062-Asbaabun-Nuzuwl: Al Jumu'ah Aayah 06: وَآخَرِينَ مِنْهُمْ لَمَّا يَلْحَقُوا بِهِمْ

 

أسْبابُ النُّزُول

Asbaabun-Nuzuwl

Sababu Za Kuteremshwa (Baadhi Ya  Suwrah Na Aayaat Za Qur-aan)

 

Imekusanywa na: Alhidaaya.com

 

062-Al-Jumu’ah Aayah 6

 

 

 

Kauli Yake Allaah (سبحانه وتعالى): 

وَآخَرِينَ مِنْهُمْ لَمَّا يَلْحَقُوا بِهِمْ ۚ وَهُوَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ﴿٣﴾

“Na wengineo ambao bado hawajakutana nao. Naye Ndiye Mwenye Enzi ya Nguvu Asiyeshindika, Mwenye Hikmah wa yote.” [Al-Jumu’a (62:3)]

 

 

Sababun-Nuzuwl:

 

حَدَّثَنِي عَبْدُ الْعَزِيزِ بْنُ عَبْدِ اللَّهِ، قَالَ حَدَّثَنِي سُلَيْمَانُ بْنُ بِلاَلٍ، عَنْ ثَوْرٍ، عَنْ أَبِي الْغَيْثِ، عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ، رضى الله عنه قَالَ كُنَّا جُلُوسًا عِنْدَ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم فَأُنْزِلَتْ عَلَيْهِ سُورَةُ الْجُمُعَةِ ‏ وَآخَرِينَ مِنْهُمْ لَمَّا يَلْحَقُوا بِهِمْ قَالَ قُلْتُ مَنْ هُمْ يَا رَسُولَ اللَّهِ فَلَمْ يُرَاجِعْهُ حَتَّى سَأَلَ ثَلاَثًا، وَفِينَا سَلْمَانُ الْفَارِسِيُّ، وَضَعَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم يَدَهُ عَلَى سَلْمَانَ ثُمَّ قَالَ ‏"‏ لَوْ كَانَ الإِيمَانُ عِنْدَ الثُّرَيَّا لَنَالَهُ رِجَالٌ ـ أَوْ رَجُلٌ ـ مِنْ هَؤُلاَءِ ‏"‏‏.‏

 

Amesimulia Abul-Ghayth (رضي الله عنه) kutoka kwa Abuu Hurayrah (رضي الله عنه): Tulikuwa tumeketi pamoja na Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) akateremshiwa Suwrah Al-Jumu’ah:

وَآخَرِينَ مِنْهُمْ لَمَّا يَلْحَقُوا بِهِمْ ۚ وَهُوَ الْعَزِيزُ الْحَكِيمُ﴿٣﴾

“Na wengineo ambao bado hawajakutana nao. Naye Ndiye Mwenye Enzi ya Nguvu Asiyeshindika, Mwenye Hikmah wa yote.” [Al-Jumu’a (62:3)]

 

Nikauliza: Ni akina nani hao Ee Rasuli wa Allaah? Hakunijibu mpaka nilipomuuliza mara ya tatu. Na kati yetu alikuwapo Salmaan Al-Faarisiyy (رضي الله عنه). Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) akaweka mkono wake juu ya Salmaan, kisha akasema: “Lau kama imaan ingalikuwa kwenye ath-thurayyaa (mojawapo wa sayari) wangaliifikia watu (au) mtu katika watu hawa (yaani jamaa za akina Salmaan Al-Faarisiyy).” [Al-Bukhaariy Kitabu Cha Tafsiyr (65)]

 

Share