Imaam Ibn Baaz: Vitabu Muhimu Vya Tafsiyr, Hadiyth Na Fiqh

 

Vitabu Muhimu Vya Tafsiyr, Hadiyth Na Fiqh

 

Imaam Ibn Baaz (Rahimahu Allaah)

 

Alhidaaya.com

 

 

SWALI:

 

Naomba unieleweshe majina ya vitabu muhimu vya Tafsiyr (ufafanuzi wa maana za Qur-aan), Hadiyth na Fiqh (Falsafa ya Shariy’ah ya Kiislamu).

 

 

JIBU:

 

 

 

A-Vitabu muhimu vya Tafsiyr ni pamoja na:

 

 

1. Tafsiyr ya Ibn Jariyr

 

2. Tafsiyr ya Ibn Kathiyr

 

3. Al-Baghaway

 

4. Ibn Sa’dy na

 

5. Al-Shanqiytwiy.

 

 

 

B-Vitabu muhimu vya Hadiyth ni pamoja na:

 

 

1. Vitabu viwili Swahiyh vya Hadiyth (yaani Al-Bukhaariy na Muslim)

 

2. Sunan (mikusanyiko ya Hadiyth ambazo zimefafanuliwa kwa maudhui ya ki-Fiqh) iliyoandikwa na Wakusanyaji Wanne wa Hadiyth (Imaam Abuu Daawuwd, At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy na Ibn Maajah)

 

3. Muntaqa Al-Akhbaar

 

4. ‘Umdat Al-Hadiyth

 

5. Buluwgh Al-Maraam na

 

6. Al-Arba’un An-Nawawiyyah na hitimisho za Al-Haafidhw Ibn Rajab. Ni Hadiyth khamsini zilizosimuliwa kutoka kwa Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) chini ya jina la Jawami’ Al-Kalim (fupi lakini ni lenye kutosheleza kiufafanuzi).

 

 

 

C-Vitabu muhimu vya Fiqh ni pamoja na:

 

1. Al-Mughny na Al-Muqni’ ambacho ni cha Mwanachuoni mkubwa, Imaam Abuu Muhammad bin ‘Abdillaah bin Qudaamah (Rahimahu Allaah)

 

2. Al-Rawdhw Al-Murabba’ Sharh Zaad Al-Mustanqa’ chenye sharh ya Shaykh ‘Abdur-Rahmaan bin Qaasim (Rahimahu Allaahu) na

 

3. Sharh Al-Muhadhab cha An-Nawawiy (Rahimahu Allaahu).

 

Allaah Atujaalie mafanikio!

 

 

[Fataawa Ibn Baaz, Angalia kwa namba ya Sura, Sura ya 24, Kitabu Kuhusiana Na Tafsiyr, Vitabu Muhimu Vya Tafsiyr]

 

 

 

 

Share