزًا﴿٣﴾

Na Akunusuru Allaah nusura yenye nguvu kabisa.

 

هُوَ الَّذِي أَنزَلَ السَّكِينَةَ فِي قُلُوبِ الْمُؤْمِنِينَ لِيَزْدَادُوا إِيمَانًا مَّعَ إِيمَانِهِمْ ۗ وَلِلَّـهِ جُنُودُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ ۚ وَكَانَ اللَّـهُ عَلِيمًا حَكِيمًا﴿٤﴾

Yeye Ndiye Aliyeteremsha utulivu katika nyoyo za Waumini ili Awazidishie iymaan pamoja na iymaan zao. Na ni ya Allaah Pekee majeshi ya mbinguni na ardhini, na Allaah ni daima Mjuzi wa yote, Mwenye hikmah wa yote.

 

لِّيُدْخِلَ الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا وَيُكَفِّرَ عَنْهُمْ سَيِّئَاتِهِمْ ۚ وَكَانَ ذَٰلِكَ عِندَ اللَّـهِ فَوْزًا عَظِيمًا﴿٥﴾

Ili Awaingize Waumini wa kiume na Waumini wa kike Jannaat zipitazao chini yake mito, ni wenye kudumu humo, na Awafutie maovu yao; na kukawa huko mbele ya Allaah, ni kufuzu adhimu.

 [[Al-Fat-h: 1 – 5]

 

 

Sababun-Nuzuwl: 

 

 

عَنْ أَنَسٍ ابن مالك رضى الله عنه  قَالَ لَمَّا نَزَلَتْ: ((إِنَّا فَتَحْنَا لَكَ فَتْحًا مُبِينًا * لِيَغْفِرَ لَكَ اللَّهُ‏))  إِلَى قَوْلِهِ: ((‏فَوْزًا عَظِيمًا‏))‏ مَرْجِعَهُ مِنَ الْحُدَيْبِيَةِ وَهُمْ يُخَالِطُهُمُ الْحُزْنُ وَالْكَآبَةُ وَقَدْ نَحَرَ الْهَدْىَ بِالْحُدَيْبِيَةِ فَقَالَ ‏"‏ لَقَدْ أُنْزِلَتْ عَلَىَّ آيَةٌ هِيَ أَحَبُّ إِلَىَّ مِنَ الدُّنْيَا جَمِيعًا ‏"‏ ‏.‏

 Anas bin Maalik (رضي الله عنه) amesema:  Ilipoteremka:

 

إِنَّا فَتَحْنَا لَكَ فَتْحًا مُّبِينًا﴿١﴾

Mpaka kauli Yake:

فَوْزًا عَظِيمًا

Alipokuwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) na Maswahaba  wanarudi kutoka Hudaybiyah wakiwa katika hali ya kuzidiwa na  ghadhabu, huzuni na dhiki (kwa kuzuiliwa na Makafiri Quryash kuingia Makkah) Wakawa wamechinja Hady (mnyana wa Hajj) wao. (Hapo zikateremshwa Aayah hizo) na Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasema: “Hakika nimeteremshiwa Aayah ambazo ni vipenzi zaidi kuliko dunia nzima.”  [Muslim Kitaab Al-Jihaad Was Sayr]    

 

 

Pia,

 

عَنْ أَنَسٍ ابن مالك رضى الله عنه:  ((إِنَّا فَتَحْنَا لَكَ فَتْحًا مُّبِينًا))  قالَ الْحُدَيْبِيَةُ‏.‏ قَالَ أَصْحَابُهُ هَنِيئًا مَرِيئًا فَمَا لَنَا?  فَأَنْزَلَ اللَّهُ : ‏ ‏((لِيُدْخِلَ الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ جَنَّاتٍ‏))  قَالَ شُعْبَةُ فَقَدِمْتُ الْكُوفَةَ فَحَدَّثْتُ بِهَذَا كُلِّهِ عَنْ قَتَادَةَ ثُمَّ رَجَعْتُ فَذَكَرْتُ لَهُ فَقَالَ أَمَّا:  ‏((‏إِنَّا فَتَحْنَا لَكَ‏))‏ فَعَنْ أَنَسٍ، وَأَمَّا هَنِيئًا مَرِيئًا فَعَنْ عِكْرِمَةَ‏.

