16-Imaam Ibn ‘Uthaymiyn: Inafaa Mtoto Wa Kike Kumlipa Baba Yake Zakaatul-Fitwr?

Inafaa Mtoto Wa Kike Kumlipa Baba Yake Zakaatul-Fitwr?

 

Imaam Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu Allaah)

 

www.alhidaaya.com

 

 

SWALI:

 

Mtoto wa kike anaweza kumlipia baba yake Zakaatul-Fitwr?

 

JIBU:

 

Imaam Ibn 'Uthaymiyn (Rahimahu- Allaah) amesema:

 

Yeyote anayelipa Zakaatul-Fitwr kwa mtu na ambaye hakuwajibika kumlipia lazima achukue ruhusa yake. Hivyo ikiwa Zayd anamlipia 'Amr bila ya ruhusa yake, itakuwa ni batili, kwa sababu Zayd hakuwajibika kumlipia 'Amr Zakaatul-Fitwr.

 

Ni muhimu kwamba niyyah sahihi itiwe ikiwa kwa ajili ya kujitolea mtu binafsi au kumlipia mtu mwignine. Hii ni kutokana na hukmu inayojulikana sana kwa Fuqahaa ambao wameiita 'taswarruf al-fudhwuwl' ikimaanishwa suala wakati mtu anamfanyia mwenziwe kitendo bila ya ruhusa yake, je huwa kitendo kinasihi kikamilifu au inategemea ruhusa na ridhaa ya mtu mwengine? 

 

Kuna ikhtilaaf baina ya ‘Ulamaa katika mas-ala haya. Na rai iliyo sahihi kabisa ni kwamba inasihi ikiwa mtu mwengine ametoa ruhusa. Na Shaykh amenukuu Hadiyth ya Abu Hurayrah alipozungumza na Shaytwaan alipokuwa akiilinda Zakaah.

 

Hii inathibitisha suala kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amekubali kitendo cha Shaytwaan alichomfanyia Abuu Hurayarah na akakichukulia kuwa kimesihi japokuwa iliyochukuliwa ilikuwa ni kutoka katika Zakaah na Abu Hurayrah alipewa majukumu ya kuilinda na sio mtu mwengine.

[Ash-Sharh Al-Mumti' 6/165]

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

 

Share