22-Abu Bakr Asw-Swiddiyq (Radhwiya Allaahu 'anhu): Kufariki Kwake

Abu Bakr (Radhiya Allaahu ‘anhu) alikuwa Khalifya hwa mwanzo wa Waislamu na alikuwa amiri wa mwanzo aliyetumwa na Mtume wa Mwenyezi Mungu kuongoza msafara wa Hajj katika mwaka wa tisa wa Hijri, na alikuwa wa mwanzo kuikusanya Qur-aan na kuiandika katika kitabu kimoja baada ya hapo mwanzo kuwa iliandikwa ndani ya majani, mifupa, vigogo vya miti nk..

Alikuwa akiruhusiwa na Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam) yeye na 'Umar bin Al-Khatwtwaab (Radhiya Allaahu ‘anhu) kutoa fatwa hata wakati wa uhai wake Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam).

Alifariki dunia siku ya Jumatatu mwezi 13 Jumaadal-Aakhir mwaka wa 13 wa Hijri mwafaka na mwezi wa Agusti mwaka wa 634 akiwa na umri wa miaka 63, na baba yake alifariki baada yake kwa kiasi cha miezi sita.

 

Share