Anas bin Maalik (رضي الله عنه) amesema kuhusu:

إِنَّا فَتَحْنَا لَكَ فَتْحًا مُّبِينًا

Inahusiana na (Bay’ah) ya Hudaybiyah.  Maswahaba wa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) wakasema kumwambia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): “Hongera na furaha kwako, lakini je sisi tunapata nini?” Hapo Allaah Akateremsha:

 

لِّيُدْخِلَ الْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ جَنَّاتٍ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الْأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا وَيُكَفِّرَ عَنْهُمْ سَيِّئَاتِهِمْ ۚ وَكَانَ ذَٰلِكَ عِندَ اللَّـهِ فَوْزًا عَظِيمًا﴿٥﴾

Ili Awaingize Waumini wa kiume na Waumini wa kike Jannaat zipitazao chini yake mito, ni wenye kudumu humo, na Awafutie maovu yao; na kukawa huko mbele ya Allaah, ni kufuzu adhimu. [Al-Bukhaariy]

 

Pia,

 

عن أَنَسٍ ابن مالك رضى الله عنه  عن زَيْدِ بْنِ أَسْلَمَ، عَنْ أَبِيهِ، قَالَ سَمِعْتُ عُمَرَ بْنَ الْخَطَّابِ، رضى الله عنه يَقُولُ كُنَّا مَعَ رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فِي بَعْضِ أَسْفَارِهِ فَكَلَّمْتُ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَسَكَتَ ثُمَّ كَلَّمْتُهُ فَسَكَتَ ثُمَّ كَلَّمْتُهُ فَسَكَتَ فَحَرَّكْتُ رَاحِلَتِي فَتَنَحَّيْتُ وَقُلْتُ ثَكِلَتْكَ أُمُّكَ يَا ابْنَ الْخَطَّابِ نَزَرْتَ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم ثَلاَثَ مَرَّاتٍ كُلُّ ذَلِكَ لاَ يُكَلِّمُكَ مَا أَخْلَقَكَ أَنْ يَنْزِلَ فِيكَ قُرْآنٌ قَالَ فَمَا نَشِبْتُ أَنْ سَمِعْتُ صَارِخًا يَصْرُخُ بِي قَالَ فَجِئْتُ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَقَالَ: "يَا ابْنَ الْخَطَّابِ لَقَدْ أُنْزِلَ عَلَىَّ هَذِهِ اللَّيْلَةَ سُورَةٌ مَا أُحِبُّ أَنَّ لِي بِهَا مَا طَلَعَتْ عَلَيْهِ الشَّمْسُ" ‏:‏ ‏((‏إنَّا فَتَحْنَا لَكَ فَتْحًا مُبِينًا )) ‏.‏ قَالَ أَبُو عِيسَى هَذَا حَدِيثٌ حَسَنٌ صَحِيحٌ غَرِيبٌ

 

Kutoka kwa Anas bin Maalik kutoka Zayd bin Aslam kutoka kwa baba yake amesema: Nilimsikia  'Umar bin Al-Khattwaab (رضي الله عنه)  akisema: Tulikuwa na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  wakati mmoja wa safari zake, nikamwambia jambo lakini alikuwa kimya. Kisha nikamwambia tena lakini alikuwa kimya. Nikaharakiza kasi yangu ya kipando changu kwenda mbele. Nikasema (kujiambia mwenyewe): “Mama yako akupoteze ee ibn Al-Khattwaab! Umemchagiza Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  mara tatu na kila mara hakukujibu! Unastahili kwamba uteremshiwe jambo  juu yako katika Qur-aan.” (‘Umar) Akasema:  Haikuchukua muda mrefu kabla kusikia sauti ikiniita.   Nikamwendea Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  akasema: “Ee ibn Al-Khatwaab! Imeteremshwa Suwrah kwangu jana usiku ambayo ni kipendzi zaidi kwangu kulikoni chochote kile  kinachochomozewa na jua.”

