22-Swahiyh Al-Bukhaariy: Kitabu Cha As-Sahw (Kusahau Katika Swalaah) - كتاب السّهو

 

 

 

كِتابُ السّهو

22-Kitabu Cha As-Sahw (Kusahu Katika Swalaah)

 

 

 

Alhidaaya.com

 

 

 

 

 

01-Mlango

 

 باب مَا جَاءَ فِي السَّهْوِ إِذَا قَامَ مِنْ رَكْعَتَىِ الْفَرِيضَةِ

 

Kinachosemwa Kuhusu As-Sahw (Kusahau) Endapo Mtu Atasimama (Kuswali Rakaa Ya Tatu Bila Kukaa) Baada Ya Rakaa Ya Pili Ya Swalaah Ya Faradhi

 

 

 

حَدَّثَنَا عَبْدُ اللَّهِ بْنُ يُوسُفَ، أَخْبَرَنَا مَالِكُ بْنُ أَنَسٍ، عَنِ ابْنِ شِهَابٍ، عَنْ عَبْدِ الرَّحْمَنِ الأَعْرَجِ، عَنْ عَبْدِ اللَّهِ ابْنِ بُحَيْنَةَ ـ رضى الله عنه ـ أَنَّهُ قَالَ صَلَّى لَنَا رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم رَكْعَتَيْنِ مِنْ بَعْضِ الصَّلَوَاتِ ثُمَّ قَامَ فَلَمْ يَجْلِسْ، فَقَامَ النَّاسُ مَعَهُ، فَلَمَّا قَضَى صَلاَتَهُ وَنَظَرْنَا تَسْلِيمَهُ كَبَّرَ قَبْلَ التَّسْلِيمِ فَسَجَدَ سَجْدَتَيْنِ وَهُوَ جَالِسٌ ثُمَّ سَلَّمَ‏.‏

 

Amesimulia ‘Abdullaah Bin Buhaynah (رضي الله عنه):

 

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alituswalisha Rakaa mbili akasimama (kwa ajili ya Rakaa ya tatu) bila kukaa chini kwanza (baada ya Rakaa ya pili). Watu nao wakamfuata na kusimama naye. Alivyokaribia kumaliza Swalaah yake, tulimngojea mpaka akamaliza Swalaah hiyo, lakini akatamka Takbiyr kabla ya Tasliym na akasujudu mara mbili (Sajdatu-Sahw) wakati alipokaa, kisha akamaliza Swalaah hiyo kwa Tasliym.

 

Swahiyh Al-Bukhaariy: Hadiyth: 1224

Mjalada: 2

 

Kitabu: 22

 

Hadiyth: 1

 

 

 

حَدَّثَنَا عَبْدُ اللَّهِ بْنُ يُوسُفَ، أَخْبَرَنَا مَالِكٌ، عَنْ يَحْيَى بْنِ سَعِيدٍ، عَنْ عَبْدِ الرَّحْمَنِ الأَعْرَجِ، عَنْ عَبْدِ اللَّهِ ابْنِ بُحَيْنَةَ ـ رضى الله عنه ـ أَنَّهُ قَالَ إِنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَامَ مِنِ اثْنَتَيْنِ مِنَ الظُّهْرِ لَمْ يَجْلِسْ بَيْنَهُمَا، فَلَمَّا قَضَى صَلاَتَهُ سَجَدَ سَجْدَتَيْنِ ثُمَّ سَلَّمَ بَعْدَ ذَلِكَ‏.‏

 

Amesimulia ‘Abdullaah Bin Buhaynah (رضي الله عنه):

 

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alisimama baada ya Rakaa ya pili ya Swalaah ya Adhuhuri bila ya kukaa chini (baina ya Rakaa ya pili na ya tatu). Alipomaliza Swalaah alisujudu Sijdah mbili (za Sahw; za kusahau), kishaa akamalizia Swalaah kwa Tasliym.

 

Swahiyh Al-Bukhaariy: Hadiyth: 1225

Mjalada: 2

 

Kitabu: 22

 

Hadiyth: 2

 

 

 

 

 

 

02-Mlango

باب إِذَا صَلَّى خَمْسًا

 

Endapo Mtu Anaswali Rakaa Tano (Badala Ya Rakaa Nne)

 

 

 

حَدَّثَنَا أَبُو الْوَلِيدِ، حَدَّثَنَا شُعْبَةُ، عَنِ الْحَكَمِ، عَنْ إِبْرَاهِيمَ، عَنْ عَلْقَمَةَ، عَنْ عَبْدِ اللَّهِ ـ رضى الله عنه ـ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم صَلَّى الظُّهْرَ خَمْسًا فَقِيلَ لَهُ أَزِيدَ فِي الصَّلاَةِ فَقَالَ ‏ "‏ وَمَا ذَاكَ ‏"‏‏.‏ قَالَ صَلَّيْتَ خَمْسًا‏.‏ فَسَجَدَ سَجْدَتَيْنِ بَعْدَ مَا سَلَّمَ‏.‏

 

Amesimulia ‘Abdullaah (رضي الله عنه):

 

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) aliswali Rakaa tano katika Swalaah ya Adhuhuri, mtu mmoja akamuuliza iwapo Rakaa zimeongezeka Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akauliza: “Unasema nini?” Yule mtu akasema: “Umeswalisha Rakaa tano.” Hapo Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akasujudu Sijdah mbili za Sahw baada ya Tasliym.

