40-Al-Arba’uwn An-Nawawiyyah: Kuwa Duniani Kama Vile Mgeni Au Mpita Njia

 

Al-Arba’uwn An-Nawawiyyah:

 

Hadiyth Ya 40

 

كُنْ في الدُّنْيا كأنَّكَ غَرِيبٌ أو عابرُ سبِيلٍ

 

Kuwa Duniani Kama Vile Mgeni Au Mpita Njia

 

Alhidaaya.com

 

 

 

Sikiliza Hadiyth:

 

 

 

عن ابنِ عُمَرَ رضي اللهُ عنهما قال: أَخَذَ رسُول اللهِ صلى الله عليه وسلم بِمَنْكِبيَّ فقال: ((كُنْ في الدُّنْيا كأنَّكَ غَرِيبٌ، أو عابرُ سبِيلٍ))

 

وكانَ ابنُ عُمَرَ رَضي اللهُ عنهما يقولُ: إذا أمْسَيْتَ فلا تَنْتظِرِ الصبَّاحَ، وإذا أصْبَحْتَ فلا تَنْتَظِرِ الَمسَاءَ، وخُذْ مِنْ صِحَّتِكَ لِمَرضِكَ، ومِنْ حَياتِكَ لِمَوْتِكَ. رَوَاهُ الْبُخَارِيُّ    

Imepokelewa kutoka kwa Ibn ‘Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) ambaye amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alinishika bega akasema: “Kuwa (ishi) duniani kama vile mgeni au mpita njia.”

 

Na Ibn ‘Umar (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) alikuwa akisema: Utakapoamka basi usingojee (kutegemea kuishi mpaka) asubuhi. Na utakapoamka asubuhi basi usingojee (kutegemea kuishi mpaka) jioni. Na chukua (mafao ya) siha yako kwa maradhi yako, na (mafao ya) uhai wao kwa mauti yako.  [Al-Bukhaariy]

 

 

 

Share