11-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Kuongezeka Mikono Katika Chakula

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب تكثير الأيدي عَلَى الطعام

11-Mlango Wa Kuongezeka Mikono Katika Chakula

 

Alhidaaya.com

 

 

Hadiyth – 1

عن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : قَالَ رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((  طَعَامُ الاثنينِ كافِي الثلاثةِ ، وطَعَامُ الثَّلاَثَةِ كافي الأربعة )) متفق عَلَيْهِ .

Imepokewa kutoka kwa Abuu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: "Chakula cha wawili kinawatosha watatu, na cha watatu kinawatosha wanne." [Al-Bukhaariy, Muslim, Maalik na At-Tirmidhiy]

 

 

Hadiyth – 2

وعن جابر رضي الله عنه ، قَالَ : سَمِعْتُ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، يقول : ((  طَعَامُ الوَاحِدِ يَكْفِي الاثْنَيْنِ ، وَطَعَامُ الاثْنَيْنِ يَكْفِي الأَرْبَعَةَ ، وَطَعَامُ الأرْبَعَةِ يَكْفِي الثَّمَانِيَةَ )) رواه مسلم .

Amesema Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nimemsikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: "Chakula cha mmoja kinawatosha wawili, na cha wa wawili kinawatosha wanne, na cha wanne kinawatosha wanane." [Muslim]

 

 

 

Share