 

إِنَّا فَتَحْنَا لَكَ فَتْحًا مُّبِينًا

 

[At-Tirmidhiy amesema Hadiyth Hasan Swahiyh Ghariyb]

 

Na katika Riwaayah nyenginezo kama hizo:

 

عَنْ زَيْدِ بْنِ أَسْلَمَ، عَنْ أَبِيهِ، أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم كَانَ يَسِيرُ فِي بَعْضِ أَسْفَارِهِ، وَعُمَرُ بْنُ الْخَطَّابِ يَسِيرُ مَعَهُ لَيْلاً، فَسَأَلَهُ عُمَرُ بْنُ الْخَطَّابِ عَنْ شَىْءٍ فَلَمْ يُجِبْهُ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم ثُمَّ سَأَلَهُ فَلَمْ يُجِبْهُ، ثُمَّ سَأَلَهُ فَلَمْ يُجِبْهُ وَقَالَ عُمَرُ بْنُ الْخَطَّابِ ثَكِلَتْكَ أُمُّكَ يَا عُمَرُ، نَزَرْتَ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم ثَلاَثَ مَرَّاتٍ، كُلُّ ذَلِكَ لاَ يُجِيبُكَ‏.‏ قَالَ عُمَرُ فَحَرَّكْتُ بَعِيرِي ثُمَّ تَقَدَّمْتُ أَمَامَ الْمُسْلِمِينَ، وَخَشِيتُ أَنْ يَنْزِلَ فِيَّ قُرْآنٌ، فَمَا نَشِبْتُ أَنْ سَمِعْتُ صَارِخًا يَصْرُخُ بِي ـ قَالَ ـ فَقُلْتُ لَقَدْ خَشِيتُ أَنْ يَكُونَ نَزَلَ فِيَّ قُرْآنٌ‏.‏ وَجِئْتُ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَسَلَّمْتُ عَلَيْهِ فَقَالَ ‏"‏ لَقَدْ أُنْزِلَتْ عَلَىَّ اللَّيْلَةَ سُورَةٌ لَهِيَ أَحَبُّ إِلَىَّ مِمَّا طَلَعَتْ عَلَيْهِ الشَّمْسُ، ثُمَّ قَرَأَ: ((إِنَّا فَتَحْنَا لَكَ فَتْحًا مُبِينًا‏))

 

Kutoka kwa Zayd bin Aslam kutoka kwa baba yake kwamba Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم)  alikuwa katika safari usiku mmoja na ‘Umar bin Al-Khatwaab alikwa pamoja naye. ‘Umar  ibn Al-Khatwaab akamuuliza Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) jambo lakini hakumjibu. Kisha akamuuliza tena lakini hakumjibu. Akamuuliza tena lakini hakumjibu.  ‘Umar akasema:  (kujiambia mwenyewe): “Ee ibn Al-Khatwaab! Mama yako akupoteze, kwani umemchagiza (صلى الله عليه وآله وسلم) mara tatu, lakini hakukujibu.”  ‘Umar Akasema Nikamwendesha mnyama wangu kwa kasi kuwatangulia  Waislamu mbele na nikawa nakhofu kuwa iteremshwa jambo katika Qur-aan.  Sikusubiri hata dakika nikasikia mtu ananiita. Nikasema: Nilikuwa nakhofu kwamba nimeteremshiwa Qur-aan. Nikafika kwa Rasuli wa Alaah (صلى الله عليه وآله وسلم) nikamsalimia akasema:  “Hakika nimeteremshiwa  usiku Suwrah ambayo hakika ni kipenzi kwangu kuliko chochote kile kilichochomozewa na jua.” Kisha akasoma:

إِنَّا فَتَحْنَا لَكَ فَتْحًا مُّبِينًا

[Al-Bukhaariy  Kitaab Al-Maghaaziy; Baab Ghazwat Al-Hudaybiyah, pia Riwaaya kama hizo katika Kitaab Fadhwaail Al-Qur-aan, Kitaab At-Tafsiyr]

Share