 

Swahiyh Al-Bukhaariy: Hadiyth: 1226

Mjalada: 2

 

Kitabu: 22

 

Hadiyth: 3

 

 

 

 

 

 

03-Mlango

 

باب إِذَا سَلَّمَ فِي رَكْعَتَيْنِ أَوْ ثَلاَثٍ فَسَجَدَ سَجْدَتَيْنِ مِثْلَ سُجُودِ الصَّلاَةِ أَوْ أَطْوَلَ

 

Ikiwa Mtu Anamaliza Swalaah Yake Kwa Tasliym Baada Ya Kuswali Rakaa Mbili Au Tatu (Kwa Makosa), Basi Alete Sijdah Mbili Kama Sijdah Za Kawaida Za Swalaah Au Ndefu Zaidi

 

 

 

حَدَّثَنَا آدَمُ، حَدَّثَنَا شُعْبَةُ، عَنْ سَعْدِ بْنِ إِبْرَاهِيمَ، عَنْ أَبِي سَلَمَةَ، عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ ـ رضى الله عنه ـ قَالَ صَلَّى بِنَا النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم الظُّهْرَ أَوِ الْعَصْرَ فَسَلَّمَ، فَقَالَ لَهُ ذُو الْيَدَيْنِ الصَّلاَةُ يَا رَسُولَ اللَّهَ أَنَقَصَتْ فَقَالَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم لأَصْحَابِهِ ‏ "‏ أَحَقٌّ مَا يَقُولُ ‏"‏‏.‏ قَالُوا نَعَمْ‏.‏ فَصَلَّى رَكْعَتَيْنِ أُخْرَيَيْنِ ثُمَّ سَجَدَ سَجْدَتَيْنِ‏.

 

‏ قَالَ سَعْدٌ وَرَأَيْتُ عُرْوَةَ بْنَ الزُّبَيْرِ صَلَّى مِنَ الْمَغْرِبِ رَكْعَتَيْنِ فَسَلَّمَ وَتَكَلَّمَ ثُمَّ صَلَّى مَا بَقِيَ وَسَجَدَ سَجْدَتَيْنِ وَقَالَ هَكَذَا فَعَلَ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم‏.‏

 

Amesimulia Abu Hurayrah (رضي الله عنه):  

 

Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alituswalisha Swalaah ya Adhuhuri au Alasiri na akaimalizia kwa Tasliym. Dhul-Yadayn alimwambia: “Ee Rasuli wa Allaah! Je, hii imepunguzwa?” Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akawauliza Swahaba zake: “Je, amesema kweli?”  Wakajibu: “Naam!” Basi Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akaswalisha Rakaa mbili   kisha akafanya Sijdah mbili (za Sahw).

 

Sa’ad alisema: “Nilimuona ‘Urwah bin Az-Zubayr aliswali Rakaa mbili (badala ya tatu) katika Swalaah ya Maghribi na akamaliza kwa Tasliym. Kisha akaongea. (Alipojulishwa kuhusu hivyo), alikamilisha salio la Swalaah yake kisha akasujudu Sijdah mbili, kisha akasema: “Hivi ndivyo alivyofanya Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم).”

 

Swahiyh Al-Bukhaariy: Hadiyth: 1227

Mjalada: 2

 

Kitabu: 22

 

Hadiyth: 4

 

 

 

 

 

 

04-Mlango

 

باب مَنْ لَمْ يَتَشَهَّدْ فِي سَجْدَتَىِ السَّهْوِ

 

Ambaye Hakuisoma Tashahhud (Attaahiyyaat) Baada Ya Sijdah Za Sahw

 

 

 

وَسَلَّمَ أَنَسٌ وَالْحَسَنُ وَلَمْ يَتَشَهَّدَا.
وَقَالَ قَتَادَةُ لاَ يَتَشَهَّدُ.

 

Anas na Al-Hasan walimalizia Swalaah kwa Tasliym bila ya kuisoma Tashahhud. Na Qataadah alisema kuwa Tashahhud haitakiwi kusomwa (baada ya kuleta Sijdatus-Sahw).  

