057-Asbaabun-Nuzuwl: Al-Israa Aayah 057: أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ يَدْعُونَ يَبْتَغُونَ إِلَىٰ رَبِّهِمُ الْوَسِيلَةَ أَيُّهُمْ أَقْرَبُ وَيَرْجُونَ رَحْمَتَهُ

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

 

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

017-Asbaab Nuzuwl Suwrah Al-Israa Aayah 56-57

 

 

 

Kauli Zake Allaah (سبحانه وتعالى):

 

قُلِ ادْعُوا الَّذِينَ زَعَمْتُم مِّن دُونِهِ فَلَا يَمْلِكُونَ كَشْفَ الضُّرِّ عَنكُمْ وَلَا تَحْوِيلًا ﴿٥٦﴾

Sema: Iteni wale ambao mnadai (ni waabudiwa) pasi Naye, basi hawamiliki kukuondesheeni dhara na wala kuihamisha (kwa mwengine).

 

 

أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ يَدْعُونَ يَبْتَغُونَ إِلَىٰ رَبِّهِمُ الْوَسِيلَةَ أَيُّهُمْ أَقْرَبُ وَيَرْجُونَ رَحْمَتَهُ وَيَخَافُونَ عَذَابَهُ ۚ إِنَّ عَذَابَ رَبِّكَ كَانَ مَحْذُورًا ﴿٥٧﴾

Hao wanaowaomba (wao wenyewe) wanatafuta kwa Rabb wao njia ya kujikurubisha, yupi miongoni mwao awe karibu zaidi na wanataraji rahmah Yake, na wanakhofu adhabu Yake. Hakika adhabu ya Rabb wako ni ya kutahadhariwa daima. [Al-Israa: 56- 57]

 

Sababun-Nuzuwl: 

 

 

حَدَّثَنَا أَبُو بَكْرِ بْنُ أَبِي شَيْبَةَ، حَدَّثَنَا عَبْدُ اللَّهِ بْنُ إِدْرِيسَ، عَنِ الأَعْمَشِ، عَنْ إِبْرَاهِيمَ، عَنْ أَبِي مَعْمَرٍ، عَنْ عَبْدِ اللَّهِ، فِي قَوْلِهِ عَزَّ وَجَلَّ ‏: ((أُولَئِكَ الَّذِينَ يَدْعُونَ يَبْتَغُونَ إِلَى رَبِّهِمُ الْوَسِيلَةَ أَيُّهُمْ أَقْرَبُ‏))‏ قَالَ كَانَ نَفَرٌ مِنَ الْجِنِّ أَسْلَمُوا وَكَانُوا يُعْبَدُونَ فَبَقِيَ الَّذِينَ كَانُوا يَعْبُدُونَ عَلَى عِبَادَتِهِمْ وَقَدْ أَسْلَمَ النَّفَرُ مِنَ الْجِنِّ ‏.‏

 

Ametuhadithia Abuu Bakkr bin Abiy Shaybah, ametuhadithia ‘Abdullaah bin Idriys, kutoka kwa Al-A’mash, kutoka kwa Ibraahiym, kutoka kwa Abuu Ma’mar, kutoka kwa ‘Abdullaah kuhusu kauli Yake Allaah (عز وجل):

 

أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ يَدْعُونَ يَبْتَغُونَ إِلَىٰ رَبِّهِمُ الْوَسِيلَةَ أَيُّهُمْ أَقْرَبُ وَيَرْجُونَ رَحْمَتَهُ  

Hao wanaowaomba (wao wenyewe) wanatafuta kwa Rabb wao njia ya kujikurubisha, yupi miongoni mwao awe karibu zaidi na wanataraji rahmah Yake, 

 

Amesema:  Kulikuwa na kundi la majini walisilimu lakini walikuwa wakiabudiwa, na wale waliowaabudu wakaendeea kuwaabudu ilhali majini hao walioabudiwa walisilimu.   

 

 

Na katika Riwaayah nyengine,

 

عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ، مَسْعُودٍ ‏((‏أُولَئِكَ الَّذِينَ يَدْعُونَ يَبْتَغُونَ إِلَى رَبِّهِمُ الْوَسِيلَةَ))‏ قَالَ: نَزَلَتْ فِي نَفَرٍ مِنَ الْعَرَبِ كَانُوا يَعْبُدُونَ نَفَرًا مِنَ الْجِنِّ فَأَسْلَمَ الْجِنِّيُّونَ وَالإِنْسُ الَّذِينَ كَانُوا يَعْبُدُونَهُمْ لاَ يَشْعُرُونَ فَنَزَلَتْ: ((أُولَئِكَ الَّذِينَ يَدْعُونَ يَبْتَغُونَ إِلَى رَبِّهِمُ الْوَسِيلَةَ‏)) مسلم‏

Kutoka kwa ‘Abdullaah bin Mas’uwd kuhusu Aayah:

 

 

أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ يَدْعُونَ يَبْتَغُونَ إِلَىٰ رَبِّهِمُ الْوَسِيلَةَ

Hao wanaowaomba (wao wenyewe) wanatafuta kwa Rabb wao njia ya kujikurubisha...

 

Kasema: Imeteremka kuhusu kundi la Waarabu walikuwa wakiabudu kundi katika majini. Majini hao walisilimu lakini watu waliendelea kuwaabudu bila ya wao kuhisi. Ikateremka:

 

أُولَـٰئِكَ الَّذِينَ يَدْعُونَ يَبْتَغُونَ إِلَىٰ رَبِّهِمُ الْوَسِيلَةَ

Hao wanaowaomba (wao wenyewe) wanatafuta kwa Rabb wao njia ya kujikurubisha…  [Muslim]

 

Na Riwaayah katika Al-Bukhaariy

 

عَنْ عَبْدِ اللَّهِ رضى الله عنه فِي هَذِهِ الآيَةِ: ((‏الَّذِينَ يَدْعُونَ يَبْتَغُونَ إِلَى رَبِّهِمِ الْوَسِيلَةَ‏))‏ قَالَ نَاسٌ مِنَ الْجِنِّ كَانُوا‏‏ يُعْبَدُونَ فَأَسْلَمُوا‏.‏

البخاري

Kutoka kwa ‘Abdullaah bin Mas’uwd amesema kuhusu Aayah hii:

 

الَّذِينَ يَدْعُونَ يَبْتَغُونَ إِلَىٰ رَبِّهِمُ الْوَسِيلَةَ

Wale wanaowaomba (wao wenyewe) wanatafuta kwa Rabb wao njia ya kujikurubisha…

 

Imeteremshwa kuhusu baadhi ya majini waliokuwa wakiabudiwa na binaadamu. Kisha (majini hao) wakasilimu (lakini watu wakaendelea kuwaabudu). [Al-Bukhaariy Kitaab At-Tafsiyr]

 

 

Share