35-Al-Arba’uwn An-Nawawiyyah: Msihusudiane Msizidishiane Bei Msibughudhiane

 

Al-Arba’uwn An-Nawawiyyah:

 

Hadiyth Ya 35

 

لا تَحَاسَدُوا، ولا تَنَاجَشُوا، ولا تَباغَضُوا

 

Msihusudiane Msizidishiane Bei Msibughudhiane

 

 

Alhidaaya.com

 

Sikiliza Hadiyth:

 

 

عن أبي هُريرةَ رضي اللهُ عنه قال: قال رسوُل الله صلى الله عليه وسلم: ((لا تَحَاسَدُوا، ولا تَنَاجَشُوا، ولا تَباغَضُوا، ولا تَدَابَرُوا، ولا يَبعْ بَعْضُكُمْ على بَيْعِ بَعْضٍ، وكُونُوا عِبادَ اللهِ إخْوَاناً، المُسْلمُ أَخُو المُسْلمِ: لا يَظْلِمُهُ، وَلَا يَخْذُلُهُ، ولا يَكْذِبُهُ، ولا يَحْقِرُهُ، التَّقْوَى هاهُنا - ويُشِيرُ إلى صَدْرِه ثَلاثَ مَرَّاتٍ، بِحَسْبِ امْرِىءٍ مِنَ الشَّرِّ أن يَحْقِرَ أخاهُ المُسْلِمَ، كُلُّ المُسْلِمِ على الْمسْلِم حَرَامٌ: دَمُهُ ومالُهُ وعِرْضُهُ)) رَوَاهُ مُسْلِمٌ  

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Msihusudiane, wala msizidishiane bei (biashara), wala msibughudhiane, wala msitengane, wala msishindane kwa kupunguza bei.  Lakini enyi waja wa Allaah kuweni ndugu. Muislamu ni ndugu wa Muislamu mwenzake, hamdhulumu wala hamtelekezi, wala hamuongopei, wala hamdharau.  Taqwa iko hapa.” (huku akiashiria kifuani kwake kwa vidole vyake) mara tatu. “Ni uovu wa kutosha kwa mtu kumdharau ndugu yake Muislamu. Muislamu ameharamishiwa kwa Muislamu mwenzake: damu yake, mali yake na heshima yake.” [Muslim]

 

 

Share