 

 

حَدَّثَنَا عَبْدُ اللَّهِ بْنُ يُوسُفَ، أَخْبَرَنَا مَالِكُ بْنُ أَنَسٍ، عَنْ أَيُّوبَ بْنِ أَبِي تَمِيمَةَ السَّخْتِيَانِيِّ، عَنْ مُحَمَّدِ بْنِ سِيرِينَ، عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ ـ رضى الله عنه ـ‏.‏ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم انْصَرَفَ مِنِ اثْنَتَيْنِ فَقَالَ لَهُ ذُو الْيَدَيْنِ أَقُصِرَتِ الصَّلاَةُ أَمْ نَسِيتَ يَا رَسُولَ اللَّهِ فَقَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏ "‏ أَصَدَقَ ذُو الْيَدَيْنِ ‏"‏‏.‏ فَقَالَ النَّاسُ نَعَمْ‏.‏ فَقَامَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَصَلَّى اثْنَتَيْنِ أُخْرَيَيْنِ ثُمَّ سَلَّمَ ثُمَّ كَبَّرَ فَسَجَدَ مِثْلَ سُجُودِهِ أَوْ أَطْوَلَ ثُمَّ رَفَعَ‏.‏

 

Amesimulia Abu Hurayrah (رضي الله عنه):  

 

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) aliswalisha Rakaa mbili   akamaliza Swalaah yake. Dhul-Yadayn alimuuliza: “Je, hii Swalaah imepunguwa au wewe umesahau Rasuli wa Allaah?” akauliza: “Je Dhul-Yadayn kasema kweli?” Watu     wakajibu: “Naam!” Hapo Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akasimama akaswali Rakaa mbili zilizobakia na akamalizia kwa Tasliym. Kisha akatamka Takbiyr na akaleta Sijdah mbili kama za kawaida au ndefu zaidi kidogo, kisha akainuka.

 

Swahiyh Al-Bukhaariy: Hadiyth: 1228

Mjalada: 2

 

Kitabu: 22

 

Hadiyth: 5

 

 

 

حَدَّثَنَا سُلَيْمَانُ بْنُ حَرْبٍ، حَدَّثَنَا حَمَّادٌ، عَنْ سَلَمَةَ بْنِ عَلْقَمَةَ، قَالَ قُلْتُ لِمُحَمَّدٍ فِي سَجْدَتَىِ السَّهْوِ تَشَهُّدٌ قَالَ لَيْسَ فِي حَدِيثِ أَبِي هُرَيْرَةَ‏.‏

 

Amesimulia Salamah Bin ‘Aqlamah (رضي الله عنه):

 

Nilimuuliza Muhammad (bin Siriyn) iwapo Tashahhud ni lazima isomwe baada ya Sijdah mbili za Sahw. Alijibu: Haimo katika Hadiyth za Abu Hurayrah (رضي الله عنه).

 

Swahiyh Al-Bukhaariy: Hadiyth: 1228b

Mjalada: 2

 

Kitabu: 22

 

Hadiyth: 6

 

 

 

 

 

 

05-Mlango

 

باب مَنْ يُكَبِّرُ فِي سَجْدَتَىِ السَّهْوِ

 

Kutamka Takbyir Katika Sijdah Za Sahw

 

 

 

حَدَّثَنَا حَفْصُ بْنُ عُمَرَ، حَدَّثَنَا يَزِيدُ بْنُ إِبْرَاهِيمَ، عَنْ مُحَمَّدٍ، عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ ـ رضى الله عنه ـ قَالَ صَلَّى النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم إِحْدَى صَلاَتَىِ الْعَشِيِّ ـ قَالَ مُحَمَّدٌ وَأَكْثَرُ ظَنِّي الْعَصْرَ ـ رَكْعَتَيْنِ ثُمَّ سَلَّمَ ثُمَّ قَامَ إِلَى خَشَبَةٍ فِي مُقَدَّمِ الْمَسْجِدِ فَوَضَعَ يَدَهُ عَلَيْهَا وَفِيهِمْ أَبُو بَكْرٍ وَعُمَرُ ـ رضى الله عنهما ـ فَهَابَا أَنْ يُكَلِّمَاهُ وَخَرَجَ سَرَعَانُ النَّاسِ فَقَالُوا أَقَصُرَتِ الصَّلاَةُ وَرَجُلٌ يَدْعُوهُ النَّبِيُّ صلى الله عليه وسلم ذُو الْيَدَيْنِ فَقَالَ أَنَسِيتَ أَمْ قَصُرَتْ فَقَالَ ‏ "‏ لَمْ أَنْسَ وَلَمْ تُقْصَرْ ‏"‏‏.‏ قَالَ بَلَى قَدْ نَسِيتَ‏.‏ فَصَلَّى رَكْعَتَيْنِ ثُمَّ سَلَّمَ ثُمَّ كَبَّرَ فَسَجَدَ مِثْلَ سُجُودِهِ أَوْ أَطْوَلَ، ثُمَّ رَفَعَ رَأْسَهُ فَكَبَّرَ، ثُمَّ وَضَعَ رَأْسَهُ فَكَبَّرَ فَسَجَدَ مِثْلَ سُجُودِهِ أَوْ أَطْوَلَ، ثُمَّ رَفَعَ رَأْسَهُ وَكَبَّرَ‏.‏

 

Amesimulia Abu Hurayrah (رضي الله عنه):   

 

Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) aliswalisha moja ya Swalaah za jioni- Muhammad (msimulizi aliyetangulia) amesema:  “Nadhani ilikuwa Swalaah ya Alasiri-” alimaliza baada ya kuswali Rakaa mbili tu. Kisha akasimama karibu na kipande cha ubao mbele ya Msikiti akaweka mikono juu yake. Abu Bakr na ‘Umar (رضي الله عنهما) walikuwa miongoni mwa watu waliokuweko, lakini hawakuthubutu kusema naye kuhusu hilo (kwa sababu ya heshima kubwa mno wanayomuheshimu). Waliokuwa na haraka wakatoka nje wakasema: “Je, Swalaah hii imepunguzwa?” Mtu ambaye Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alikuwa akimwita   Dhul-Yadayn alimwambia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم): “Je Swalaah hii imepunguzwa, au umesahau?” Akasema: “Sijasahau wala Swalaah haijapunguzwa.” Akasema: “Ni kweli umesahau.” Basi Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akaswali Rakaa mbili, akamalizia kwa Tasliym, kisha akatamka Takbiyr na akaleta Sijdah mbli za Sahw kama za kawaida au ndefu zaidi kidogo, kisha akanyanyua kichwa chake akatamka Takbiyr.

 

Swahiyh Al-Bukhaariy: Hadiyth:1229

Mjalada: 2

 

Kitabu: 22

 

Hadiyth: 7

 

 

 

حَدَّثَنَا قُتَيْبَةُ بْنُ سَعِيدٍ، حَدَّثَنَا لَيْثٌ، عَنِ ابْنِ شِهَابٍ، عَنِ الأَعْرَجِ، عَنْ عَبْدِ اللَّهِ ابْنِ بُحَيْنَةَ الأَسْدِيِّ، حَلِيفِ بَنِي عَبْدِ الْمُطَّلِبِ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَامَ فِي صَلاَةِ الظُّهْرِ وَعَلَيْهِ جُلُوسٌ، فَلَمَّا أَتَمَّ صَلاَتَهُ سَجَدَ سَجْدَتَيْنِ فَكَبَّرَ فِي كُلِّ سَجْدَةٍ وَهُوَ جَالِسٌ قَبْلَ أَنْ يُسَلِّمَ، وَسَجَدَهُمَا النَّاسُ مَعَهُ مَكَانَ مَا نَسِيَ مِنَ الْجُلُوسِ‏.‏ تَابَعَهُ ابْنُ جُرَيْجٍ عَنِ ابْنِ شِهَابٍ فِي التَّكْبِيرِ‏.‏

 

Amesimulia ‘Abdullaah Buhaynah Al-Asdiyy (رضي الله عنه):   

Swahib wa Bani ’Abdul-Muttwalib.

 

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alisimama kwa ajili ya Swalaah ya Adhuhuri. Ilikuwa akae kitako (baada ya Rakaa ya pili, lakini akasimama kuswali Rakaa ya tatu bila kukaa kwa kusoma Tashahhud). Alipomaliza Swalaah akaleta Sijdah mbili na akatamka Takbiyr kwa kila Sijdah wakati amekaa, kabla ya kumaliza Swalaah kwa Tasliym; na watu pia wakaleta Sijdah mbili pamoja naye, (Sajdatus-Sahw ambazo zilikuwa ni) mbadala wa kule kusahau kukaa (kwa ajili ya Tashahhud).

 

Swahiyh Al-Bukhaariy: Hadiyth: 1230

Mjalada: 2

 

Kitabu: 22

 

Hadiyth: 8

 

 

 

 

 

 

06-Mlango

 

 

باب إِذَا لَمْ يَدْرِ كَمْ صَلَّى ثَلاَثًا أَوْ أَرْبَعًا سَجَدَ سَجْدَتَيْنِ وَهْوَ جَالِسٌ

 

Endapo Mtu Atasahau Kama Ameswali Rakaa Tatu Au Mbili Alete Sijdah Mbili Wakati Amekaa Katika Rakaa Yake Ya Mwisho

 

 

 

حَدَّثَنَا مُعَاذُ بْنُ فَضَالَةَ، حَدَّثَنَا هِشَامُ بْنُ أَبِي عَبْدِ اللَّهِ الدَّسْتَوَائِيُّ، عَنْ يَحْيَى بْنِ أَبِي كَثِيرٍ، عَنْ أَبِي سَلَمَةَ، عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ ـ رضى الله عنه ـ قَالَ قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم ‏ "‏ إِذَا نُودِيَ بِالصَّلاَةِ أَدْبَرَ الشَّيْطَانُ وَلَهُ ضُرَاطٌ حَتَّى لاَ يَسْمَعَ الأَذَانَ، فَإِذَا قُضِيَ الأَذَانُ أَقْبَلَ، فَإِذَا ثُوِّبَ بِهَا أَدْبَرَ فَإِذَا قُضِيَ التَّثْوِيبُ أَقْبَلَ حَتَّى يَخْطِرَ بَيْنَ الْمَرْءِ وَنَفْسِهِ يَقُولُ اذْكُرْ كَذَا وَكَذَا مَا لَمْ يَكُنْ يَذْكُرُ حَتَّى يَظَلَّ الرَّجُلُ إِنْ يَدْرِي كَمْ صَلَّى، فَإِذَا لَمْ يَدْرِ أَحَدُكُمْ كَمْ صَلَّى ثَلاَثًا أَوْ أَرْبَعًا فَلْيَسْجُدْ سَجْدَتَيْنِ وَهْوَ جَالِسٌ ‏"‏‏.‏

