07-Fatwa: Inafaa Kutoa Zakaatul-Fitwr Kwa Familia Ya Mkewe Ambao Wanahitaji?

 

Je, Inafaa Kutoa Zakaatul-Fitwr Kwa Familia Ya Mkewe Ambao Wanahitaji?

www.alhidaaya.com

 

 

SWALI:

 

Inafaa kutoa Zakaatul-Fitwr kwa familia ya mke wangu ambao wanahitaji?

 

 

JIBU:

 

AlhamduliLLaah,

 

Zakaatul-Fitwr itolewe kwa masikini na wanaohitaji kwa sababu Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) amesema: "Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alifaradhisha Zakaatul-Fitwr kuwapa masikini iwe kama ni kutakasa Swawm ya mfungaji kutokana na maneno ya upuuzi na machafu" [Imesumiliwa na Abuu Daawuwd [1609] na ikapewa daraja ya Hasan na An-Nawawiy katika al-Majmuu' [6/126] na Imaam Al-Albaaniy katika Swahiyh Abi Daawuwd]

 

Ikiwa familia ya mke wako ni masikini na wenye kuhitaji, hakuna ubaya kuwapa Zakaatul-Fitwr, bali ni bora zaidi kuliko kuwapa wengine kwa sababu familia ya mke wako (wakwe, mashemeji, mawifi) wana haki kuwahudumia kama ni sehemu ya kumheshimu mke na kumtendea wema na upole. 

 

Imaam Ibn 'Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) amesema katika An-Nuwr 'alaa ad-Darb [682]:

 

"Hakuna shaka kwamba wakwe, mashemeji na mawifi wana haki ambazo ni zaidi ya mtu mwengine yeyote" [mwisho wa kunukuu]

  

Na Allaah Anajua zaidi

 

 

Share