12-Fatwa: Kutoa Kiwango Cha Zakaatul-Fitwr Katika Vyama Vya Misaada Mwanzo Wa Ramadhwaan

Kutoa Kiwango Cha Zakaatul-Fitwr Katika Vyama Vya Misaada Mwanzo Wa Ramadhwaan

 

www.alhidaaya.com

 

 

 

SWALI:

 

Vyama vya misaada vinaruhusiwa kupokea Zakaatul-Fitwr mwanzo wa Ramadhwaan ili waweze kuigawa kwa mpangilio mzuri kabisa?

 

JIBU:

 

Sifa Zote Ni Za Allaah

 

Ikiwa hakuna watu masikini katika eneo au wale watakaopokea hawaihitajii hasa, na hawatoila bali wataiuza kwa nusu ya thamani yake, na ikiwa ni tabu kupata maskini na wanaohitaji watakaoila, hivyo inaruhusiwa kuituma nje ya nchi. Inaruhusiwa kutoa thamani (ya Zakaatul-Fitwr) mwanzo wa mwezi kwa dalali ambaye atainunua (Zakaatul-Fitwr) na kuituma kwa watu wanaostahiki wakati huo unapotakiwa kulipwa, ambao ni usiku kabla ya 'Iyd au siku mbili kabla yake.

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

[Al-Fataawa Al-Jibriyn fil A'maal Ad-Da'wiyyah li Fadhwiylat Ash-Shaykh 'Abdillaah bin Jibriyn Uk. 33]

 

 

Share