 

Amesimulia Abu Hurayrah (رضي الله عنه):   

 

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Adhaan ya Swalaah ikinadiwa, shaytwaan hukimbia zake huku akitoa mashuzi ili asiweze kusikia Adhaan. Pindi Adhaan inapomalizika, hurejea.  Iqaamah ikinadiwa, shaytwaan hukimbia tena. Iqaamah ikimalizika hurejea tena, na hujaribu kuingilia nafsi ya mtu kumwambia:  “Kumbuka kadhaa na kadhaa!”  Mambo ambayo hakuwa akiyawaza kabla ya Swalaah. (Shaytwaan huendelea kumshawishi) hadi mtu anayeswali anasahau ameswali Rakaa ngapi. Endapo mmoja wenu hakumbuki kama ameswali Rakaa tatu au nne, basi alete Sijdah mbili za Sahw wakati amekaa.

 

Swahiyh Al-Bukhaariy: Hadiyth: 1231

Mjalada: 2

 

Kitabu: 22

 

Hadiyth: 9

 

 

 

 

 

 

07-Mlango

 

باب السَّهْوِ فِي الْفَرْضِ وَالتَّطَوُّعِ

 

As-Sahw (Usahaulifu) Katika Swalaah Za Faradhi Na Tatwawwu’ (Nawaafil)

 

 

 

وَسَجَدَ ابْنُ عَبَّاسٍ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا سَجْدَتَيْنِ بَعْدَ وِتْرِهِ.

         

Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) alisujudu Sijdah mbili za Sahw baada ya Swalaah ya Witr.

 

 

حَدَّثَنَا عَبْدُ اللَّهِ بْنُ يُوسُفَ، أَخْبَرَنَا مَالِكٌ، عَنِ ابْنِ شِهَابٍ، عَنْ أَبِي سَلَمَةَ بْنِ عَبْدِ الرَّحْمَنِ، عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ ـ رضى الله عنه ـ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَالَ ‏ "‏ إِنَّ أَحَدَكُمْ إِذَا قَامَ يُصَلِّي جَاءَ الشَّيْطَانُ فَلَبَسَ عَلَيْهِ حَتَّى لاَ يَدْرِيَ كَمْ صَلَّى، فَإِذَا وَجَدَ ذَلِكَ أَحَدُكُمْ فَلْيَسْجُدْ سَجْدَتَيْنِ وَهُوَ جَالِسٌ ‏"‏‏.‏

 

Amesimulia Abu Hurayrah (رضي الله عنه):

 

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) amesema: “Mmoja wenu anaposimama kuswali, shaytwaan, huja kumshawishi hadi anasahau ameswali Rakaa ngapi. Basi pindi mmoja wenu ikimfikia hali hiyo, asujudu Sijdah mbili za Sahw wakati amekaa.

 

Swahiyh Al-Bukhaariy: Hadiyth: 1232

Mjalada: 2

 

Kitabu: 22

 

Hadiyth: 10

 

 

 

 

 

08-Mlango

 

باب إِذَا كُلِّمَ وَهُوَ يُصَلِّي فَأَشَارَ بِيَدِهِ وَاسْتَمَعَ

 

Endapo Mtu Anamsemesha Mtu Mwingine Anayeswali, Na Mtu Huyo Anaashiria Kwa Mkono Wake Kuwa Anasikiliza

 

 

 

