Wali Wa Kisomali Wa Kuku

 Wali Wa Kisomali Wa Kuku

 

Vipimo                                                   

Mchele - 3 vikombe

Vitunguu (viliokatwa vidogo vidogo) - 2

Mafuta - 3 vijiko vya supu

Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi iliyosagwa - 1 kijiko cha chai

Bizari ya pilau - 1 kijiko cha supu

Mdalasini - 1 kijiti

Hiliki - 3 chembe

Pilipili manga nzima - chembe chache

Siagi - Vijiko 2 vya supu                                                                        

Chumvi - kiasi

 

KUKU

Kuku kidari (Breast)   kata vipande vipande - 2 LB

Mafuta - 3 vijiko vya supu

Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi iliyosagwa - 1 kijiko cha supu

Pilipili mbichi iliyosagwa - 1 kijiko cha supu

Kotmiri iliyokatwa ndogo ndogo - kiasi

Bizari ya pilau (cummin au jiyrah) - 1 kijiko cha chai

Pilipili kubwa tamu la kijani - 1

Pilipili kubwa tamu nyekundu - 1                         

(zikate vipande vipande)

Karoti iliyokunwa - 1 – 2

Chumvi - Kiasi

 

NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA

Wali:

  1. Roweka mchele kwa muda fulani kutegemea mchele
  2. Katika sufuria tia mafuta na kaanga vitunguu hadi vibadilike  rangi kidogo.
  3. Tia thomu iliyosagwa, mdalasini, bizari ya pilau, hiliki, pilipili manga na chumvi, kaanga kidogo.
  4. Tia mchele kaanga kidogo, kisha tia maji ya moto kiasi  kutegemea na aina ya mchele kama kawaida ya kupika wali kama pilau.
  5. Tia sigai, funika upikike wali hadi uwive.

Kuku:

  1. Mchanganye kuku pamoja na thomu/tangawizi iliyosagwa, chumvi, pilipili mbichi.
  2. Katika karai tia mafuta yapate moto vizuri.
  3. Mtie kuku, bizari ya pilau (jiyrah) na ukaange, karibu na kuiva tia vitunguu.
  4. Tia mapilipili makubwa, kotmiri, na kaanga kwa dakika moja tu uzime moto na epua weka kando.

Kupakua:

Pakua wali katika sahani.

Pambia karoti iliyokunwa na ukipenda zabibu na wali uko tayari   kuliwa

 

Share