Imaam Shurayh Al-Qaadhwiy: Ninapopatwa Msiba Humshukuru Allaah Kwa Mambo Manne

Ninapopatwa Msiba Humshukuru Allaah Kwa Mambo Manne

 

Imaam Shurayh Al-Qaadhwiy (Rahimahu Allaah)

 

Alhidaaya.com

 

 

 

Amesema Imaam Shurayh Al-Qaadhwiy (Rahimahu Allaah)

 

 

“Ninapopatwa na msiba ninamhimidi Allaah  kwa mambo manne:

 

1.Nashukuru kama ikiwa hakuna kubwa zaidi ya hilo

 

 

2.Nashukuru nikiruzukiwa subira juu yake

 

 

3. Nashukuru ikiwa Allaah Ataniwezesha kutaja neno la Al-Istirjaa nikitaraji thawabu kwa Allaah

 

4.Na ninashukuru ikiwa msiba haujaweza kuharibu dini yangu."

 

[Siyar A’laam An-Nubalaa: (7/112)]

 

 

Al-Istirjaa ni kusema unapopatwa msiba wowote:

 

إِنّا للهِ وَإِنَا إِلَـيْهِ رَاجِعُـونَ

Innaa liLLaahi wa innaa Ilayhi raaji’uwn,  

 

Hakika sisi wa Allaah, na hakika sisi Kwake wenye kurejea.

 

 

 

Share