حَدَّثَنَا يَحْيَى بْنُ سُلَيْمَانَ، قَالَ حَدَّثَنِي ابْنُ وَهْبٍ، قَالَ أَخْبَرَنِي عَمْرٌو، عَنْ بُكَيْرٍ، عَنْ كُرَيْبٍ، أَنَّ ابْنَ عَبَّاسٍ، وَالْمِسْوَرَ بْنَ مَخْرَمَةَ، وَعَبْدَ الرَّحْمَنِ بْنَ أَزْهَرَ ـ رضى الله عنهم ـ أَرْسَلُوهُ إِلَى عَائِشَةَ ـ رضى الله عنها ـ فَقَالُوا اقْرَأْ عَلَيْهَا السَّلاَمَ مِنَّا جَمِيعًا وَسَلْهَا عَنِ الرَّكْعَتَيْنِ بَعْدَ صَلاَةِ الْعَصْرِ وَقُلْ لَهَا إِنَّا أُخْبِرْنَا أَنَّكِ تُصَلِّينَهُمَا وَقَدْ بَلَغَنَا أَنَّ النَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم نَهَى عَنْهَا‏.‏ وَقَالَ ابْنُ عَبَّاسٍ وَكُنْتُ أَضْرِبُ النَّاسَ مَعَ عُمَرَ بْنِ الْخَطَّابِ عَنْهُمَا‏.‏ فَقَالَ كُرَيْبٌ فَدَخَلْتُ عَلَى عَائِشَةَ ـ رضى الله عنها ـ فَبَلَّغْتُهَا مَا أَرْسَلُونِي‏.‏ فَقَالَتْ سَلْ أُمَّ سَلَمَةَ‏.‏ فَخَرَجْتُ إِلَيْهِمْ فَأَخْبَرْتُهُمْ بِقَوْلِهَا فَرَدُّونِي إِلَى أُمِّ سَلَمَةَ بِمِثْلِ مَا أَرْسَلُونِي بِهِ إِلَى عَائِشَةَ‏.‏ فَقَالَتْ أُمُّ سَلَمَةَ ـ رضى الله عنها ـ سَمِعْتُ النَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم يَنْهَى عَنْهَا ثُمَّ رَأَيْتُهُ يُصَلِّيهِمَا حِينَ صَلَّى الْعَصْرَ، ثُمَّ دَخَلَ عَلَىَّ وَعِنْدِي نِسْوَةٌ مِنْ بَنِي حَرَامٍ مِنَ الأَنْصَارِ فَأَرْسَلْتُ إِلَيْهِ الْجَارِيَةَ فَقُلْتُ قُومِي بِجَنْبِهِ قُولِي لَهُ تَقُولُ لَكَ أُمُّ سَلَمَةَ يَا رَسُولَ اللَّهِ سَمِعْتُكَ تَنْهَى عَنْ هَاتَيْنِ وَأَرَاكَ تُصَلِّيهِمَا‏.‏ فَإِنْ أَشَارَ بِيَدِهِ فَاسْتَأْخِرِي عَنْهُ‏.‏ فَفَعَلَتِ الْجَارِيَةُ فَأَشَارَ بِيَدِهِ فَاسْتَأْخَرَتْ عَنْهُ فَلَمَّا انْصَرَفَ قَالَ ‏ "‏ يَا بِنْتَ أَبِي أُمَيَّةَ سَأَلْتِ عَنِ الرَّكْعَتَيْنِ بَعْدَ الْعَصْرِ وَإِنَّهُ أَتَانِي نَاسٌ مِنْ عَبْدِ الْقَيْسِ فَشَغَلُونِي عَنِ الرَّكْعَتَيْنِ اللَّتَيْنِ بَعْدَ الظُّهْرِ فَهُمَا هَاتَانِ ‏"‏‏.‏

 

Amesimulia Kurayb (رضي الله عنه):

 

Ibn ‘Abbaas, Al-Miswar bin Makhramah na ‘Abdur-Rahmana bin Azhar walimpeleka kwenda kwa ‘Aaishah (رضي الله عنها).  Wakamwambia: Mtolee Salaam kutoka kwetu sote kisha muulize kuhusu kuswali Rakaa mbili baada ya Swalaah ya Alasiri na mwambie:  Tuliarifiwa kuwa wewe unaziswali Rakaa mbili baada ya Alasiri ilhali sisi tumejulishwa kwamba Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alikataza kuswaliwa Rakaa hizo.” Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) akasema: “Mimi pamoja na ‘Umar bin Al-Khattwaab (رضي الله عنه) tulikuwa tukiwachapa watu kila walipokuwa wakiziswali.” Kurayb (رضي الله عنه) akasema: Nikaenda kwa ‘Aaishah (رضي الله عنها) na nikamwambia ujumbe huo. ‘Aaishah (رضي الله عنها) akasema: “Nenda kamuulize Ummu Salamah kuhusu hilo.” Kwa hivyo nilirejea nikawaarifu kuhusu maneno yake. Wakaniambia mie niende kwa Ummu Salamah na swali lilo hilo walilonipeleka nalo kwa ‘Aaishah. Ummu Salamah (رضي الله عنها) akajibu: “Nilimsikia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akizikataza. Baadaye nikamuona yeye anaziswali mara baada ya kuswali Alasiri. Kisha akaingia nyumbani kwangu wakati baadhi ya wanawake wa ki-Answaari kutoka katika kabila la Bani Haraam walikuwa wamekaa na mimi. Nikamtuma mjakazi wangu kwake baada ya kumwambia mjakazi huyo: Simama karibu yake na umwambie kuwa Ummu Salamah anakuambia: Ee Rasuli wa Allaah! Nilikusikia unakataza kuswaliwa Rakaa hizi (Rakaa mbili baada ya Swalaah ya Alasiri) lakini mimi nimekuona wewe unaziswali! Akikupungia mkono mngojee.” Yule mjakazi akafanya hivyo. Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akamuashiria kwa mkono, naye akamngojea. Alipomaliza kuswali alisema: “Ee binti wa Bani Umaiyyah! Umeniuliza kuhusu Rakaa mbili baada ya Swalaah ya Alasiri. Watu wa kabila la ‘Abdul-Qays waliniijia wakanishughulisha nikawa sikuswali Rakaa mbili baada ya Swalaah ya Adhuhuri. Hizi Rakaa mbili nilizoziswali sasa hivi ni za zile nilizokosa kuziswali.”

