07-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Mume Kumtolea Salamu Mkewe na Mwanamke Kuwasalimia Maharimu Zake na kwa Kuwatolea Salamu Wageni Wanaume au Wanawake Ikiwa Hapana Hofu ya Fitna na Kuwasalimia kwa Sharti Hili

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب سلام الرجل على زوجته والمرأة من محارمه

وعلى أجنبية وأجنبيات لا يخاف الفتنة بهن وسلامهن بهذا الشرط

07-Mlango Wa Mume Kumtolea Salamu Mkewe na Mwanamke Kuwasalimia Maharimu Zake na kwa Kuwatolea Salamu Wageni Wanaume au Wanawake Ikiwa Hapana Hofu ya Fitna na Kuwasalimia kwa Sharti Hili

 

Alhidaaya.com

 

 

Hadiyth – 1

عن سهل بن سعدٍ رضي الله عنه ، قال : كَانَتْ فِينَا امْرَأةٌ – وفي رواية : كَانَتْ لَنَا عَجُوزٌ – تَأخُذُ مِنْ أصُولِ السِّلْقِ فَتَطْرَحُهُ فِي القِدْرِ ، وَتُكَرْكِرُ حَبَّاتٍ مِنْ شَعِيرٍ ، فَإذَا صَلَّيْنَا الْجُمُعَةَ ، وَانْصَرَفْنَا ، نُسَلِّمُ عَلَيْهَا ، فَتُقَدِّمُهُ إلَيْنَا . رواه البخاري .

Amesema Sahl bin Sa'd (Radhwiya Allaahu 'anhu): Kulikuwa na mwanamke kwetu, na katika riwaayah nyenginemwanamke mzee, ambaye alikuwa akitia katika chungu mizizi ya viazi vitamu na akiongeza shayiri kidogo na kuzipika pamoja. Tulipomaliza Swalaah ya Ijumaa na kutoka, tulikuwa tunamtolea salamu, naye alikuwa akitupatia chakula hicho." [Al-Bukhaariy]

 

 

Hadiyth – 2

وعن أُم هَانِىءٍ فاخِتَةَ بنتِ أَبي طالب رضي الله عنها ، قالت : أتيت النبيَّ صلى الله عليه وسلم يَوْمَ الفَتْحِ وَهُوَ يَغْتَسِلُ ، وَفَاطِمَةُ تَسْتُرُهُ بِثَوْبٍ ، فَسَلَّمْتُ ... وَذَكَرَتِ الحديث . رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwaUmmu Haani' Faakhitah bint Abu Twaalib (Radhwiya Allaahu 'anhaa) ambaye amesema: Nilikuja kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) siku ya ufunguzi (Kutekwa kwa Makkah) akiwa anaoga na Faatwimah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amemsitiri kwa nguo (aliyoishika kumziba asionekane). Nilimtolea salamu na nikaitaja Hadiyth. [Muslim]

 

 

Hadiyth – 3

وعن أسماءَ بنتِ يزيدَ رضي الله عنها ، قالت : مَرّ عَلَيْنَا النّبيُّ صلى الله عليه وسلم فِي نِسوَةٍ فَسَلَّمَ عَلَيْنَا . رواه أَبُو داود والترمذي ، وقال : (( حديث حسن )) ، وهذا لفظ أَبي داود .

ولفظ الترمذي : أنَّ رسول الله صلى الله عليه وسلم مَرَّ في المَسْجِدِ يَوْماً ، وَعُصْبَةٌ مِنَ النِّسَاءِ قُعُودٌ ، فَأَلْوَى بِيَدِهِ بالتَّسْلِيمِ .

Amesema Asmaa' bint Yaziyd (Radhwiya Allaahu 'anhu): Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipita kwenye kikundi cha wanawake na akatutolea salamu." [Abu Daawuwd na At-Tirmidhiy, na akasema ni Hadiyth Hasan]

 

 

 

Share