26-Al-Arba’uwn An-Nawawiyyah: Kila Kiungo Cha Mtu Lazima Kitolewe Swadaqah

 

Al-Arba’uwn An-Nawawiyyah:

 

Hadiyth Ya 26

 

كُلُّ سُلامَى مِنَ النَّاسِ عليه صَدَقَةٌ

 

Kila Kiungo Cha Mtu Lazima Kitolewe Swadaqah

 

Alhidaaya.com

 

 

 

Sikiliza Hadiyth:

 

 

عن أَبي هُرَيْرَةَ رَضي اللهُ عنه قال: قالَ رسُولُ الله صلى الله عليه وسلم: ((كُلُّ سُلامَى مِنَ النَّاسِ عليه صَدَقَةٌ، كُلُّ يَوْمٍ تَطْلُعُ فِيهِ الشَّمْسُ: تَعْدِلُ بَيْنَ اثْنَيْنِ صَدَقَةٌ، وتُعينُ الرَّجُلَ في دَابَّتِهِ فَتَحْمِلُهُ عَلَيْها أو تَرْفَعُ لهُ عَلَيْها متَاَعَهُ صَدَقَةٌ، والْكَلِمةُ الطَّيِّبةُ صَدَقَةٌ، وبكُلِّ خَطْوَةٍ تَمشِيها إلى الصَّلاةِ صَدَقَةٌ، وتُمِيطُ الأَذَى عنِ الطَّرِيِق صَدَقَةٌ)) رَوَاهُ الْبُخَارِيُّ وَمُسْلِمٌ   

 

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Kila kiungo cha mtu lazima akitolee swadaqah kila siku linapochomoza jua. Kufanya uadilifu baina ya wawili ni swadaqah. Kumsaidia mtu kupanda mnyama wake kwa kumsaidia  kumnyanyua  au kumnyanyulia  mizigo ni swadaqah. Neno zuri ni swadaqah. Na kila hatua unayotembea kuelekea Swalaah ni swadaqah, na kuondosha udhia katika njia ni swadaqah.” [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

 

Share