039-Maswali 200 Na Majibu Ya ‘Aqiydah: Ni Ipi Dalili Ya Kuzidiana Iymaan Kwa Wenye Kuamini?

 

200 سُؤالٌ وَ جَوَابٌ فِي الْعَقِيدَة

Maswali 200 Na Majibu Ya ‘Aqiydah

 

لِلشَّيخ حافِظ بن أحْمَد الحَكمَيّ

Shaykh Haafidhw Bin Ahmad Al-Hakamiyy (رحمه الله)

Imefasiriwa na:  Alhidaaya.com

 

039-Ni Ipi Dalili Ya Kuzidiana Iymaan Kwa Wenye Kuamini?

 

 

Swali:

 

س: ما الدليل على تفاضل أهل الإيمان فيه

 

Ni ipi dalili ya kuzidiana iymaan kwa wenye kuamini?

 

Jibu:

 

ج: قال تعالى( والسابقون السابقون أولئك المقربون )-إلى-( وأصحاب اليمين ما أصحاب اليمين )وقال تعالى( فأما إن كان من المقربين فروح وريحان وجنة نعيم وأما إن كان من أصحاب اليمين فسلام لك من أصحاب اليمين )وقال تعالى( فمنهم ظالم لنفسه ومنهم مقتصد ومنهم سابق بالخيرات بإذن الله )الآيات, وفي حديث الشفاعة( أن الله يخرج من النار من كان في قلبه وزن دينار من إيمان ,ثم من كان في قلبه نصف دينار من إيمان )- وفي رواية يخرج من النار من قال لا إله إلا الله وكان في قلبه من الخير ما يزن شعيرة ثم يخرج من النار من قال لا إله إلا الله وكان في قلبه من الخير ما يزن برة ثم يخرج من النار من قال لا إله إلا الله وكان في قلبه من الخير ما يزن ذرة .

 

 

Ni kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى):

 

وَالسَّابِقُونَ السَّابِقُونَ ﴿١٠﴾

Na waliotangulia mbele, watatangulia mbele.

أُولَـٰئِكَ الْمُقَرَّبُونَ ﴿١١﴾

Hao ndio watakaokurubishwa.

Mpaka katika kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى):

وَأَصْحَابُ الْيَمِينِ مَا أَصْحَابُ الْيَمِينِ ﴿٢٧﴾

Na watu wa kuliani, je, ni nani watu wa kuliani? [Al-Waaqi'ah: (56:10-27)]

 

Na kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى):

فَأَمَّا إِن كَانَ مِنَ الْمُقَرَّبِينَ ﴿٨٨﴾

Basi akiwa miongoni mwa waliokurubishwa.

فَرَوْحٌ وَرَيْحَانٌ وَجَنَّتُ نَعِيمٍ ﴿٨٩﴾

Basi mapumziko ya raha na manukato na Jannah ya neema.

وَأَمَّا إِن كَانَ مِنْ أَصْحَابِ الْيَمِينِ ﴿٩٠﴾

Na kama akiwa miongoni mwa watu wa kuliani.

فَسَلَامٌ لَّكَ مِنْ أَصْحَابِ الْيَمِينِ ﴿٩١﴾

Basi (ataambiwa): Salaam juu yako uliye katika watu wa kuliani. [Al-Waaqi'ah: (56:88-91)]

 

Na kauli ya Allaah (سبحانه وتعالى):

 

ثُمَّ أَوْرَثْنَا الْكِتَابَ الَّذِينَ اصْطَفَيْنَا مِنْ عِبَادِنَا ۖ فَمِنْهُمْ ظَالِمٌ لِّنَفْسِهِ وَمِنْهُم مُّقْتَصِدٌ وَمِنْهُمْ سَابِقٌ بِالْخَيْرَاتِ بِإِذْنِ اللَّـهِ ۚ  ﴿٣٢﴾

Kisha Tukawarithisha Kitabu wale Tuliowakhitari miongoni mwa Waja Wetu. Basi miongoni mwao yupo mwenye kudhulumu nafsi yake, na miongoni mwao yupo aliye wastani, na miongoni mwao yupo aliyesabiki kwa mambo mengi ya kheri kwa Idhini ya Allaah. [Faatwir: (35:32)]

 

Na katika Hadiyth ya Shifaa:

 

“Hakika Allaah Atamtoa mtu motoni mwenye nusu dinari ya Iymaan”. [Imepokewa na Al-Bukhaariy (7439) na Muslim (183)].

 

Na katika riwaayah nyingine:

 

“Atatolewa motoni mwenye kusema hapana Mungu ila Allaah, na akawa moyoni mwake kuna kheri ya uzani wa shayiri, kisha atatoka mwenye kutamka shahaadah na katika moyo wake kuna uzani wa kheri Mfano punje ya ngano, kisha atatolewa mwenye kutamka Shahaadah na ndani ya moyo wake kuna uzani wa kheri, mfano wa punje ya mahindi”. [Imepokewa na Muslim (193)-Kitaabul-Imaan].

 
 
 
Share