 

Swahiyh Al-Bukhaariy: Hadiyth: 1233

Mjalada: 2

 

Kitabu: 22

 

Hadiyth: 11

 

 

 

 

 

09-Mlango

 

باب الإِشَارَةِ فِي الصَّلاَةِ

 

Kuashiria Wakati Wa Swalaah Kwa Mtu Ambaye Yuko Ndani Ya Swalaah

 

 

 

قَالَهُ كُرَيْبٌ عَنْ أُمِّ سَلَمَةَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا عَنِ النَّبِيِّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ.

 

Hii inatoka kwa Kurayb (رضي الله عنه) kutoka kwa Ummu Salamah (رضي الله عنها) kutoka kwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم).

 

حَدَّثَنَا قُتَيْبَةُ بْنُ سَعِيدٍ، حَدَّثَنَا يَعْقُوبُ بْنُ عَبْدِ الرَّحْمَنِ، عَنْ أَبِي حَازِمٍ، عَنْ سَهْلِ بْنِ سَعْدٍ السَّاعِدِيِّ ـ رضى الله عنه ـ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم بَلَغَهُ أَنَّ بَنِي عَمْرِو بْنِ عَوْفٍ كَانَ بَيْنَهُمْ شَىْءٌ فَخَرَجَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم يُصْلِحُ بَيْنَهُمْ فِي أُنَاسٍ مَعَهُ، فَحُبِسَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم وَحَانَتِ الصَّلاَةُ فَجَاءَ بِلاَلٌ إِلَى أَبِي بَكْرٍ ـ رضى الله عنه ـ فَقَالَ يَا أَبَا بَكْرٍ إِنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم قَدْ حُبِسَ وَقَدْ حَانَتِ الصَّلاَةُ فَهَلْ لَكَ أَنْ تَؤُمَّ النَّاسَ قَالَ نَعَمْ إِنْ شِئْتَ‏.‏ فَأَقَامَ بِلاَلٌ وَتَقَدَّمَ أَبُو بَكْرٍ ـ رضى الله عنه ـ فَكَبَّرَ لِلنَّاسِ وَجَاءَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم يَمْشِي فِي الصُّفُوفِ حَتَّى قَامَ فِي الصَّفِّ، فَأَخَذَ النَّاسُ فِي التَّصْفِيقِ، وَكَانَ أَبُو بَكْرٍ ـ رضى الله عنه ـ لاَ يَلْتَفِتُ فِي صَلاَتِهِ، فَلَمَّا أَكْثَرَ النَّاسُ الْتَفَتَ فَإِذَا رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَأَشَارَ إِلَيْهِ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم يَأْمُرُهُ أَنْ يُصَلِّيَ، فَرَفَعَ أَبُو بَكْرٍ ـ رضى الله عنه ـ يَدَيْهِ فَحَمِدَ اللَّهَ وَرَجَعَ الْقَهْقَرَى وَرَاءَهُ حَتَّى قَامَ فِي الصَّفِّ، فَتَقَدَّمَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فَصَلَّى لِلنَّاسِ فَلَمَّا فَرَغَ أَقْبَلَ عَلَى النَّاسِ فَقَالَ ‏ "‏ يَا أَيُّهَا النَّاسُ مَا لَكُمْ حِينَ نَابَكُمْ شَىْءٌ فِي الصَّلاَةِ أَخَذْتُمْ فِي التَّصْفِيقِ، إِنَّمَا التَّصْفِيقُ لِلنِّسَاءِ، مَنْ نَابَهُ شَىْءٌ فِي صَلاَتِهِ فَلْيَقُلْ سُبْحَانَ اللَّهِ‏.‏ فَإِنَّهُ لاَ يَسْمَعُهُ أَحَدٌ حِينَ يَقُولُ سُبْحَانَ اللَّهِ إِلاَّ الْتَفَتَ، يَا أَبَا بَكْرٍ مَا مَنَعَكَ أَنْ تُصَلِّيَ لِلنَّاسِ حِينَ أَشَرْتُ إِلَيْكَ ‏"‏‏.‏ فَقَالَ أَبُو بَكْرٍ ـ رضى الله عنه ـ مَا كَانَ يَنْبَغِي لاِبْنِ أَبِي قُحَافَةَ أَنْ يُصَلِّيَ بَيْنَ يَدَىْ رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم‏.‏

Amesimulia Sahl Bin Sa’d (رضي الله عنه):

 

