13-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Karaha ya Kunywa Kutoka Kwa Mdomo wa Kiriba na Mfano Wake na Kubainisha Kuwa Hii ni Karaha Si Ile Ambayo ni Haramu

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب كراهة الشرب من فم القربة ونحوها وبيان أنه كراهة تنـزيه لا تحريم

13-Mlango Wa Karaha ya Kunywa Kutoka Kwa Mdomo wa Kiriba na Mfano Wake na Kubainisha Kuwa Hii ni Karaha Si Ile Ambayo ni Haramu

 

Alhidaaya.com

 

 

Hadiyth – 1

عن أَبي سعيدٍ الْخُدْريِّ رضي الله عنه ، قَالَ : نَهَى رسول الله صلى الله عليه وسلم عن اخْتِنَاثِ الأَسْقِيَةِ . يعني : أن تُكْسَرَ أفْواهُها ، وَيُشْرَبَ مِنْهَا . متفق عَلَيْهِ .

Abu Sa'iyd Al-Khudriy (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'anhu) amekataza kuvikunja viriba vya maji, anakusudia kuikunja midomo hiyo." [Al-Bukhaariy, Muslim, Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy]

 

 

Hadiyth – 2

وعن أَبي هريرة رضي الله عنه ، قَالَ : نَهَى رسول الله صلى الله عليه وسلم أن يُشْرَبَ مِنْ فِيِّ السِّقَاءِ أَوْ القِرْبَةِ . متفق عَلَيْهِ .

Amesema Abu Huraiyrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza kunywa kutoka kwa mdomo wa kiriba." [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

Hadiyth – 3

وعن أم ثابتٍ كَبْشَةَ بنتِ ثابتٍ أُختِ حَسَّانَ بن ثابتٍ رضي الله عنهما ، قالت : دخل عَلَيَّ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم فَشَرِبَ مِنْ فيِّ قِرْبَةٍ مُعَلَّقَةٍ قَائِماً ، فَقُمْتُ إِلَى فِيهَا فَقَطَعْتُهُ . رواه الترمذي ، وقال : (( حديث حسن صحيح )) .

Ummu Thaabit Kabshah bint Thaabit (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) dadake Hassaan bin Thaabit (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Aliingia kwangu Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na akanywa kutoka kwa mdomo wa kiriba kilichotundikwa akiwa amesimama. Nilisimama na kuukata mdomo wa kiriba hicho na kuuhifadhi." [At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh].

 

 

 

Share