08-Riyaadhw Asw-Swaalihiyn: Mlango Wa Anayosema Baada ya Kumfumba Macho Maiti

 

Riyaadhw Asw-Swaalihiyn

 

باب مَا يقوله بعد تغميض الميت

08-Mlango Wa Anayosema Baada ya Kumfumba Macho Maiti

 

Alhidaaya.com

 

 

عن أُم سلمة رضي الله عنها ، قالت : دَخَلَ رسولُ الله صلى الله عليه وسلم عَلَى أَبي سَلَمة وَقَدْ شَقَّ بَصَرُهُ ، فَأغْمَضَهُ ، ثُمَّ قَالَ : (( إنَّ الرُّوحَ إِذَا قُبِضَ ، تَبِعَهُ البَصَرُ )) فَضَجَّ نَاسٌ مِنْ أهْلِهِ ، فَقَالَ : (( لاَ تَدْعُوا عَلَى أنْفُسِكُمْ إِلاَّ بِخَيْرٍ ، فَإنَّ المَلاَئِكَةَ يَؤمِّنُونَ عَلَى مَا تَقُولُونَ )) ثُمَّ قَالَ : (( اللَّهُمَّ اغْفِرْ لأَبِي سَلَمَة ، وَارْفَعْ دَرَجَتْهُ في المَهْدِيِّينَ ، وَاخْلُفْهُ في عَقِبهِ في الغَابِرِينَ ، وَاغْفِرْ لَنَا وَلَهُ يَا رَبَّ العَالَمِينَ ، وَافْسَحْ لَهُ في قَبْرِهِ ، وَنَوِّرْ لَهُ فِيهِ )) رواه مسلم .

Imepokewa kutoka kwake Ummu Salamah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) amesema: Aliingia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa Abu Salamah (Radhwiya Allaahu 'anhu) macho yake yapo wazi (alipofariki) akayafumba kisha akasema: "Roho inapotolewa macho huifuata." Watu katika watu wake wakapiga, kelele, Nabiy akawambia: "Msiombee nafsi zenu isipokuwa kheri, kwani Malaaikah wanaitikia Aamiyn kwa hayo mnayosema." Kisha akasema: "Ee Mola wangu! Msamehe Abu Salamah na inua daraja yake katika walioongoka, na mbadilishie kizazi chake katika waliopita. Na utusamehe sisi na yeye ee Mola wa Ulimwengu, na mkunjulie kaburi lake, na linawirishe ndani yake." [Muslim]

 

 

Share