Taarifa kuhusu mfarakano miongoni mwa watu wa Bani ‘Amr bin ‘Awf kule Qubaa, zilimfikia Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم). Akatoka kuwaendea pamoja na Swahaba zake ili kufanya suluhu. Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alizuilika kule na wakati wa Swalaah ukawadia. Bilaal akamwendea Abu Bakr (رضي الله عنه) akamwambia: “Ee Abu Bakr! Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) kazuilika kule, na wakati wa kuswali umewadia. Je utawaswalisha watu?” Abu Bakr akajibu: “Naam, ukiwa unataka.” Basi Bilaal akatangaza Iqaamah, na Abu Bakr (رضي الله عنه) akaenda mbele, na watu wakatamka Takbyir. Wakati huo huo, Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akawa anakuja akipenya katika Swaff mpaka akasimama katika Swaff ya kwanza, watu wakaanza kupiga makofi. Abu Bakr (رضي الله عنه) alikuwa hatazami kule wala huku wakati anaswali, lakini watu walivyozidi kupiga makofi, alitazama nyuma akamwona Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم). Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) alimpa ishara aendelee kuswalisha. Abu Bakr (رضي الله عنه) akainyanyua mikono yake akamhimidi Allaah kisha akasogea nyuma mpaka akasimama kwenye Swaff ya kwanza na Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akesogea mbele akawaswalisha watu. Alipomaliza kuswalisha, aliwakhutubia watu akasema: “Enyi watu! Kwa nini mlianza kupiga makofi wakati jambo liliwatokea ninyi ndani ya Swalaah? Kupiga makofi ni kwa wanawake. Pindi mtu anapotaka kutanabahisha jambo katika Swalaah basi aseme: Subhaana-Allaah kwani hakuna (Imaam) ambaye hatageuka atakaposikia (Maamuma) akisema Subhaana-Allaah!”  Kisha Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akamgeukia Abu Bakr (رضي الله عنه) akamuuliza: “Kitu gani kilichokuzuia usiendelee kuwaswalisha watu nilipokuashiria uendelee?” Abu Bakr (رضي الله عنه) akajibu: “Haikhalisi mwana wa Abi Quhaafa kuswalisha Swalaah wakati Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) yupo hapo hapo.”

 

Swahiyh Al-Bukhaariy: Hadiyth: 1234

Mjalada: 2

 

Kitabu: 22

 

Hadiyth: 12

 

 

 

حَدَّثَنَا يَحْيَى بْنُ سُلَيْمَانَ، قَالَ حَدَّثَنِي ابْنُ وَهْبٍ، حَدَّثَنَا الثَّوْرِيُّ، عَنْ هِشَامٍ، عَنْ فَاطِمَةَ، عَنْ أَسْمَاءَ، قَالَتْ دَخَلْتُ عَلَى عَائِشَةَ ـ رضى الله عنها ـ وَهِيَ تُصَلِّي قَائِمَةً وَالنَّاسُ قِيَامٌ فَقُلْتُ مَا شَأْنُ النَّاسِ فَأَشَارَتْ بِرَأْسِهَا إِلَى السَّمَاءِ‏.‏ فَقُلْتُ آيَةٌ‏.‏ فَقَالَتْ بِرَأْسِهَا أَىْ نَعَمْ‏.‏

 

Amesimulia Asmaa (رضي الله عنها):

 

Nilikwenda kwa ‘Aaishah (رضي الله عنها) nikamkuta amesimama anaswali na watu pia wakawa wanaswali. Nikasema: Kimewatokea nini watu? Akaashiria kwa kichwa chake angani. Nikasema: Je, ipo dalili? Akaasjhiria kukubali kwa kichwa akimaanisha kusema: “Naam!”

 

Swahiyh Al-Bukhaariy: Hadiyth: 1235

Mjalada: 2

 

Kitabu: 22

 

Hadiyth: 13

 

 

 

حَدَّثَنَا إِسْمَاعِيلُ، قَالَ حَدَّثَنِي مَالِكٌ، عَنْ هِشَامٍ، عَنْ أَبِيهِ، عَنْ عَائِشَةَ ـ رضى الله عنها ـ زَوْجِ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم أَنَّهَا قَالَتْ صَلَّى رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم فِي بَيْتِهِ وَهُوَ شَاكٍ جَالِسًا، وَصَلَّى وَرَاءَهُ قَوْمٌ قِيَامًا فَأَشَارَ إِلَيْهِمْ أَنِ اجْلِسُوا فَلَمَّا انْصَرَفَ قَالَ ‏ "‏ إِنَّمَا جُعِلَ الإِمَامُ لِيُؤْتَمَّ بِهِ، فَإِذَا رَكَعَ فَارْكَعُوا وَإِذَا رَفَعَ فَارْفَعُوا ‏"‏‏.‏

 

Amesimulia ‘Aaishah (رضي الله عنها):

Mke wa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم)

 

Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) aliswali nyumbani kwake huku amekaa wakati anaumwa, na watu waliomfuata waliswali huku wamesimama, lakini Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akawaashiria nao wakae. Baada ya kumaliza Swalaah akasema: “Imaam anatakiwa kufuatwa. Hivyo anaporukuu nanyi mrukuu, anapoinuka kutoka katika Rukuu nanyi muinuke.  [Rejea Hadiyth namba (1/657) kupata hukum yake].

 

Swahiyh Al-Bukhaariy: Hadiyth: 1236

Mjalada: 2

 

Kitabu: 22

 

Hadiyth: 14

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Share