Skip navigation.
Home kabah

Mbaazi

 

Vipimo

 

Mbaazi za kopo (pigeon peas)                40 fl oz (vikopo viwili) (Vikombe vitatu)

Ikiwa mbaazi kavu                                  3 Vikombe

Tui la nazi zito                                          1 Kikombe 

Kitunguu                                                   1

Chumvi                                                      kiasi

Pilipili mbichi                                              2

 

 

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

 

1.       Ikiwa ni mbaazi kavu, roweka katika maji kwa muda wa masaa kisha chemsha hadi ziwive.

2.       Ikiwa ni mbaazi za kopo, mwaga maji yake ya kopo umimine katika sufuria.

3.       Kata vitunguu na utie katika mbaazi.

4.      Tia tui, chumvi, pililipili mbichi upike hadi kwa muda mdogo tu hadi tui lipunguke kidogo, zitakuwa tayari kuliwa.

 

     Maandazi - Tazama Vipimo Vyake kwenye 'Mikate '