05-Swahiyh Fiqh As-Sunnah: Kitabu Cha Ndoa: Mwanamke Anaweza Kukataa Kuolewa

 

Swahiyh Fiqh As-Sunnah

 

كِتَابُ الزَّوَاجِ

 

Kitabu Cha Ndoa

  

Alhidaaya.com 

 

 

05-Mwanamke Anaweza Kukataa Kuolewa:

 

Ni kwa Hadiyth y a Abu Sa’iyd:

 

"إِنَّ رَجُلاً أَتَى بابْنَةٍ له إِلى النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ  فَقَالَ: إِنَّ ابْنَتِي هذه أَبَتْ أَنْ تَتَزَوَّجَ، قَالَ: فَقَالَ لَهَا: أَطِيْعِيْ أَبَاكِ، فَقَالَت: لا، حَتَّى تُخْبِرَنِي ما حَقُّ الزَّوْجِ على زَوْجَتِهِ؟ فَرَدَّتْ عليه مَقَالَتَهَا، فَقَالَ: حَقُّ الزَّوْجِ على زَوْجَتِه: أَنْ لَوْ كَانَ به قُرْحَةً فَلَحَسَتْهَا أَوْ ابْتَدَرَ منخراه صَدِيْدًا أَوْ دَمًا ثُمَّ لَحَسَتْهُ مَا أَدَّتْ حَقَّهُ، فَقَالَتْ: وَالذيْ بَعَثَكَ بالحق، لا أتَزَوَّجُ أَبَدًا، فَقَالَ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: لا تُنْكِحُوْهُنَّ إِلاَّ بإِذْنِهِنَّ"

 

“Mtu mmoja alikwenda na binti yake kwa Rasuli (Swalla Allaah ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia:  Binti yangu huyu amekataa kuolewa.  Rasuli akamwambia binti:  Mtii baba yako.  Binti akasema:  Sikubali, mpaka unieleze ni ipi haki ya mke kumtekelezea mumewe?  Akakariri maneno hayo kwa Rasuli.  Rasuli akamwambia:  Haki ya mke kumtekelezea mumewe ni kuwa, ikiwa mumewe ana kidonda naye akakipangusa kwa ulimi wake, au kikatumbuka usaha au damu kisha akailamba, basi anakuwa bado hajatekeleza haki yake.  Binti akasema:  Naapa kwa Yule Ambaye Amekutuma kwa haki, kamwe sitoolewa.  Na Rasuli akasema:  Msiwaozeshe isipokuwa kwa ridhaa yao”.  [Hadiyth Hasan.  Imekharijiwa na Ibn Abiy Shaybah (17116)]   

 

 

Share